Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/6 uku. 16
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mungu Anaahidi Kama Dunia Itaokoka Kabisa
    Amuka!—2023
  • Habari Zenye Kuwa mu Hii Gazeti
    Amuka!—2023
  • Watu Wataharibisha Dunia Kabisa-Kabisa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/6 uku. 16

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Dunia yetu iliumbwa kwa kusudi fulani?

Kijana mwanaume anaangalia rangi mbalimbali za vitu vinavyotuzunguka

Dunia ilikusudiwa kuwa makao yenye furaha kwa ajili ya wanadamu

Dunia yetu inastahili kabisa kutegemeza uzima. Ina maji mengi, yaliyo ya lazima kwa uzima. Mwinamo, mwendo na muzunguko wa dunia, vyote vinastahili kabisa ili kuzuia bahari zisigande ao kuchemuka. Na angahewa la dunia pamoja na nguvu za sumaku za dunia vinailinda kutokana na mishale inayoweza kuua. Mufumo wa ajabu wa kutegemezana wa mimea na wanyama katika dunia unashangaza sana. Kwa hiyo, watu wengi wamefikia uamuzi wa kwamba sayari yetu dunia iliumbwa kwa kusudi fulani.—Soma Isaya 45:18.

Lakini unaweza kujiuliza, ‘Mateso na ukosefu wa haki ni sehemu ya kusudi hilo?’—Soma Kumbukumbu la Torati 32:4, 5.

Kusudi la kuumba dunia litatimizwa?

Dunia iliumbwa iwe makao yenye furaha ya watu wanaoheshimiana na wanaomupenda Muumbaji wao. Kwa hiyo, uzima wa wanadamu una kusudi kubwa sana kuliko uzima wa mimea ao wa wanyama. Tunaweza kujua Muumbaji wetu ni nani na kufurahia na kuiga haki na upendo wake.—Soma Mhubiri 12:13; Mika 6:8.

Muumbaji wetu anaweza kutimiza mambo yote anayokusudia kufanya. Kwa hiyo, tunaweza kuwa hakika kwamba atamaliza mateso na ukosefu wa haki na kufanya dunia yetu iwe makao makamilifu na yenye furaha kwa ajili ya wanadamu.—Soma Zaburi 37:11, 29; Isaya 55:11.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 3 ya kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza kuchukua kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

SOMA MAJIBU YA MAULIZO MENGINE JUU YA HABARI ZA BIBLIA KWENYE INTERNETE

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine