Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/10 uku. 5
  • Sababu Gani Mungu Anatuomba Tusali?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sababu Gani Mungu Anatuomba Tusali?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mungu anapenda tukuwe marafiki wake.
  • Mungu anapenda kukusaidia.
  • Wanadamu wako na uhitaji wa kiroho.
  • Mungu Anasikiaka Sala Zako?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Maulizo Juu Ya Habari Za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Sala Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Kumukaribia Mungu Karibu Katika Sala
    Mungu Anataka Nini Kwetu?
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/10 uku. 5

HABARI KUBWA | KUSALI KUNALETA FAIDA FULANI?

Sababu Gani Mungu Anatuomba Tusali?

Mungu anapenda tukuwe marafiki wake.

Marafiki wanazungumuza ili wakuwe na urafiki muzuri zaidi. Mungu pia anatuomba tuzungumuze naye, kwa kufanya hivyo anatupatia nafasi ya kuwa na urafiki muzuri pamoja naye. Anasema hivi: ‘Mutaniita na kuja na kusali kwangu, nami nitawasikiliza.’ (Yeremia 29:12) Kuzungumuza na Mungu kupitia sala kutatusaidia ‘kumukaribia Mungu, naye atatukaribia.’ (Yakobo 4:8) Biblia inatuhakikishia hivi: ‘Yehova iko karibu na wote wanaomuitia.’ (Zaburi 145:18) Kama tunazoea kusali, urafiki wetu pamoja na Mungu utakomaa.

‘Yehova iko karibu na wote wanaomuitia.’—Zaburi 145:18

Mungu anapenda kukusaidia.

Yesu alisema hivi: ‘Ni nani kati yenu ambaye mwana wake akimuomba mukate—je, atamupa jiwe? Kwa hiyo, ikiwa ninyi . . . munajua jinsi ya kuwapa watoto wenu zawadi zilizo nzuri, je, Baba yenu aliye mbinguni hatawapa hata zaidi vitu vyema wale wanaomuomba?’ (Mathayo 7:9-11) Ndiyo, Mungu anakuomba usali kwa sababu “yeye anakujali [anakuhangaikia]” na anataka kukusaidia. (1 Petro 5:7) Anakuomba hata umuelezee magumu yako. Biblia inatuambia hivi: ‘Musihangaike juu ya kitu chochote, bali [lakini] katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani maombi yenu na yajulishwe Mungu.’—Wafilipi 4:6.

Wanadamu wako na uhitaji wa kiroho.

Watu wenye elimu ya hali ya wanadamu wametambua kama mamilioni ya watu wanaona ulazima wa kusali. Hata watu fulani wenye kuamini kama hakuna Mungu na wenye kuamini kama mambo yake hayawezi kujulikana, wako na ulazima huo.a Jambo hilo linahakikisha kama wanadamu waliumbwa na ulazima wa kiroho. Yesu alisema hivi: “Wenye furaha ni wale wanaotambua uhitaji [ulazima] wao wa kiroho.” (Mathayo 5:3) Njia moja ya kutimiza ulazima huo ni kuzungumuza kwa ukawaida na Mungu katika sala.

Ikiwa tunasali kama vile Mungu anatuomba, tutapata faida gani?

a Uchunguzi wenye ulifanywa na Kituo cha Utafiti cha Pew katika mwaka wa 2012, ulionyesha kama katika inchi ya Amerika, watu 11 juu 100 wenye kuamini kama hakuna Mungu na wenye kuamini kama mambo yake hayawezi kujulikana, wanasali mara moja hivi katika mwezi.

Tunaweza Kusali Juu ya Mambo Gani?

Biblia inaonyesha kama tunaweza kusali juu ya kila jambo katika maisha yetu. Tunaweza kusali juu ya mambo kama vile:

  • Kuomba Musamaha: ‘Niliungama zambi yangu kwako; wala sikufunika kosa langu.’—Zaburi 32:5.

  • Kushukuru: ‘Ni vema [muzuri] kumutolea Yehova shukrani.’—Zaburi 92:1.

  • Kusifu: ‘Nitamubariki Yehova nyakati zote; daima sifa yake itakuwa katika kinywa changu.’—Zaburi 34:1.

  • Kuomba Muongozo: “Unitembeze katika njia ya amri zako, kwa maana nimependezwa nayo.”—Zaburi 119:35.

  • Kuomba Nguvu: ‘Nigeukie na kunionyesha kibali. Umupe mutumishi wako nguvu zako.’—Zaburi 86:16.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine