Ukuwe Macho Shetani Anapenda Kukumeza!
‘Mukuwe wenye kulinda. Adui yenu, Ibilisi, anatembea huku na huku kama simba anayenguruma, akitafuta kumumeza mutu.’—1 PET. 5:8.
1. Eleza namna kiumbe mumoja wa roho aligeuka na kuwa Shetani.
WAKATI fulani alikuwa na uhusiano muzuri na Yehova. Lakini kisha muda fulani, kiumbe huyo wa roho alianza kutamani wanadamu wamuabudu. Kuliko kuachana mbiombio na tamaa hiyo mbaya, aliikomalisha mupaka ilimusukuma afanye zambi. (Yak. 1:14, 15) Tunajua kwamba kiumbe huyo ni Shetani, mwenye “hakusimama imara katika kweli.” Alimuasi Yehova na kuwa ‘baba ya uongo.’—Yoh. 8:44.
2, 3. Majina “Shetani,” “Ibilisi,” “nyoka,” na ‘joka mukubwa,’ yanaonyesha nini juu ya adui mukubwa wa Yehova?
2 Tangu wakati aliasi, Shetani ameonyesha kwamba yeye ndiye adui mukubwa wa Yehova na wa wanadamu wote. Majina yenye Shetani amepewa katika Biblia, inaonyesha wazi kwamba yeye ni mutu mubaya sana. Jina Shetani linamaanisha “Mupinzani,” hilo linaonyesha kwamba kiumbe huyo wa roho haunge mukono utawala wa Mungu; lakini, anauchukia na anatumia nguvu zake zote ili kupiganisha utawala huo. Kusudi kubwa la Shetani, ni kuona utawala wa Yehova unafikia mwisho.
3 Andiko la Ufunuo 12:9, linamuita Shetani kuwa Ibilisi. Jina hilo linamaanisha “Musingiziaji ao muchongezi.” Hilo linatukumbusha kwamba Shetani amemusingizia Yehova kwa kumuita musema-uongo. Maneno “nyoka wa zamani” inatukumbusha wakati Shetani alitumia nyoka katika shamba la Edeni ili kumudanganya Eva. Maneno ‘joka mukubwa’ yanatutolea wazo la munyama mukubwa sana mwenye kuogopesha; na anastahili kuitwa hivyo kwa sababu anajikaza sana ili kuzuia kusudi la Yehova na kuangamiza watumishi Wake.
4. Tutazungumuzia nini katika habari hii?
4 Kwa kweli, Shetani anashambulia sana uaminifu wetu. Ndiyo sababu Biblia inatushauria hivi: ‘Mutunze akili zenu, mukuwe wenye kulinda. Adui yenu, Ibilisi, anatembea huku na huku kama simba anayenguruma, akitafuta kumumeza mutu.’ (1 Pet. 5:8) Ili tuelewe vizuri shauri hilo, katika habari hii tutazungumuzia sifa tatu za Shetani zenye tunapaswa kuelewa ili tujue sababu gani tunapaswa kumupinga adui huyo mukubwa wa Yehova na wa watumishi Wake.
SHETANI NI MWENYE NGUVU
5, 6. (a) Toa mifano yenye kuonyesha kwamba viumbe wa roho wako na “uwezo katika nguvu.” (b) Ni katika njia gani Shetani iko na “uwezo wa kusababisha kifo”?
5 Viumbe wa roho wenye kuitwa malaika wako na “uwezo katika nguvu.” (Zab. 103:20) Viumbe hao wako na akili na nguvu zaidi kuliko wanadamu. Bila shaka, malaika waaminifu wanatumia nguvu zao ili kufanya mambo mazuri. Kwa mufano, usiku moja malaika wa Yehova aliua maaskari Waashuru 185000. Ingekuwa vigumu sana kwa mwanadamu, na hata jeshi nzima kuua maadui hao. (2 Fal. 19:35) Wakati mwingine malaika mumoja alitumia nguvu na ufundi wake ili kutosha mitume wa Yesu katika gereza. Hata kama walinzi walikuwa kila mahali ili kuchunga gereza hilo, malaika huyo alifungua mulango, aliwatosha mitume hao inje, na kisha akafunga mulango!—Mdo. 5:18-23.
6 Viumbe wa roho waaminifu wanatumia nguvu zao ili kufanya mambo mazuri, lakini Shetani anatumia nguvu zake ili kufanya mambo mabaya. Bila shaka iko na nguvu na anachochea wengine kufanya mambo mabaya! Biblia inamuita ‘mutawala wa ulimwengu huu’ na ‘mungu wa mufumo huu wa mambo.’ (Yoh. 12:31; 2 Kor. 4:4) Shetani Ibilisi iko pia na “uwezo wa kusababisha [kuleta] kifo.” (Ebr. 2:14) Hilo halimaanishe kwamba anaua watu wote moja kwa moja. Lakini, watu wameiga tabia yake ya kuua kila mahali katika dunia. Zaidi ya hilo, kwa sababu Eva alisikiliza uongo wa Shetani na Adamu alikosa kumutii Mungu, zambi na kifo vilienea juu ya wanadamu wote. (Rom. 5:12) Katika njia hizo, Ibilisi iko na “uwezo wa kusababisha kifo.” Ndiyo sababu Yesu alimuita “muuaji.” (Yoh. 8:44) Shetani ni adui yetu mukubwa kabisa na mwenye nguvu!
7. Namna gani mashetani wameonyesha kama wako na nguvu?
7 Wakati tunamupinga Shetani, tunapinga pia wale wote wenye kumuunga mukono ili kukataa utawala mukubwa wa Yehova. Kati ya wale wenye kumuunga mukono, kuna mashetani, ni kusema, malaika wenye walimuasi Yehova. (Ufu. 12:3, 4) Tangu zamani, mashetani hao wameonyesha kwamba wako na nguvu nyingi sana kwa kuwatesa sana wanadamu. (Mt. 8:28-32; Mk. 5:1-5) Usizarau nguvu za mashetani ao zile za ‘mutawala wa roho waovu.’ (Mt. 9:34) Bila musaada wa Yehova, hatuwezi kupata ushindi katika vita yenye tunapigana na Shetani.
SHETANI NI MUKALI SANA
8. (a) Shetani iko na kusudi gani? (Ona picha kwenye mwanzo wa habari hii.) (b) Kulingana na mambo yenye umejionea, ni nini inaonyesha kwamba watu wa dunia hii ni wakali kama Shetani?
8 Mutume Petro alilinganisha Shetani na ‘simba mwenye kunguruma.’ Kitabu kimoja kinasema kwamba neno la Kigiriki lenye kutafsiriwa ‘mwenye kunguruma’ linamaanisha “kilio cha munyama mwenye njaa kubwa.” Maneno hayo inaonyesha kwamba Shetani ni mutu mubaya na mukali sana! Shetani anatawala dunia yote; lakini, hajatosheka na angali na njaa ya kupata watu wengi zaidi. (1 Yoh. 5:19) Shetani anaona dunia yote kuwa ni kitu cha kuonja tu. Kwa hiyo, anashambulia zaidi sana mabaki ya Wakristo watiwa-mafuta na wale wenye kuwasaidia, ni kusema, “kondoo wengine.” (Yoh. 10:16; Ufu. 12:17) Shetani anapenda kuwameza watumishi wa Yehova. Mateso makali yenye Wakristo wamepata tangu wakati wa mitume mupaka leo, inahakikisha kabisa kwamba Shetani ni mukali sana.
9, 10. (a) Namna gani Shetani alijaribu kuzuia kusudi la Mungu kwa ajili ya taifa la Israeli? (Toa mifano.) (b) Sababu gani Shetani alishambulia sana taifa la Israeli? (c) Unawaza Ibilisi anajisikia namna gani wakati mutumishi wa Yehova anafanya zambi nzito leo?
9 Tena, Shetani anaonyesha kwamba iko mutu mubaya sana kwa sababu anajikaza kuzuia kusudi la Mungu lifanyike. Simba mwenye njaa hasikiliake huruma munyama mwenye anakamata. Hasikiliake munyama huyo huruma mbele ya kumuua wala hahuzunikake hata kidogo kisha kumuua. Vilevile, Shetani hasikilie huruma watu wenye anajaribu kumeza. Kwa mufano, fikiria wakati Waisraeli waliangukia katika zambi, kama vile uasherati na pupa (tamaa kubwa). Bila shaka, kila mara Shetani Ibilisi alikuwa anajificha na kuangalia mambo hayo. Kwa mufano, wakati unasoma habari yenye kuonyesha matokeo mabaya sana ya matendo ya Zimri na pupa ya Gehazi, unaweza “kuona” namna simba huyo mwenye kunguruma anafurahi sana kwa sababu amepata ushindi?—Hes. 25:6-8, 14, 15; 2 Fal. 5:20-27.
Wakati mutumishi wa Yehova anafanya zambi, Shetani anafurahi sana(Ona fungu la 10)
10 Kuna sababu ya pekee yenye ilifanya Shetani ashambulie sana taifa la Israeli. Bila shaka, ni kwa sababu taifa hilo lingetokeza Masiya, ni kusema, mutu mwenye angeponda Shetani na kutetea utawala wa Yehova. (Mwa. 3:15) Shetani hakupenda Waisraeli waendelee kuwa na urafiki pamoja na Mungu. Kwa hiyo, alifanya yake yote ili waangukie katika zambi. Usifikiri kwamba Shetani alihuzunika wakati Mufalme Daudi alifanya uasherati ao kwamba alimusikilia nabii Musa huruma wakati hakustahili tena kuingia katika Inchi ya Ahadi. Lakini, Shetani anafurahi sana wakati mutumishi wa Mungu anafanya zambi nzito. Bila shaka, wakati mutumishi wa Mungu anaangukia katika zambi nzito, Ibilisi anaona jambo hilo kuwa ni ushindi, na ushindi huo ni njia moja yenye anatumia ili kumuzihaki ao kumuchekelea Yehova.—Met. 27:11.
11. Sababu gani Shetani alimujaribu Sara?
11 Shetani alichukia sana familia yenye ingetokeza Masiya. Kwa mufano, fikiria jambo lenye lilitokea muda mufupi kisha Mungu kumuambia Abrahamu kwamba atakuwa “taifa kubwa.” (Mwa. 12:1-3) Wakati Abrahamu na Sara walikuwa katika inchi ya Misri, Farao aliomba wamulete Sara katika nyumba yake. Bila shaka alipenda akuwe bibi yake. Lakini, Yehova alimulinda na kumuokoa Sara katika hali hiyo yenye hatari. (Soma Mwanzo 12:14-20.) Muda mufupi mbele Isaka azaliwe, jambo lenye kufanana na hilo lilifanyika huko Gerari. (Mwa. 20:1-7) Tunaweza kusema kwamba ni Shetani ndiye alikuwa anaongoza mambo? Shetani alifikiri kwamba Sara mwenye aliacha muji tajiri wa Uru na kuanza kuishi katika mahema angedanganywa na nyumba nzuri ya Farao na ya Abimeleki? Shetani alikuwa anafikiri kwamba Sara atamuacha Abrahamu, Yehova, na kuolewa na wafalme hao? Biblia haiseme jambo fulani, lakini tuko na sababu nzuri ya kuwa hakika kwamba Ibilisi angefurahi sana ikiwa Sara angepoteza pendeleo la kuwa katika familia yenye ingetokeza Masiya. Shetani angefurahi sana wakati angeona namna Sara anaharibu ndoa yake, sifa yake, na urafiki wake pamoja na Yehova. Shetani ni mukali sana kabisa!
12, 13. (a) Kisha Yesu kuzaliwa, namna gani Shetani alionyesha kwamba ni mukali sana? (b) Unawaza Shetani anajisikia namna gani juu ya vijana wenye kumupenda Yehova na wenye kujikaza kumutumikia leo?
12 Yesu alizaliwa miaka mingi kisha kufa kwa Abrahamu. Unawaza Shetani alimuona mutoto huyo kuwa mwenye sura nzuri, mwenye kupendwa na watu, ao wa maana sana? Hapana, kwa sababu alijua kwamba mutoto huyo atakomaa na kuwa Masiya. Bila shaka, Yesu ndiye angekuwa sehemu ya kwanza ya uzao wa Abrahamu, uzao wenye “ungezivunja kazi za Ibilisi.” (1 Yoh. 3:8) Je, Shetani alijua kwamba kwa kumuua mutoto huyo angefanya jambo mbaya sana? Shetani hahangaikie hata kidogo kujua mambo mazuri na mabaya. Bila kukawia, Shetani alifanya mipango ya kumuua mutoto Yesu. Namna gani?
13 Wakati watu wenye elimu ya nyota walimuambia Mufalme Herode kwamba ‘mufalme wa Wayahudi amezaliwa,’ alijisikia mubaya sana na akafanya mipango ya kumuua. (Mt. 2:1-3, 13) Ili akuwe hakika kwamba mutoto huyo amekufa, alitoa amri ya kuua watoto wadogo wote wenye kuwa na miaka mbili kwenda chini, katika Bethlehemu na maeneo yake yote. (Soma Mathayo 2:13-18.) Yesu aliokoka mauaji hayo makubwa, lakini jambo hilo linatufundisha nini juu ya adui wetu Shetani? Hilo linatufundisha kwamba Ibilisi haone uzima wa mwanadamu kuwa wa lazima. Hawasikilie watoto huruma hata kidogo. Kwa kweli, Shetani ni “simba anayenguruma.” Usisahau hata kidogo kwamba yeye ni mukali sana!
SHETANI NI MUSEMA-UONGO
14, 15. Namna gani Shetani ‘anapofusha akili za wasioamini’?
14 Ili kuwafanya watu wapoteze urafiki wao pamoja na Yehova, Mungu mwenye upendo, Shetani anatumia sana uongo. (1 Yoh. 4:8) Shetani anadanganya watu kwa kuwafanya ‘wasitambue uhitaji wao wa kiroho.’ (Mt. 5:3) Kwa hiyo, ‘anapofusha akili za wasioamini, ili nuru ya habari njema yenye utukufu juu ya Kristo, aliye mufano wa Mungu, isipenyeze [isiingize] mwangaza.’—2 Kor. 4:4.
15 Njia kubwa zaidi yenye Shetani anatumia ili kudanganya watu ni dini za uongo. Shetani anafurahi sana kuona watu wanaabudu wazazi wao wa zamani, wanyama ao vitu vyenye kuwazunguka, kuliko kumuabudu Yehova, mwenye ‘anataka watu wajitoe kikamili’ kwake. (Kut. 20:5) Hata watu wengi wenye kufikiri kwamba wanamuabudu Mungu kwa njia yenye kufaa, wanashikamana na mafundisho ya uongo na desturi zenye hazina maana yoyote. Wako katika hali mbaya sana kama ile ya watu wenye Yehova aliambia hivi: ‘Kwa nini munaendelea kulipa pesa kwa ajili ya kitu ambacho si mukate, na kwa nini kazi yenu ni kwa ajili ya kitu ambacho hakishibishe? Munisikilize kwa makini [uangalifu], na mukule yaliyo mema, na nafsi yenu ipate furaha tele katika unono.’—Isa. 55:2.
16, 17. (a) Sababu gani Yesu alimuambia Petro: ‘Enda nyuma yangu, Shetani’? (b) Namna gani Shetani anaweza kutudanganya ili tusiendelee kuwa macho?
