Somo 4
Ibilisi Ni Nani?
Shetani Ibilisi—yeye alitoka wapi? (1, 2)
Namna gani Shetani anawadanganya watu? (3-7)
Kwa nini unapaswa kumupinga Ibilisi? (7)
1. Neno “Ibilisi” linamaanisha mutu fulani anayeeleza mambo mabaya ya uwongo juu ya mutu mwingine. “Shetani” maana yake adui au mupinzani. Hayo ndiyo majina aliyopewa adui mukuu wa Mungu. Mwanzoni, yeye alikuwa malaika mukamilifu mbinguni pamoja na Mungu. Lakini, baadaye, alifikiri zaidi sana juu yake mwenyewe na aliitaka ibada ambayo ni ya Mungu.—Matayo 4:8-10.
2. Malaika huyu, Shetani, alisema kwa Hawa kupitia kwa nyoka. Kwa kumuelezea mambo ya uwongo, alimufanya Hawa akose utii kwa Mungu. Kwa kufanya hivyo Shetani alishambulia kile kinachoitwa “Enzi-Kuu” ya Mungu, au cheo chake kama Aliye Juu Zaidi. Shetani alitilia shaka kwamba Mungu hatawali vizuri na hafanyi hivyo kwa faida bora zaidi ya Raia Wake. Pia Shetani alitilia shaka kwamba binadamu yeyote hangeweza kubaki mwaminifu kwa Mungu. Kwa kufanya hivyo, Shetani alijifanya mwenyewe kuwa adui wa Mungu. Hiyo ndiyo sababu yeye alikuja kuitwa Shetani Ibilisi.—Mwanzo 3:1-5; Yobu 1:8-11; Ufunuo 12:9.
3. Shetani kwa ujanja anajaribu kuwafanya watu wamuabudu yeye. (2 Wakorinto 11:3, 14) Njia moja anayotumia kwa kudanganya watu ni dini isiyo ya kweli. Ikiwa dini inafundisha mambo ya uwongo juu ya Mungu, kwa kweli dini hiyo inatumikia kusudi la Shetani. (Yoane 8:44) Watu walio washiriki wa dini isiyo ya kweli wanaweza kuamini kwa moyo wote kwamba wao wanamuabudu Mungu wa kweli. Lakini kwa kweli wao wanamutumikia Shetani. Yeye ni ‘mungu wa ulimwengu huu.’—2 Wakorinto 4:4.
4. Uhusiano na roho wabaya ni njia nyingine Shetani anatumia ili kuleta watu wawe chini ya nguvu yake. Wanaweza kuwaita roho wabaya ili wawalinde, ili wazuru wengine, ili waeleze mambo ya wakati ujao, au wafanye miujiza. Shetani ni kani yenye uovu inayojificha nyuma ya mazoea hayo yote. Ili kumupendeza Mungu, sisi tunapaswa kuacha kabisa kuwa na uhusiano na roho wabaya.—Kumbukumbu la Torati 18:10-12; Matendo 19:18, 19.
5. Pia Shetani anadanganya watu kwa njia ya kujivunia rangi ya ngozi kupita kiasi pamoja na ibada inayotolewa matengenezo ya kisiasa. Kuna wengine wanaojisikia kwamba taifa lao au rangi yao ya ngozi ndiyo nzuri kupita ya wengine. Lakini hilo si kweli. (Matendo 10:34, 35) Watu wengine wanatazamia matengenezo ya kisiasa kumaliza magumu ya binadamu. Kwa kufanya hivyo, wanakataa Ufalme wa Mungu. Ufalme huo ndiyo njia pekee ya kumaliza magumu yetu.—Danieli 2:44.
6. Njia nyingine Shetani anatumia ili kudanganya watu ni kwa kuwajaribu kwa tamaa za zambi. Yehova anatuelezea sisi kuepuka mazoea ya zambi kwa sababu anajua kwamba yatatuumiza. (Wagalatia 6:7, 8) Kuna watu wangependa wewe uungane nao katika mazoea kama hayo. Hata hivyo, ukumbuke kwamba ni Shetani kweli kweli anayependa wewe ufanye mambo hayo.—1 Wakorinto 6:9, 10; 15:33.
7. Shetani anaweza kutumia mateso au upinzani kukufanya wewe umuache Yehova. Wengine wa wapendwa wako wanaweza kukasirika sana kwa sababu wewe unajifunza Biblia. Wengine wanaweza kukuchekelea. Uhai ulio nao ni wa nani? Shetani anapenda kukutisha ili kwamba usimamishe kujifunza juu ya Yehova. Usimuache Shetani ashinde! (Matayo 10:34-39; 1 Petro 5:8, 9) Kwa kupingana na Ibilisi, unaweza kumufanya Yehova awe na furaha na kuonyesha kwamba unategemeza enzi Yake.—Mezali 27:11.
[Picha katika ukurasa wa 9]
Dini isiyo ya kweli, uhusiano na roho wabaya, na pia kupenda taifa lako vinadanganya watu
[Picha katika ukurasa wa 9]
Pinga Shetani kwa kuendelea kujifunza juu ya Yehova