Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/7 uku. 7
  • Je, Kuna Dini Yoyote Ambayo Unaweza Kutumainia?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Kuna Dini Yoyote Ambayo Unaweza Kutumainia?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna Gani Naweza Kupata Dini ya Kweli?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Sababu Gani Unapaswa Kuichunguza Dini Yako?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Mwisho wa Dini ya Uwongo Unakaribia!
    Misho wa Dini ya Uwongo Unakaribia!
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/7 uku. 7

Je, Kuna Dini Yoyote Ambayo Unaweza Kutumainia?

Ikiwa kuna dini fulani ambayo imekuvunja moyo, inaweza kuwa vigumu kwako kutumainia dini yoyote. Lakini uwe na uhakika kwamba kuna dini ambayo unaweza kutumainia. Yesu alipokuwa duniani, aliunda kikundi cha wafuasi waaminifu na akawafundisha kuishi kupatana na kanuni za Mungu. Wafuasi wa kweli wa Kristo ni watu waaminifu wanaojikaza kuishi kupatana na kanuni za Kikristo. Unaweza kuwapata katika dini gani?

Estelle, aliyetajwa katika habari iliyotangulia, anasema hivi: “Mwishowe, nilianza sasa kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Sikukawia kuelewa maana ya andiko la Yohana 8:32, ambalo linasema hivi: ‘Mutaijua kweli, nayo kweli itawaweka ninyi huru.’”

Ray, ambaye anatajwa pia katika habari iliyotangulia, anasema hivi: “Nilipojifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova, nilijifunza kwamba si Mungu ndiye anawaletea watu mateso. Nilifurahia kujua kwamba hata kama Mungu ana sababu nzuri inayofanya aache watu waendelee kuteseka, anaahidi pia kuondoa mateso hivi karibuni.

Ni wazi kwamba ni vigumu kufanya mambo mazuri katika dunia ya leo ambamo watu wengi wana mwenendo mubaya. Lakini inawezekana kuwa na mwenendo muzuri. Watu wengi wana lazima ya musaada ili kuelewa mafundisho ya Biblia na kuyafuata katika maisha yao. Ndiyo maana, katika dunia yote, Mashahidi wa Yehova wanafundisha mamilioni ya watu Biblia nyumbani bila kulipwa. Kila juma, watu wengi wanajifunza mambo ambayo Biblia inafundisha kabisa. Hilo linafanya wanamukaribie Muumbaji wao na kufanya maisha yao yawe yenye furaha zaidi.a

Uwaulize Mashahidi wa Yehova sababu gani wanatumainia dini yao

Wakati utakutana na Mashahidi wa Yehova, uwaulize sababu gani wanatumainia dini yao. Uchunguze mafundisho yao na ikiwa mambo ambayo wanafanya yanapatana na kanuni za Kikristo. Kisha, uamue wewe mwenyewe ikiwa kuna dini ambayo unaweza kutumainia.

a Ili kupata habari zingine, soma kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine