Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb21 Mwezi wa 1 uku. 5
  • Linda Ndoa Yako

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Linda Ndoa Yako
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maisha ya Kisha Siku ya Ndoa
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • Maulizo juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Matatizo Si Mwisho wa Ndoa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Namna Mukristo Anaweza Kufanya Ndoa Yake Ikuwe ya Muzuri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2021
mwb21 Mwezi wa 1 uku. 5
Bwana anaikala chini, pembeni ya bibi yake na iko na furaha wakati iko anamusaidia kufua manguo.

MAISHA YA MUKRISTO

Linda Ndoa Yako

Yehova anaona naziri ya ndoa kuwa jambo nzito. Anasema kama bwana anapaswa kushikamana na bibi yake, na bibi anapaswa kushikamana na bwana yake. (Mt 19:5, 6) Kuko watumishi mingi wa Mungu wenye kuwa na ndoa yenye furaha. Lakini, hakuna ndoa yenye inakamilika. Magumu haikosake mu ndoa. Watu mingi wanasema kama juu ya kumaliza magumu mu ndoa, inaomba bibi na bwana watengane ao wavunje ndoa. Lakini sisi hatupaswe kuwa na mawazo ya vile. Bibi na bwana Wakristo wanapaswa kufanya nini ili kulinda ndoa yao?

Fikiria hii mambo tano:

  1. Ulinde moyo wako kwa kuepuka kujifurahisha na mambo ya uasherati na uepuke kuchezea wengine kimapenzi. Ile mambo inaletaka tu magumu mu ndoa.​—Mt 5:28; 2Pe 2:14.

  2. Ufanye urafiki wako pamoja na Mungu ukuwe nguvu, na ukuwe na tamaa ya kumufurahisha Mungu mu ndoa yako.​—Zb 97:10.

  3. Uvae utu mupya na umufanyie bibi ao bwana yako mambo fulani ya kidogo-kidogo ya muzuri yenye itafanya akupende sana.​—Kol 3:8-10, 12-14.

  4. Uzoee kuzungumuza na mwenzako kwa heshima na ujikaze ili mazungumuzo yenu ikuwe yenye kujenga.​—Kol 4:6.

  5. Umupatie bwana ao bibi yako haki yake. Ufanye vile kwa upendo sana.​—1Ko 7:3, 4; 10:24.

Wakati Wakristo wanaheshimia ndoa, ile inaonyesha kama wanaheshimia Yehova, mwenye aliianzisha.

MUANGALIE VIDEO TUNAPASWA “KUKIMBIA KWA UVUMILIVU”​—KIMBIA KWA KUTII SHERIA, NA KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:

  • Picha yenye inatoka mu video ‘Tunapaswa ‘Kukimbia kwa Uvumilivu’​—Kimbia kwa Kutii Sheria.’ Ndugu Calou na dada Calou wanacheka kisha hotuba yao ya arusi mu Jumba la Ufalme.

    Hata kama ku mwanzo ndoa inaweza kuwa muzuri, ni magumu gani inaweza kutokea?

  • Picha yenye inatoka mu video ‘Tunapaswa ‘Kukimbia kwa Uvumilivu’​—Kimbia kwa Kutii Sheria.’ Ndugu Calou na dada Calou wako wanazungumuzia magumu yao kwa upole. Wako na Biblia yenye kuwa wazi ku meza.

    Namna gani kanuni zenye kuwa mu Biblia zinaweza kusaidia ule mwenye anaona kama bibi ao bwana yake hamupendi tena sana?

  • Picha yenye inatoka mu video ‘Tunapaswa ‘Kukimbia kwa Uvumilivu’​—Kimbia kwa Kutii Sheria.’ Ndugu Calou iko anasomea bibi yake na watoto wake wawili wanamuke habari fulani yenye kuwa mu ‘Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia.’

    Mutumikishe kanuni za Biblia ili ndoa yenu ikuwe na furaha

    Ni kanuni gani zenye bibi na bwana wanapaswa kufuata?

  • Bibi na bwana wanapaswa kufanya nini ili ndoa yao ikuwe na furaha?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine