Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w12 1/11 uku. 16-17
  • Je, Mungu Ataleta Serikali Moja Itakayotawala Dunia Yote?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Mungu Ataleta Serikali Moja Itakayotawala Dunia Yote?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Ni Nani Mufalme wa Ufalme wa Mungu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2020
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 1/11 uku. 16-17

Neno la Mungu Linafundisha Nini?

Je, Mungu Ataleta Serikali Moja Itakayotawala Dunia Yote?

Habari hii inazungumuzia maulizo fulani ambayo labda umekwisha kujiuliza na inaonyesha mahali ambapo unaweza kupata majibu katika Biblia. Mashahidi wa Yehova watafurahi kukusaidia upate majibu ya maulizo hayo.

1. Sababu gani watu wana lazima ya serikali ao guvernema moja tu duniani pote?

Leo, watu wana magumu duniani pote. Katika inchi fulani, watu wengi ni masikini na wanaonewa. Katika inchi zingine, watu wengi wana vitu vingi zaidi ya vile wanavyohitaji. Dunia ikitawaliwa na serikali moja tu, mali ya dunia inaweza kugawanywa sawasawa.​—Soma Mhubiri 4:1; 8:9.

2. Ni nani anayestahili kuongoza serikali ya dunia yote?

Wazo la kusema dunia yote itawaliwe na serikali moja halipendeze watu wengi kwa sababu hakuna mutu anayeweza kutawala vizuri. Hakuna mutu anayeweza kukubaliwa na watu wote. Tena, watu wanapopata mamlaka, wanaitumia vibaya. Watu wanaogopa kama mutu mumoja tu akitawala dunia yote, anaweza kutesa watu wote na kuwaonea.​—Soma Methali 29:2; Yeremia 10:23.

Yehova Mungu amemuchagua Yesu, Mwana wake, ili atawale watu milele. (Luka 1:32, 33) Yesu anajua magumu ya watu. Alipokuwa hapa duniani, aliponyesha wagonjwa, alifundisha watu wapole, na alipitisha wakati pamoja na watoto. (Marko 1:40-42; 6:34; 10:13-16) Kwa hiyo, Yesu ndiye Mutawala anayestahili kabisa.​—Soma Yohana 1:14.

3. Je, inawezekana kabisa serikali moja itawale dunia yote?

Mungu amemufanya Mwana wake kuwa Mufalme ili atawale dunia akiwa mbinguni. (Danieli 7:13, 14) Kwa mufano, mutawala wa inchi hakae katika kila muji wa inchi anayotawala, vilevile Yesu hahitaji kukaa duniani ili kutawala watu.​—Soma Mathayo 8:5-9, 13.

Je, watu wote watakubali kutawaliwa na Yesu? Hapana. Ni wale tu wanaopenda mema ndio watamukubali. Yehova ataondoa duniani wale wote wanaokataa Mutawala mwenye upendo na haki ambaye amechagua.—Soma Mathayo 25:31-33, 46.

4. Mutawala wa dunia yote atafanya nini?

Kama vile muchungaji anavyokusanya kondoo zake, Yesu ameanza kukusanya watu wapole wa mataifa yote na kuwafundisha njia za Mungu za upendo. (Yohana 10:16; 13:34) Kwa bidii, watu kama hao wanamuunga Yesu mukono na utawala wake. (Zaburi 72:8; Mathayo 4:19, 20) Duniani pote, watu waaminifu wanaotawaliwa na Yesu wanatangaza kwa umoja kama Yesu amekuwa Mufalme.​—Soma Mathayo 24:14.

Hivi karibuni, Yesu atatumia nguvu zake ili kuondoa serikali mbaya za leo zinazowatesa watu. Amechagua watu fulani kati ya wafuasi wake waaminifu ili watawale dunia pamoja naye wakiwa mbinguni. (Danieli 2:44; 7:27) Kupitia Ufalme wake, Yesu atajaza ujuzi juu ya Yehova duniani pote na kurudisha paradiso iliyopotea hapo mwanzoni.​—Soma Isaya 11:3, 9; Mathayo 19:28.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 8 ya kitabu hiki, Biblia Inafundisha Kabisa Nini?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine