Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp16 na. 4 uku. 16
  • Biblia Inasema Nini?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Biblia Inasema Nini?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ni mwanadamu alianzisha dini?
  • Ni jambo la maana kuwa katika dini fulani?
  • Dini
    Amuka!—2014
  • Ni Lazima Kabisa Kuwa mu Dini Fulani?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Namna Gani Naweza Kupata Dini ya Kweli?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Dini Inayokubaliwa na Mungu
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
wp16 na. 4 uku. 16

Biblia Inasema Nini?

Ni mwanadamu alianzisha dini?

WATU FULANI WANAAMINI kwamba ni mwanadamu alianzisha dini; wengine wanawaza kwamba Mungu anatumia dini ili kusaidia watu wamukaribie. Wewe unawaza namna gani?

MAMBO BIBLIA INASEMA

Kuna “ibada [ao, dini] iliyo safi na isiyotiwa unajisi [ao, uchafu] kwa maoni ya Mungu wetu na Baba.” (Yakobo 1:27) Dini safi ao ya kweli inatoka kwa Mungu.

BIBLIA INATUFUNDISHA TENA NINI?

  • Ili tumupendeze Mungu, dini yetu inapaswa kutegemea kweli ya Biblia.—Yohana 4:23, 24.

  • Dini zenye kutegemea mawazo ya watu hazina faida yoyote.—Marko 7:7, 8.

Ni jambo la maana kuwa katika dini fulani?

UNAWEZA KUJIBU NINI?

  • Ndiyo

  • Hapana

  • Inalingana na hali

MAMBO BIBLIA INASEMA

“Acheni tufikiriane ili kuchocheana katika upendo na matendo mazuri, bila kuacha kukusanyika pamoja.” (Waebrania 10:24, 25) Mungu anataka waabudu wake wakusanyike pamoja katika kikundi chenye kupangwa muzuri.

BIBLIA INATUFUNDISHA TENA NINI?

  • Wale wenye wanaabudu Mungu wanapaswa kuungana katika imani.—1 Wakorintho 1:10, 11.

  • Wale wenye kuwa katika dini yenye Mungu anakubali wanafanya familia moja ya ndugu na dada duniani pote.—1 Petro 2:17.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 15 ya kitabu hiki, chenye kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova

Kinapatikana pia kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org/swc

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine