Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • ijwbq habari 90
  • Ni Lazima Kabisa Kuwa mu Dini Fulani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ni Lazima Kabisa Kuwa mu Dini Fulani?
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jibu ya Biblia
  • Biblia Inasema Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Dini
    Amuka!—2014
  • Namna Gani Naweza Kupata Dini ya Kweli?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Dini Inayokubaliwa na Mungu
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
ijwbq habari 90
Kikundi ya watu wenye wamekutana juu ya kumuabudu Mungu

Ni Lazima Kabisa Kuwa mu Dini Fulani?

Jibu ya Biblia

Ndiyo. Mungu anapenda watu wakutane juu ya kumuabudu. Biblia inasema hivi: “Tufikiriane ili kutiana moyo katika upendo na matendo ya muzuri, bila kuacha kukutana pamoja.”​—Waebrania 10:24, 25, maelezo ya chini.

Yesu alionyesha kama wanafunzi wake wangefanyiza kikundi yenye kupangwa muzuri wakati aliwaambia hivi: “Kwa jambo hili wote watajua kama ninyi ni wanafunzi wangu​—kama muko na upendo kati yenu.” (Yohana 13:35) Juu ya kuonyesha ule upendo, wanafunzi wa Yesu walipaswa kukutana pamoya na waamini wenzao. Walipaswa kupangwa mu makutaniko na kukutana pamoya kwa ukawaida juu ya kumuabudu Mungu. (1 Wakorinto 16:19) Na wote, mu dunia yote, wangefanyiza familia moya ya Kikristo.​—1 Petro 2:17.

Zaidi ya kuwa mu dini fulani, mutu anapaswa kufanya nini ingine?

Biblia inasema kama watu wanapaswa kukutana pamoya juu ya kumuabudu Mungu. Lakini haiseme kama mutu anakubaliwa na Mungu juu tu iko mu dini fulani. Juu mutu akubaliwe na Mungu, dini yake inapaswa kumusaidia atumikishe kanuni za Mungu mu maisha yake ya kila siku. Kwa mufano, Biblia inasema hivi: “Dini yenye kuwa safi na yenye haina uchafu kwa maoni ya Mungu wetu na Baba ni hii: kuhangaikia mayatima na wajane katika taabu yao, na kuendelea kubakia bila doa kutokana na ulimwengu.”​—Yakobo 1:27, maelezo ya chini.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine