SOMO YA 55
Usaidie Kutaniko Yako
Mu dunia yote, mamilioni ya watu wanamuabudu Yehova kwa furaha mu maelfu ya makutaniko. Wako wenye shukrani sana juu mule wanapata mafundisho na muongozo. Na wako na hamu sana ya kufanya mambo mbalimbali juu ya kusaidia kutaniko. Na weye unapenda kusaidia kutaniko yako?
1. Namna gani unaweza kutumia wakati na nguvu yako juu ya kusaidia kutaniko?
Siye wote tunaweza kusaidia kutaniko. Kwa mufano, kama mu kutaniko yenu muko ndugu na dada wenye kuzeeka ao walemavu, unaweza kuwasaidia kufika ku mikutano. Ao unaweza kuwasaidia kufanya mambo ingine, sawa vile kuenda kuwauzia vitu ku soko ao kuwafanyia kazi za ku nyumba. (Soma Yakobo 1:27.) Tena, tunaweza kujitolea juu ya kusaidia kusafisha na kutunza Jumba ya Ufalme. Hakuna mutu mwenye anatukazaka kufanya ile mambo. ‘Tunajitoa kwa kujipendea’ juu tunapenda Mungu na ndugu na dada zetu.—Zaburi 110:3.
Mashahidi wa Yehova wenye kubatizwa wanaweza kusaidia kutaniko mu njia zingine. Ndugu wenye wanatimiza mambo yenye Maandiko inaomba wanaweza kuwa watumishi wa huduma na hata kufikia kuwa wazee. Na ndugu na dada, wote wanaweza kusaidia kazi ya kuhubiri iendelee kwa kufanya kazi ya upainia. Mashahidi fulani wanaweza kusaidia kujenga nafasi ya kuabudia ao kuhamia mu eneo kwenye kutaniko iko na lazima ya musaada.
2. Namna gani tunaweza kutumia makuta yetu na vitu vyetu juu ya kusaidia kutaniko?
Tunaweza ‘kumuheshimia Yehova kupitia vitu vyetu vyenye samani.’ (Mezali 3:9) Ni pendeleo sana kutoa makuta yetu na vitu vingine juu ya kusaidia kutaniko na kazi ya kuhubiri iendelee mbele. (Soma 2 Wakorinto 9:7.) Michango yetu inatumiwaka pia juu ya kutolea ndugu na dada misaada wakati wa magumu. Watu fulani wanaamuaka kukuwa ‘naweka kitu fulani pembeni’ kwa ajili ya muchango. (Soma 1 Wakorinto 16:2.) Tunaweza kutia michango yetu mu visanduku vya michango vyenye vinakuwaka fasi kwenye tunakusanyikiaka. Ao tunaweza kutoa kupitia Enternete ku donate.jw.org. Yehova anatupatia nafasi ya kuonyesha kama tunamupenda kupitia namna tunatumia makuta yetu na vitu vyetu.
TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI
Tuone mambo fulani yenye unaweza kufanya juu ya kusaidia kutaniko.
3. Tunaweza kutoa michango
Yehova na Yesu wanapenda wale wenye wanatoa kwa furaha. Kwa mufano, Yesu alisifu mujane maskini mwenye alitoa muchango, hata kama alitoa makuta kidogo sana. Musome Luka 21:1-4, na kisha muzungumuzie hii maulizo:
Ni lazima tutoe makuta mingi juu Yehova afurahi?
Yehova na Yesu wanajisikiaka namna gani wakati tunatoa kwa kujipendea?
Juu ya kuona namna michango inatumiwaka, muangalie VIDEO. Kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.
Namna gani michango inatumiwaka juu ya kusaidia makutaniko mu dunia yote?
4. Tunaweza kujitolea juu ya kusaidia kazi mbalimbali
Zamani, watumishi wa Yehova walikuwa natumika sana juu ya kutunza fasi ya ibada. Ni kweli kama walikuwa wanatoa michango, lakini kuko mambo ingine yenye walikuwa wanafanya. Musome 2 Mambo ya Nyakati 34:9-11, na kisha muzungumuzie hii ulizo:
Kila Mwisraeli alifanya nini juu ya kusaidia kutunza nyumba ya Yehova ao fasi ya ibada?
Juu ya kuona namna Mashahidi wa Yehova wanafuata mufano wa watumishi wa Yehova wa zamani, muangalie VIDEO. Kisha muzungumuzie maulizo yenye kufuata.
Juu ya nini ni muzuri kusaidia ili Jumba ya Ufalme iendelee kuwa safi na mu hali ya muzuri?
Unaweza kufanya nini juu ya kusaidia?
5. Ndugu wanaweza kujikaza juu wafikie kufanya mambo mingi zaidi mu kutaniko
Biblia inatia moyo wanaume Wakristo wafanye yao yote juu ya kusaidia kutaniko. Juu ya kuona mufano, muangalie VIDEO. Kisha muzungumuzie ulizo yenye kufuata.
Vile uliona mu video, Ryan alifanya nini juu afikie kusaidia kutaniko zaidi?
Biblia inaonyesha mambo yenye ndugu wanapaswa kutimiza juu wafikie kuwa watumishi wa huduma na wazee. Musome 1 Timoteo 3:1-13, na kisha muzungumuzie hii maulizo:
Ndugu wenye wanapenda kuwa watumishi wa huduma na wazee, wanapaswa kutimiza mambo gani?
Familia zao zinapaswa kuwa namna gani? —Ona mustari wa 4 na 11.
Wakati ndugu anajikaza kutimiza mambo yenye Maandiko inaomba, ile inaletea watu wote mu kutaniko faida gani?
KAMA MUTU ANAULIZA: “Mashahidi wa Yehova wanatoshaka wapi makuta ya kusaidia kazi yao iendelee?”
Utamujibia nini?
KWA KIFUPI
Yehova anafurahi sana wakati tunajikaza kutumikisha wakati yetu, nguvu yetu, na vitu vyetu juu ya kusaidia kutaniko.
Maulizo ya kujikumbusha
Namna gani tunaweza kutumia wakati yetu na nguvu yetu juu ya kusaidia kutaniko?
Namna gani tunaweza kutumia makuta yetu na vitu vyetu juu ya kusaidia kutaniko?
Unapenda kufanya nini juu ya kusaidia kutaniko?
HABARI ZINGINE
Ona juu ya nini Mungu halombake tena watumishi wake watoe sehemu ya kumi.
“Biblia Inasema Nini Juu ya Kutoa Sehemu ya Kumi?” (Inapatikana ku Enternete)
Biblia inaonyesha kama kuko kazi fulani zenye ndugu wenye kubatizwa tu njo wanapaswa kufanya. Lakini itakuwa namna gani kama dada mwenye kubatizwa analazimika kufanya zile kazi?
“Ukichwa mu Kutaniko” (Munara wa Mulinzi wa Mwezi wa 2, 2021)
Ona namna Mashahidi fulani wenye bidii, wanajikazaka sana juu ya kufikishia waabudu wenzao vichapo.
Namna Vichapo Vinapelekwa Katika Maeneo ya Mbali ya Congo (4:25)
Tofauti na matengenezo ingine ya kidini, ona namna tunapataka makuta ya kuendelesha kazi yetu.
“Mashahidi wa Yehova Wanatosha Feza Wapi? (Inapatikana ku Enternete)