16 Shetani anaweza kudanganya hata watumishi wa Yehova wenye kumutumikia kwa bidii. Kwa mufano, fikiria jambo lenye lilitokea wakati Yesu aliwaambia mitume wake kwamba watu wanakaribia kumuua. Mutume Petro alikuwa anamupenda Yesu; kwa hiyo, alimuchukua pembeni na kumuambia hivi: ‘Ujitendee kwa fazili [kwa wema], Bwana; wewe hautapatwa hata kidogo na jambo hili.’ Yesu alimujibu waziwazi hivi: ‘Enda nyuma yangu, Shetani!’ (Mt. 16:22, 23) Sababu gani Yesu alimuita Petro “Shetani”? Kwa sababu Yesu alijua jambo lenye lilikuwa karibu kutokea. Saa ilikuwa imekaribia ili kupitia kifo chake atoe zabihu ya ukombozi na kuonyesha kabisa kwamba Ibilisi ni musema-uongo. Kwa sababu wakati huo ulikuwa wa maana katika historia ya wanadamu, Yesu hakuona kwamba ni wakati wa ‘kujitendea’ kwa wema. Shetani angefurahi ikiwa Yesu angeregeza musimamo wake wa kuendelea kuwa macho.
17 Kwa sababu mwisho wa ulimwengu huu muovu unakaribia, sisi pia tunaishi wakati wa hatari. Shetani anapenda tusiendelee kuwa macho, ni kusema, ‘tujitendee’ kwa wema kwa kutafuta kujulikana katika ulimwengu huu ili tusione kwamba ni jambo la lazima tutende kwa haraka. Usikubali Shetani akuzuie kuendelea kuwa macho! Kwa hiyo, ‘uendelee kukesha.’ (Mt. 24:42) Shetani anadanganya watu kwamba mwisho wa ulimwengu huu ungali mbali ao kwamba hautakuja hata siku moja. Usiamini uongo huo.
18, 19. (a) Namna gani Shetani anajikaza kutudanganya ili tufikiri kwamba Yehova hawezi kutupenda? (b) Namna gani Yehova anatusaidia tuendelee kutunza akili zetu na kuendelea kuwa macho?
18 Shetani anajikaza kutudanganya katika njia ingine. Anapenda tuamini kwamba Mungu hawezi kutupenda na kwamba hawezi kusamehe zambi zetu. Huo ni uongo wa Shetani. Lakini, ni nani mwenye Yehova hawezi kupenda hata kidogo? Ni Shetani. Ni nani mwenye Yehova hawezi kusamehe hata kidogo? Ni Shetani. Lakini Biblia inatuhakikishia hivi: ‘Mungu hakosi kuwa mwadilifu hivi kwamba asahau kazi yenu na upendo mulioonyesha kwa ajili ya jina lake.’ (Ebr. 6:10) Yehova anafurahia sana bidii yenye tunafanya ili kumupendeza, na kazi yenye tunamufanyia haiko ya bure. (Soma 1 Wakorintho 15:58.) Kwa hiyo, tusimuruhusu Shetani atudanganye.
19 Tumejifunza kwamba Shetani ni mwenye nguvu, mukali sana, na musema-uongo. Namna gani tunaweza kupata ushindi juu ya adui huyo mwenye kuogopesha? Yehova hatuache bila ulinzi. Neno lake linatusaidia kutambua njia za Shetani, na ‘hatukose kuzijua mbinu [njia] zake.’ (2 Kor. 2:11) Wakati tunajua vizuri njia za Shetani, hilo linatusaidia kutunza akili zetu na kuendelea kuwa macho. Lakini haitoshe tu kujua njia za Shetani. Biblia inasema hivi: ‘Mumupinge Ibilisi, naye atawakimbia ninyi.’ (Yak. 4:7) Habari yenye kufuata itazungumuzia njia tatu zenye zinaweza kutusaidia kupigana na Shetani na kupata ushindi.