Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/10 uku. 6-8
  • Sala— Inaweza Kukuletea Faida Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sala— Inaweza Kukuletea Faida Gani?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Amani ya akili.
  • Faraja na nguvu wakati wa magumu.
  • Hekima kutoka kwa Mungu.
  • Kusali Kunaweza Kukuletea Faida Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Go Rapela Modimo go Nyoko go Šutetsa Thina Naye
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/10 uku. 6-8
Mwanamuke mwenye kusali, anawaza juu ya mama yake mwenye kuwa mugonjwa

HABARI KUBWA | KUSALI KUNALETA FAIDA FULANI?

Inaweza Kukuletea Faida Gani?

Mbele ya kufanya jambo lolote, kwa kawaida unaweza kujiuliza, ‘Jambo hili litaniletea faida gani?’ Lakini, kujiuliza hivyo juu ya sala kunaonyesha kama unatafuta faida yako mwenyewe? Hapana. Kwa kawaida, tunapenda kujua ikiwa inaleta faida ao hapana. Hata Ayubu, mwanaume muaminifu, aliuliza hivi: ‘Kama ningemuita, je, angenijibu?’—Ayubu 9:16.

Katika habari zenye zilitangulia, tulizungumuzia mambo yenye kuhakikisha kama sala haiko tu desturi ya kidini ao aina fulani ya matunzo ya akili. Mungu wa kweli anasikiliza sala kabisa. Kama tunasali kwa njia ya muzuri na juu ya mambo yenye kufaa, atatusikiliza. Kwa kweli, anatuomba tumukaribie. (Yakobo 4:8) Kwa hiyo, tunaweza kupata faida gani kama tunazoea kusali katika maisha yetu? Acha tuzungumuzie faida fulani tu za sala.

Amani ya akili.

Wakati magumu yanatokea katika maisha yako, unajisikia kuwa na mahangaiko sana? Biblia inatutia moyo ‘tusali bila kuacha’ wakati kama huo, na ‘maombi yetu yajulishwe Mungu.’ (1 Wathesalonike 5:17; Wafilipi 4:6) Biblia inatuhakikishia kama, ikiwa tunasali kwa Mungu, “amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote itailinda mioyo [yetu] na nguvu [zetu] za akili.” (Wafilipi 4:7) Kwa kumuambia Baba yetu wa mbinguni mahangaiko yetu katika sala, tunaweza kuwa na utulivu kwa kiasi fulani. Yeye mwenyewe anatutia moyo tufanye hivyo. Andiko la Zaburi 55:22 linasema hivi: ‘Umutupie Yehova muzigo wako, naye mwenyewe atakutegemeza.’

‘Umutupie Yehova muzigo wako mwenyewe atakutegemeza.’—Zaburi 55:22

Watu wengi duniani wamepata amani hiyo. Hee Ran, wa inchi ya Korea ya Kusini anasema hivi: “Hata kama niko na magumu ya nguvu, wakati ninasali juu ya magumu hayo, ninajisikia kuwa mwenye kutulia na ninajisikia kuwa niko na nguvu ya kuvumilia.” Cecilia, wa inchi ya Ufilipino, anasema hivi: “Kuwa mama kunanifanya nikuwe na woga juu ya watoto wangu wanawake na juu ya mama yangu muzazi mwenye hawezi tena kunitambua. Lakini kwa sababu ya sala, ninapata uwezo wa kupitisha siku yangu bila mahangaiko mengi. Ninajua kama Yehova atanisaidia niwahangaikie.”

Faraja na nguvu wakati wa magumu.

Unapambana na mahangaiko makubwa ya akili, pengine hali zenye kutia uzima katika hatari ao hali zenye kuhuzunisha sana? Kusali kwa “Mungu wa faraja [kitulizo] yote” kunaweza kukufanya utulie kabisa. Biblia inasema kama ‘anatufariji katika ziki yetu yote.’ (2 Wakorintho 1:3, 4) Kwa mufano, wakati fulani Yesu alikuwa mwenye huzuni sana, ‘alipiga magoti na kuanza kusali.’ Matokeo yalikuwa nini? ‘Malaika kutoka mbinguni akamutokea akamutia nguvu.’ (Luka 22:41, 43) Nehemia, mwanaume mwengine muaminifu, aliteseka kwa sababu ya kuogopeshwa na watu wabaya wenye walijaribu kumufanya aache kazi ya Mungu. Alisali hivi: “Sasa itie mikono yangu nguvu.” Mambo yenye yalitokea kisha hapo yanaonyesha kama Mungu alimusaidia kabisa ashinde woga wake na kumaliza kazi yake. (Nehemia 6:9-16) Reginald, wa inchi ya Ghana, anaeleza namna sala inamusaidia. Anasema hivi: “Wakati ninasali, zaidi sana katika hali ya magumu yenye kunipita akili, ninajisikia kama nimemuambia magumu yangu mutu mwenye kuwa na uwezo wa kunisaidia na mwenye kunihakikishia kama hakuna sababu ya kuhangaika.” Kwa kweli, Mungu anaweza kutufariji wakati tunasali kwake.

Hekima kutoka kwa Mungu.

Maamuzi fulani yenye tunakamata yanaweza kutuletea matokeo ya siku nyingi sisi na watu wenye tunapenda. Namna gani tunaweza kukamata maamuzi ya hekima? Biblia inasema: ‘Kwa hiyo, ikiwa yeyote kati yenu anakosa hekima [zaidi sana katika kupambana na magumu], na aendelee kumuomba Mungu, kwa maana yeye anawapa wote kwa ukarimu na bila kushutumu; naye atapewa hiyo.’ (Yakobo 1:5) Kama tunasali ili kupata hekima, Mungu anaweza kutumia roho yake takatifu ili ituongoze kukamata maamuzi ya hekima. Kwa kweli, tunaweza kumuomba roho takatifu kwa sababu Yesu anatuhakikishia kama ‘Baba aliye mbinguni atawapa hata zaidi roho takatifu wale wanaomuomba!’—Luka 11:13.

Mwanaume anasali

“I consistently prayed to Jehovah for guidance in making the right decision.”—Kwabena,Ghana

Hata Yesu aliona ulazima wa kumuomba Baba yake musaada wakati alikamata maamuzi ya maana. Biblia inasema kama wakati alitaka kuchagua wanaume 12 wenye wangekuwa mitume wake, ‘aliendelea kusali kwa Mungu usiku wote.’—Luka 6:12.

Kama Yesu, watu wengi leo wametiwa moyo kwa kuona namna Mungu amesikiliza sala zao za kumuomba musaada ili kukamata maamuzi ya hekima. Regina, wa inchi ya Ufilipino, anasema juu ya magumu mbalimbali yenye amepata, kama vile kuhangaikia mahitaji yake na ya familia yake kisha bwana yake kufa, kupoteza kazi, na matatizo ya kulea watoto. Ni nini kimemusaidia kukamata maamuzi ya hekima? Anasema, “Ninapata musaada wa Yehova kupitia sala.” Kwabena, wa inchi ya Ghana, anasema sababu gani aliomba Mungu musaada, “Nilipoteza kazi yangu ya ujenzi yenye kulipa muzuri.” Juu ya maamuzi yenye alikuwa anafikiria kukamata, anasema, “Niliendelea kumuomba Yehova muongozo ili kukamata uamuzi wa muzuri.” Anasema tena, “Ninaamini kabisa kama Yehova alinisaidia kuchagua kazi yenye inaniwezesha kushugulikia mahitaji yangu ya kimwili na ya kiroho.” Kama unasali juu ya mambo yenye kugusa urafiki wako pamoja na Mungu, wewe pia unaweza kupata muongozo wake.

Tumetaja tu faida kidogo zenye sala inaweza kukuletea. (Ili kuona faida zingine, soma kisanduku “Faida za Sala.”) Lakini, ili upate faida hizo, ni lazima kwanza umujue Mungu na mapenzi yake. Kama unapenda kufanya hivyo, tunakutia moyo uombe Mashahidi wa Yehova wakusaidie kujifunza Biblia.a Hilo linaweza kuwa jambo la kwanza la kukusaidia umukaribie ‘Musikiaji wa sala.’—Zaburi 65:2.

a Ili kupata habari zingine, zungumuza na Mashahidi wa Yehova wa eneo lenu ao ufungue adresi yetu ya Internete, www.jw.org.

Faida za Sala

Amani ya akili: ‘Musihangaikejuu ya kitu chochote, bali [lakini] katika kila jambo kwa sala na dua [kuomba kwa bidii] pamoja na kutoa shukrani maombi yenu yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote itailinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili kwa njia ya Kristo Yesu.’—Wafilipi 4:6, 7.

Faraja kutoka kwa Mungu:‘Abarikiwe Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo, Baba ya rehema nyororo na Mungu wa faraja [kitulizo] yote, ambaye anatufariji katika ziki yetu yote.’—2 Wakorintho 1:3, 4.

Muongozo ili kukamata maamuzi ya hekima:‘Ikiwa yeyote kati yenu anakosa hekima, na aendelee kumuomba Mungu, kwa maana yeye anawapa wote kwa ukarimu na bila kushutumu; naye atapewa hiyo.’—Yakobo 1:5.

Musaada wa kuepuka majaribu: ‘Musali, ili musiingie katika jaribu.’—Luka 22:40.

Musamaha wa zambi: ‘Watu wangu ambao jina langu limeitwa juu yao wakijinyenyekeza na kusali na kutafuta uso wangu na wakigeuka kutoka katika njia zao mbaya, basi mimi nitasikia nikiwa mbinguni na kusamehe zambi yao.’—2 Mambo ya Nyakati 7:14.

Njia ya kusaidia wengine: ‘Dua ya mutu muadilifu . . . ina nguvu nyingi.’—Yakobo 5:16.

Kitia-moyo wakati sala zetu zinasikiwa: ‘Yehova akaendelea kumuambia [Sulemani]: Nimeisikia sala yako na ombi lako la kutaka kibali [kukubaliwa] ambalo uliomba kibali mbele zangu.’—1 Wafalme 9:3.

“Niliendelea kumuomba Yehova muongozo ili kukamata uamuzi wa muzuri.” —Kwabena, inchi ya Ghana

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine