Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w11 1/9 uku. 30-31
  • Ashtakiwa kwa Uwongo!

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ashtakiwa kwa Uwongo!
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jinsi ya Kukataa Kishawishi
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Musa Apokea Mgawo wa Pekee
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Mungu Anayechukia Ukosefu wa Haki
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Thamini Mambo Matakatifu!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
w11 1/9 uku. 30-31

Kwa Ajili Ya Vijana

Ashtakiwa kwa Uwongo!

YOSEFU​—SEHEMU YA 2

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika matukio yanayozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama wahusika wakuu wanavyohisi. Wazia kwamba masimulizi haya ni halisi kabisa.

Wahusika wakuu: Yosefu, Potifa, na mke wake

Muhtasari: Yosefu afungwa gerezani isivyo haki, lakini Yehova yuko pamoja naye.

1 CHUNGUZA TUKIO HILI.​—SOMA MWANZO 39:7, 10-23.

Unatambua hisia gani katika sauti ya mke wa Potifa anapomshtaki Yosefu kwa uwongo?

․․․․․

Eleza kuhusu nyumba ya gereza kama unavyoiwazia.

․․․․․

Mwanzoni, Yosefu alitendewa jinsi gani alipokuwa gerezani? (Dokezo: Ona Zaburi 105:17, 18.)

․․․․․

2 CHIMBA ZAIDI.

Kama Yosefu hangekuwa na imani yenye nguvu, angefanya uamuzi gani mbaya alipokuwa gerezani? (Dokezo: Ona Ayubu 30:20, 21.)

․․․․․

Tunajuaje kwamba Yosefu hakumlaumu Yehova kwa kufungwa gerezani? (Dokezo: Ona Mwanzo 40:8; 41:15, 16.)

․․․․․

Unafikiri ni sifa gani zilizomsaidia Yosefu kuvumilia alipofungwa gerezani isivyo haki? (Dokezo: Soma na utafakari maandiko yanayofuata: Mika 7:7; Luka 14:11; Yakobo 1:4.)

․․․․․

Yosefu alipata mazoezi gani gerezani, na huenda mazoezi hayo yalimsaidia jinsi gani baadaye maishani? (Dokezo: Ona Mwanzo 39:21-23; 41:38-43.)

․․․․․

3 TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Baraka ambazo wale wanaovumilia wanapata.

․․․․․

Mazoezi ambayo unaweza kupata unapovumilia hali ngumu.

․․․․․

Utegemezo wa Yehova unapojaribiwa.

․․․․․

NJIA NYINGINE UNAYOWEZA KUTUMIA MAMBO HAYO.

Je, umewahi kujikuta katika hali ya mfadhaiko, bila mtu wa kukusaidia? Huenda Yehova alikusaidia kwa njia gani ulipokuwa ukipambana na jaribu hilo? (Dokezo: Soma na utafakari andiko la 1 Wakorintho 10:13.)

․․․․․

4 NI MAMBO GANI KATIKA SIMULIZI HILI AMBAYO YAMEKUGUSA MOYO SANA, NA KWA NINI?

․․․․․

Ikiwa huna Biblia, waombe Mashahidi wa Yehova wakupe moja, au soma habari zaidi katika Intaneti www.watchtower.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine