WIMBO 137
Wanamuke Wenye Imani
Maandishi
1. Hana, Maria, Sara, na wengine
Walikuwa na imani kabisa.
Walimuogopa sana Yehova.
Kuko tena wanamuke wengine
Wenye walimupenda Yehova,
Lakini Biblia haikuwataya.
2. Wale wanamuke walikuwa na
Upendo, uhodari, na imani,
Na sifa zingine za kuvutia.
Na leo tunaona dada zetu
Wenye kuwa washikamanifu.
Basi tuwaige, tutabarikiwa.
3. Wajane na mama na dada zetu,
Muko natumika kwa nguvu sana.
Muko wapole, tena watiifu.
Mujue, Yehova anawapenda.
Tunasali awasaidie
Ili musichoke, na mubarikiwe.
(Ona pia Flp. 4:3; 1 Ti. 2:9, 10; 1 Pe. 3:4, 5.)