MAISHA YA MUKRISTO
“Zawadi kwa Ajili ya Yehova”
Namna gani tunaweza “kuja leo tukiwa na zawadi katika mukono kwa ajili ya Yehova”? (1Ny 29:5, 9, 14) Hapa chini kuko njia mbalimbali zenye tunaweza kutumia ili kutoa michango ya kujipendea ili kutegemeza kazi ya Mashahidi wa Yehova mu inchi yetu na mu dunia yote.
MICHANGO YENYE TUNATOA KUPITIA JW.ORG AO KUPITIA VISANDUKU VYA MICHANGO INATENGEMEZA:
KAZI YA KUHUBIRI MU DUNIA YOTE
kazi ya kujenga na kazi mbalimbali kwenye biro ya tawi na katika biro za kutafsiri
masomo mbalimbali ya kiteokrasi
watumishi wa pekee wa wakati wote
halmashauri za kutoa misaada
kazi ya kuchapisha, kufanya video, na vichapo vya kielektronike
GARAMA ZA KUTANIKO
garama kidogo-kidogo za kutaniko na kutunza na kutengeneza Jumba la Ufalme
azimio lolote lenye kutaniko linafanya ili kutumia biro ya tawi feza ya kutegemeza:
kazi ya kujenga Majumba ya Ufalme na Majumba ya Mikusanyiko mu dunia yote
programu ya mu Dunia Yote Kuhusu Misaada
kazi zingine zenye tunafanya mu dunia yote
MIKUSANYIKO MBALIMBALI
Michango yenye tunatoa ku mikusanyiko ya eneo inatiwa mu michango kwa ajili ya kazi yenye tunafanya mu dunia yote. Kisha, feza zenye tunatumia ku mikusanyiko ya eneo, ya pekee, na ya kimataifa zinachukuliwa mu michango kwa ajili ya kazi yenye tunafanya mu dunia yote.
Michango yenye inatolewa kwenye mikusanyiko ya muzunguko inatumiwa ili kulipia, kutumikisha, na kutengeneza mahali pa kufanyia mikusanyiko hiyo na garama zingine za muzunguko. Muzunguko unaweza kuamua kutuma feza ya ziada mu michango kwa ajili ya kazi yenye Mashahidi wa Yehova wanafanya mu dunia yote.