Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/10 uku. 16
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/10 uku. 16

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Sababu gani tusali Ufalme wa Mungu uje?

Yesu akiwa juu ya farasi anaenda kushinda maadui wa Ufalme wa Mungu

Ungependa kujua mengi juu ya Ufalme wa Mungu na mambo Ufalme huo utafanya?

Ufalme wa Mungu ni serikali ya mbinguni. Yesu aliwaambia wafuasi wake wasali ufalme huo uje kwa sababu utarudisha haki na amani duniani. Hakuna serikali ya watu inayoweza kumaliza kabisa-kabisa jeuri, ukosefu wa haki, na magonjwa, lakini Ufalme wa Mungu unaweza na utafanya hivyo. Mungu amemuchagua Mwana wake, Yesu, akuwe Mufalme wa Ufalme huo. Yehova amechagua pia kikundi cha wafuasi wa Yesu watawale pamoja na Yesu katika Ufalme huo.—Soma Luka 11:2; 22:28-30.

Hivi karibuni, Ufalme wa Mungu utawaondoa watu wote wanaopinga utawala wa Mungu. Kwa hiyo, tunapoomba Ufalme wa Mungu uje, tunaomba uje kuchukua nafasi ya serikali zote za watu.—Soma Danieli 7:13, 14; Ufunuo 11:15, 18.

Sababu gani Ufalme wa Mungu utaletea watu faida?

Yesu ni Mufalme anayestahili kwa sababu ni mwenye huruma. Kwa kuwa ni Mwana wa Mungu, ana uwezo pia wa kusaidia watu wote wanaomuomba Mungu musaada.—Soma Zaburi 72:8, 12-14.

Ufalme wa Mungu utaletea faida watu wote wanaosali kwa moyo wote uje na kuishi kupatana na mapenzi ya Mungu. Ukijifunza mambo Biblia inafundisha juu ya Ufalme wa Mungu hautajuta hata siku moja.—Soma Luka 18:16, 17; Yohana 4:23.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 8 ya kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza kupata kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internetewww.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine