Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp18 na. 1 uku. 3
  • Muongozo wa Biblia Ni Wenye Faida Leo?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Muongozo wa Biblia Ni Wenye Faida Leo?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2018
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Utangulizi
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2018
  • Mambo ya Muzuri na ya Mubaya: Biblia Ni Muongozo Wenye Kutumainika
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2024
  • Endelea Kufuata Muongozo wa Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Habari Zenye Kuwa mu Gazeti Hili la Amuka!: Je, Biblia Inaweza Kukuletea Faida Katika Maisha?
    Amuka!—2019
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2018
wp18 na. 1 uku. 3

Muongozo wa Biblia Ni Wenye Faida Leo?

WATU FULANI WANASEMA HAPANA. Munganga mumoja alilinganisha kutumia Biblia ili ituongoze na kutumia kitabu fulani chenye kiliandikwa katika miaka ya 1920 ili kufundisha kemia (chimie). Mutu mwenye haheshimie Biblia anaweza hata kuuliza ikiwa mutu anaweza kusoma kitabu chenye kuonyesha namna ya kutumikisha ordinatere ya zamani ili kujua namna ya kutumikisha ordinatere ya sasa. Katika maneno mengine, watu fulani wanafikiri kuwa Biblia ni ya zamani sana na kuwa haiwezi tena kutumainiwa.

Sababu gani mutu atumie muongozo huo wa zamani katika ulimwengu wa leo wenye umefanya maendeleo katika mambo ya teknolojia? Zaidi ya hilo, site nyingi za Internete zinaendelea kutoa mashauri mengi na muongozo wa hivi karibuni. Programu mbalimbali kwenye televizyo zinatoa mashauri kutoka kwa wanasaikolojia (psychologues) wenye uzoefu, walimu wenye kufundisha namna ya kuishi, na waandikaji wa vitabu, wakiingiza mamiliare ya dola.

Kwa sababu kuko habari za sasa zenye zinatolewa kila dakika, sababu gani tutafute muongozo katika Biblia​—kitabu chenye kilimalizika kuandikwa kumepita karibu miaka 2000? Je, watu wenye hawaheshimie Biblia hawaseme kweli wakati wanasema kuwa kutumia kitabu hicho cha zamani ili kituongoze ni kama vile kutumia kitabu cha zamani chenye kufundisha kemia ao kitabu cha zamani chenye kuonyesha namna ya kutumia ordinatere? Kwa kweli, mawazo hayo ni yenye makosa. Sayansi na teknolojia vinabadilika haraka sana, lakini mahitaji ya musingi ya wanadamu yamebadilika? Watu wangali wanatafuta maisha yenye kusudi na pia kuishi kwa furaha na usalama kwa kiasi fulani, kuishi muzuri na watu wa familia, na kuwa na marafiki wazuri.

Hata kama Biblia ni kitabu cha zamani, inazungumuzia mambo hayo na mengine zaidi. Pia, imeongozwa na roho ya Muumbaji wetu. Inatuongoza katika kila hatua ya maisha yetu na kututolea mambo yenye tuko nayo lazima ili kupambana na magumu yoyote yenye yanatusumbua. (2 Timotheo 3:16, 17) Zaidi ya hilo, Biblia inatutolea mashauri yenye hayana mwisho​—mashauri yenye kuwa na faida sikuzote! Biblia yenyewe inasema hivi: “Neno la Mungu liko hai.”​—Waebrania 4:12.

Mambo yenye Biblia inasema yanaweza kabisa kuwa ya kweli? Imepoteza faida yake, ao inaendelea kabisa kuwa kitabu chenye kuwa na mashauri ya muzuri na yenye faida leo, ni kusema, kitabu chenye kuwa hai? Kusudi la gazeti hili Munara wa Mulinzi, la kwanza kati ya magazeti ya pekee yenye yatafuatana, ni kukusaidia kupata majibu ya maulizo hayo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine