WIMBO 36
Tulinde Moyo Wetu
Maandishi
1. Tuulinde moyo wetu;
Tuepuke zambi.
Mungu anajua mambo
Yote ya mu moyo.
Moyo unaweza
Kutuongoza mubaya.
Basi tumutii Mungu
na tulinde moyo.
2. Tumutafute Yehova
Kwa kusali sana.
Kila siku tumusifu,
na kumushukuru.
Tufuate mambo yenye
Anatufundisha.
Na tumufurahishe kwa
Moyo wetu wote.
3. Tuepuke mawazo ya
Kuchafua moyo.
Tuache Neno ya Mungu
Itutie nguvu.
Mungu anapenda watu
Washikamanifu.
Tutamuabudu yeye
Mu maisha yote.