Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/8 uku. 7
  • Mungu Anakukaribia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mungu Anakukaribia
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Je, Kweli Yehova Anakuhangaikia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kutangaza “Habari Njema juu ya Yesu”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Biblia Inafundisha Nini juu ya Mungu?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Kuwa Rafiki ya Mungu Ndiyo Njia ya Muzuri Zaidi ya Maisha
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/8 uku. 7

KICHWA | MUNGU ANAKUONA

Mungu Anakukaribia

‘Hakuna mutu anayeweza kuja kwangu isipokuwa Baba, aliyenituma, amuvute.’—YOHANA 6:44.

SABABU INAYOFANYA WATU FULANI WAWE NA MASHAKA: Watu fulani wanaomuamini Mungu wanajisikia kuwa mbali naye. Christina, mwanamuke wa Irlande anayeenda kwenye kanisa kila juma, anasema hivi: “Nilimuona tu kuwa Mungu aliyeumba kila kitu. Lakini sikumujua. Hakuna hata siku nilijisikia kuwa karibu naye.”

MAMBO NENO LA MUNGU LINAFUNDISHA: Unapojisikia kuwa umepotea, Yehova haache hata kidogo kukusaidia. Yesu alionyesha namna Mungu anatuhangaikia kupitia mufano huu: ‘Mutu akiwa na kondoo 100 na mumoja apotee, je, hatawaacha wale 99 milimani na kuondoka kuenda kumutafuta yule anayepotea?’ Somo ni gani? ‘Vivyo hivyo Baba yangu aliye mbinguni hatamani [ao hapendi] mumoja wa wadogo hawa aangamie.’—Mathayo 18:12-14.

Kila ‘mumoja wa wadogo hawa ’ ni wa maana sana mbele ya Mungu. Namna gani Mungu ‘anatafuta yule anayepotea’? Andiko linalotajwa kwenye mwanzo wa habari hii linaonyesha kwamba Yehova anavuta watu kwake.

Mashahidi wa Yehova wanazungumuza na mwanaume fulani juu ya habari ya Biblia katika muji mukubwa

Leo, ni nani wanatembelea watu nyumbani kwao na mahali pa watu wengi ili kuwaonyesha ujumbe wa Biblia juu ya Mungu?

Fikiria namna Mungu alichukua hatua ili kuvuta watu wenye mioyo mizuri kwake. Wakati wa mitume, Mungu alimutuma Filipo, mutume Mukristo, akutane na motokari ya kukokotwa na wanyama ya ofisa Muetiopia. Mungu alipenda Filipo amufasirie ofisa huyo maana ya unabii fulani wa Biblia ambao alikuwa anasoma. (Matendo 8:26-39) Kisha hapo, Mungu alimuongoza mutume Petro atembelee kwenye nyumba ya Kornelio mukubwa katika jeshi la Roma, ambaye alikuwa amesali na kujikaza kumuabudu Mungu. (Matendo 10:1-48) Mungu alimuongoza pia mutume Paulo na wenzake kwenye muto fulani inje ya muji wa Filipi. Kwenye muto huo, walikutana na ‘muabudu wa Mungu’ anayeitwa Lidia, na “Yehova akafungua wazi moyo wake asikilize kwa makini [ao kwa uangalifu].”—Matendo 16:9-15.

Katika hali hizo zote, Yehova aliwasaidia wale waliokuwa wanamutafuta wapate nafasi ya kumujua. Leo, ni nani wanatembelea watu nyumbani kwao na mahali pa watu wengi ili kuwaonyesha ujumbe wa Biblia juu ya Mungu? Watu wengi wanaweza kujibia, “Ni Mashahidi wa Yehova.” Ujiulize, ‘Inawezekana Mungu anawatumia ili anikaribie?’ Tunakuomba usali kwa Mungu akusaidie ukubali bidii anayofanya ili umukaribie.a

a Ili kupata habari zaidi, tazama video Sababu Gani Ujifunze Biblia? kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine