Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/3 uku. 16
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Sababu Gani Yesu Aliteseka na Kufa?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Ulizo la 2: Nitakapokufa, Nitaenda Wapi?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Kifo cha Yesu na Ufufuo Wake—Vinaweza Kukuletea Faida Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/3 uku. 16
Watu wanajifurahisha kwenye bahari katika dunia paradiso na watoto wanaogelea

MAULIZO JUU YA HABARI ZA BIBLIA YANAJIBIWA

Kifo cha Yesu kinatuletea faida gani?

Wakati Mungu aliumba wanadamu, alikusudia waishi milele duniani bila kuteseka na magonjwa wala kifo. Lakini, Adamu, mutu wa kwanza, hakumutii Muumbaji wake na akapoteza tumaini la kuishi milele. Kwa sababu sisi ni wazao wa Adamu, tuliriti kifo kutoka kwake. (Waroma 5:8, 12; 6:23) Yehova, Mungu wa kweli, alimutuma Mwana wake, Yesu, duniani akufe na kulipia mambo ambayo Adamu alipoteza.​—Soma Yohana 3:16.

Yesu alikufa ili kuwezesha wanadamu wapate uzima wa milele. Unawaza uzima usiokuwa na mwisho duniani utakuwa namna gani?

Kifo cha Yesu kinatuwezesha kupata musamaha wa zambi zetu na uzima wa milele. Biblia inatuelezea namna uzima utakuwa duniani wakati hatutateseka tena na uzee, magonjwa, na kifo.​—Soma Isaya 25:8; 33:24; Ufunuo 21:4, 5.

Namna gani tunapaswa kukumbuka kifo cha Yesu?

Magaribi iliyotangulia kifo chake, Yesu aliwaambia wafuasi wake wakumbuke kifo chake kupitia sherehe isiyo na mambo mengi. Kukumbuka kifo cha Yesu kwa njia hiyo kila mwaka kunatuwezesha kufikiria namna Yesu na Yehova wanapenda wanadamu sana.​—Soma Luka 22:19, 20; 1 Yohana 4:9, 10.

Mwaka huu, Ukumbusho wa kifo cha Yesu utafanywa Siku ya Kwanza, tarehe 14 Mwezi wa 4, kisha jua kushuka. Unaalikwa kuja kukusanyika siku hiyo pamoja na Mashahidi wa Yehova wa eneo lenu.​—Soma Waroma 1:11, 12.

Ili kupata habari zingine, soma sura ya 4 na ya 5 ya kitabu hiki, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza kuchukua kitabu hiki kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine