Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/9 uku. 16
  • Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unaweza Kufanya Nini ili Familia Yako Ikuwe na Furaha?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Linda Ndoa Yako
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
  • Ndoa Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • Mufanye Ndoa Yenu Ikuwe Yenye Nguvu na Yenye Furaha
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/9 uku. 16
[Picha kwenye ukurasa wa 16]

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Unaweza kufanya nini ili ndoa yako iwe yenye furaha?

Shauri la Biblia juu ya kufanya ndoa iwe yenye furaha lina matokeo mazuri kwa sababu linatoka kwa Yule aliyeanzisha ndoa, Yehova Mungu. Biblia inatufundisha tukomalishe sifa ambazo zinaweza kufanya ndoa yetu iwe yenye furaha na inatuonya juu ya tabia ambazo zinaweza kuharibu ndoa. Pia inatufundisha ufundi wa kupashana habari ambao unaongeza furaha katika ndoa.​—Soma Wakolosai 3:8-10, 12-14.

Bwana na bibi wanapaswa kuheshimiana. Ikiwa wote wawili wanakubali madaraka ambayo Mungu amewapatia katika ndoa, wanaweza kuwa wenye furaha.​—Soma Wakolosai 3:18, 19.

Ni nini kinachofanya ndoa idumu?

Bibi na bwana waliooana wanaweza kuendelea kukaa pamoja ikiwa wanapendana. Mungu anatufundisha namna ya kupendana. Mungu na Mwana wake, Yesu, ni mifano mizuri ya upendo wa kujitoa kwa ajili ya wengine.​—Soma 1 Yohana 4:7, 8, 19

Ikiwa bibi na bwana wanaheshimu ndoa kwa kuiona kuwa mupango wa Mungu, wanaweza kuendelea kukaa pamoja. Mungu aliumba ndoa uwe muungano wenye kudumu kati ya mwanaume na mwanamuke ili familia ziwe na usalama. Ndoa inaweza kudumu kwa sababu Mungu aliumba wanaume na wanawake ili wasaidiane kwa kutimiziana mahitaji ya kimwili na ya moyoni. Pia aliwaumba kwa mufano wake, wakiwa na uwezo wa kuiga upendo wake.​—Soma Mwanzo 1:27; 2:18, 24.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 14 ya kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza pia kuchukua kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine