Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp17 na. 4 uku. 11-12
  • Elias Hutter na Biblia Zake za Kiebrania Zenye Kuvutia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Elias Hutter na Biblia Zake za Kiebrania Zenye Kuvutia
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “UZURI WA TAFSIRI HIYO”
  • TAFSIRI YA KIEBRANIA YA “AGANO JIPYA”
  • MATOKEO YENYE KUENDELEA
  • Unakumbuka?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Tafsiri ya Biblia Yenye Kuwa Mwepesi Kueleweka
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Yehova Mungu, Anazungumuza na Watu Wake
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
wp17 na. 4 uku. 11-12

Elias Hutter na Biblia Zake za Kiebrania Zenye Kuvutia

UNAWEZA kusoma Kiebrania cha Biblia? Pengine hapana. Pengine haujaona hata siku moja Biblia ya Kiebrania. Lakini, unaweza kufurahia zaidi Biblia yako kwa kujifunza jambo fulani kupitia habari ya mutu mumoja mwenye elimu ya Biblia wa miaka ya 1500, mwenye kuitwa Elias Hutter, na pia kujua tafsiri mbili za Biblia ya Kiebrania zenye alichapisha.

Elias Hutter alizaliwa katika mwaka wa 1553 katika Görlitz, muji mudogo wenye kuwa karibu na mupaka wa sasa wa Ujerumani na Polandi na inchi ya Jamhuri ya Cheki. Hutter alijifunza luga za mashariki kwenye Masomo ya Juu ya Kilutheri katika Jena. Wakati alikuwa na miaka 24 hivi, aliwekwa kuwa profesa wa Kiebrania katika muji wa Leipzig. Akiwa mutu mwenye kuleta mabadiliko katika mambo ya elimu, alianzisha masomo katika muji wa Nuremberg; kwenye masomo hiyo wanafunzi wangeweza kujifunza Kiebrania, Kigiriki, Kilatini, na Kijerumani kwa muda wa miaka ine. Wakati huo, jambo hilo halikuwezekana kwenye masomo ya kawaida ao kwenye masomo ya juu.

“UZURI WA TAFSIRI HIYO”

Ukurasa wa kwanza wa Biblia ya Kiebrania ya Hutter ya 1587

Ukurasa wa kwanza wa Biblia ya Kiebrania ya Hutter ya 1587

Katika mwaka wa 1587, Hutter alitokeza tafsiri ya Kiebrania ya sehemu ya Biblia yenye watu wengi wanaita Agano la Kale. Tafsiri hiyo iliitwa Derekh ha-Kodesh, jina lenye kutoka katika andiko la Isaya 35:8 na linamaanisha “Njia ya Utakatifu.” Mupangilio muzuri wa maandishi unaonyesha wazi mafasirio yenye kusema kwamba “kila kitu kinashuhudia uzuri wa tafsiri hiyo.” Lakini jambo lenye lilifanya tafsiri hiyo ikuwe ya maana sana ni kwamba, wanafunzi wangeweza kuitumia kama chombo kizuri sana ili kujifunza Kiebrania.

Ili kuelewa sababu gani Biblia ya Kiebrania ya Hutter ilikuwa ya lazima sana, fikiria shida mbili zenye wanafunzi walipata wakati walikuwa wanasoma Biblia ya Kiebrania. Kwanza, Biblia ya Kiebrania inatumia alfabeti yenye kuwa tofauti na yenye haijulikane na watu wengi, na pili, viambishi (préfixes et suffixes) vyenye kutumiwa vinafanya ikuwe nguvu kujua neno la musingi. Kwa mufano, fikiria neno la Kiebrania: נפשׁ (ne’phesh), lenye kumaanisha “nafsi.” Kwenye Ezekieli 18:4, neno hilo liko na kiambishi ה (ha), chenye kumaanisha “ile,” na kufanyiza neno lenye kuwa na sehemu mbili הנפשׁ (han·ne’phesh), lenye kumaanisha moja kwa moja “ile nafsi.” Kwa mutu mwenye hana uzoefu, הנפשׁ (han·ne’phesh) inaweza kuonekana kuwa neno tofauti kabisa na נפשׁ (ne’phesh).

Ili kusaidia wanafunzi wake, Hutter alitumia ufundi muzuri wa uchapishaji: Mupangilio wa maandishi wenye kuwa na herufi za Kiebrania zenye kuwa nzito na pia zenye haziko nzito. Aliandika sehemu ya musingi ya kila neno kwa kutumia herufi nzito. Alitumia herufi zenye haziko nzito kwa ajili ya viambishi. Njia hiyo ilifanya ikuwe mwepesi kwa wanafunzi kutambua sehemu ya musingi ya neno la Kiebrania, na pia kuwasaidia katika kujifunza Kiebrania. Les Saintes Écritures. Traduction du monde nouveau (avec notes et références) inatumia njia kama hiyo katika maelezo ya chini.a Sehemu ya musingi inaandikwa na herufi nzito, na viambishi vinaandikwa kwa herufi za kawaida. Sehemu zenye kuonyeshwa wazi katika picha zinaonyesha mupangilio wa maneno katika Biblia ya Kiebrania ya Hutter kwenye Ezekieli 18:4 na pia mupangilio wenye kutumiwa katika maelezo ya chini ya Bible avec notes et références kwenye mustari huo.

Ezekieli 18:4 katika Biblia ya Kiebrania ya Hutter, na katika maelezo ya chini ya Les Saintes Écritures. Traduction du monde nouveau (avec notes et références

TAFSIRI YA KIEBRANIA YA “AGANO JIPYA”

Hutter alichapisha pia sehemu ya Biblia yenye watu wengi wanaita Agano Jipya, ikiwa na maandishi katika luga 12. Tafsiri hiyo ilitolewa katika mwaka wa 1599 na mara nyingi inaitwa Polyglotte de Nuremberg. Hutter alipenda kutia ndani Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika luga ya Kiebrania. Lakini, alisema kwamba hata kama “angekuwa tayari kulipa feza nyingi” kwa ajili ya tafsiri kama hiyo ya Kiebrania, utafiti ungekuwa kazi bure.b Kwa hiyo, aliamua yeye mwenyewe kutafsiri Agano Jipya katika Kiebrania kutoka katika Kigiriki. Akiacha mipango ingine pembeni, Hutter alimaliza kazi yote ya kutafsiri katika mwaka moja tu!

Tafsiri ya Kiebrania ya Hutter ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ilikuwa nzuri kadiri gani? Katika mwaka wa 1891 Franz Delitzsch, Mwebrania mwenye kuwa na elimu, aliandika hivi: “Tafsiri yake ya Kiebrania inafunua uelewaji wa luga wenye haupatikane kwa urahisi kati ya Wakristo na ingali inasomwa, kwa sababu mara nyingi alichagua kwa usahihi maneno yenye kufaa.”

MATOKEO YENYE KUENDELEA

Kazi ya Hutter ya kutafsiri haikumuletea utajiri; ni wazi kwamba tafsiri zake hazikuuzwa sana. Hata hivyo, kazi yake imekuwa ya maana sana na imekuwa pia na matokeo yenye kuendelea. Kwa mufano, tafsiri yake ya Kiebrania ya Agano Jipya ilirekebishwa na kuchapwa tena katika mwaka wa 1661 na William Robertson na kisha tena na Richard Caddick katika mwaka wa 1798. Kwa kutafsiri kutoka katika Kigiriki cha zamani, Hutter alitafsiri kwa njia yenye kufaa majina ya cheo Kyʹri·os (Bwana) na The·osʹ (Mungu) kama “Yehova” (יהוה, JHVH) kila mahali penye Maandiko ya Kiebrania yalitajwa ao kila mahali penye aliona kama Maandiko yalikuwa yanazungumuzia Yehova. Jambo hilo ni lenye kupendeza kwa sababu hata kama tafsiri nyingi za Agano Jipya hazitumie jina la pekee la Mungu, tafsiri ya Hutter ni ushuhuda mwingine wenye kuunga mukono kurudishwa kwa jina la Mungu katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo.

Wakati utaona tena jina la Mungu, Yehova, katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo ao wakati utaona jina hilo katika maelezo ya chini ya Bible avec notes et références, kumbuka kazi ya Elias Hutter na pia Biblia zake za Kiebrania zenye kuvutia.

a Ona maelezo ya pili yenye kuwa chini kwenye andiko la Ezekieli 18:4 na Appendice 3B katika Bible avec notes et références.

b Ni wazi kwamba, watu wenye elimu ya Biblia walikuwa tayari wametokeza tafsiri za Kiebrania za Agano Jipya. Mumoja kati yao, alikuwa Simon Atoumanos, mutawa wa Bizantini, katika mwaka wa 1360 hivi. Mwengine alikuwa Oswald Schreckenfuchs, wa Ujerumani, katika mwaka wa 1565 hivi. Tafsiri hizo hazikuchapishwa hata siku moja na leo zimekwisha kupotea.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine