Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/3 uku. 16
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tunapaswa Kukumbuka Kifo cha Yesu Jinsi Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • ‘Mufanye Hivi kwa Kunikumbuka Mimi’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Sababu Gani Yesu Aliteseka na Kufa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/3 uku. 16

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Sababu gani Tunapaswa Kukumbuka Kifo cha Yesu?

Watu wanafurahia maisha katika paradiso duniani

Kifo cha Yesu kinawezesha watu kuwa na tumaini gani la wakati unaokuja?—Isaya 25:8; 33:24

Kifo cha Yesu ndilo tukio la maana sana katika historia; alikufa ili kurudisha maisha ya watu namna yalipaswa kuwa. Wakati mutu aliumbwa hangeweza kufanya mambo mabaya, kugonjwa, ao kufa. (Mwanzo 1:31) Lakini zambi iliingia katika dunia kupitia mutu mumoja, Adamu. Yesu alitoa uzima wake ili kutuokoa kutoka katika zambi na kifo.—Soma Mathayo 20:28; Waroma 6:23.

Mungu alituonyesha upendo mukubwa sana kwa kutuma Mwana wake duniani ili akufe kwa ajili yetu. (1 Yohana 4:9, 10) Yesu aliwaambia wafuasi wake wakumbuke kifo chake kupitia tukio lisilokuwa na mambo mengi lenye kutia ndani mukate na divai. Wakati tunafanya hivyo kila mwaka, tunaonyesha shukrani yetu kwa ajili ya upendo Mungu na Mwana wake walituonyesha.—Soma Luka 22:19, 20.

Ni nani wanastahili kula mukate na kunywa divai?

Wakati Yesu aliwaambia wanafunzi wake kwa mara ya kwanza wakumbuke kifo chake, alisema juu ya agano, ao mapatano. (Mathayo 26:26-28) Agano hilo liliwawezesha wao na hesabu kidogo ya watu wengine kupata tumaini la kuwa wafalme na makuhani pamoja naye mbinguni. Mamilioni ya watu wanakumbuka kifo cha Yesu, lakini ni wale tu wenye kuwa katika agano hilo ndio wanakula mukate na kunywa divai.—Soma Ufunuo 5:10.

Kwa miaka karibu 2000, Yehova amekuwa akichagua watu wenye watakuwa wafalme. (Luka 12:32) Watu hao ni wachache kwa kuwalinganisha na wale wenye wataishi milele kwenye dunia.—Soma Ufunuo 7:4, 9, 17.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 5 ya kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza pia kupata kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine