Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp24 na. 1 uku. 6-9
  • Mambo ya Muzuri na ya Mubaya: Biblia Ni Muongozo Wenye Kutumainika

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mambo ya Muzuri na ya Mubaya: Biblia Ni Muongozo Wenye Kutumainika
  • Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2024
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • TUKO NA LAZIMA YA MUONGOZO WA MUNGU
  • NAMNA BIBLIA INAONYESHA MUONGOZO WA MUNGU
  • Musaada Zaidi Kwa Ajili Ya Familia
    Amuka!—2018
  • Kuko Muongozo Wenye Kutumainika Wenye Unaweza Kutusaidia Kuwa na Maisha ya Muzuri Wakati Wenye Kuja?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Mambo ya Muzuri na ya Mubaya: Uamuzi Wenye Unapaswa Kukamata
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2024
  • Unaweza Kupata Musaada
    Amuka!—2020
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2024
wp24 na. 1 uku. 6-9

Mambo ya Muzuri na ya Mubaya: Biblia Ni Muongozo Wenye Kutumainika

Hatuwezi kuwa hakika kama maamuzi yetu itakuwa na matokeo ya muzuri kama tu inategemea namna tunajisikia ao mawazo ya wengine. Biblia inaonyesha juu ya nini, lakini pia inafasiria mambo mingi zaidi. Inatusaidia tujue mambo ya muzuri na ya mubaya, na ile njo siri ya kuwa na maisha yenye furaha.

TUKO NA LAZIMA YA MUONGOZO WA MUNGU

Mu Biblia, Yehovaa Mungu anafasiria kama wanadamu wako na lazima ya muongozo wake na hawawezi kujiongoza wao wenyewe. (Yeremia 10:23) Njo maana, alitupatia kanuni za kutuongoza zenye kupatikana mu Biblia. Anapenda familia ya wanadamu na hapendi tukamate maamuzi ya mubaya yenye itatuumiza na kufanya maisha yetu ikuwe nguvu. (Kumbukumbu la Torati 5:29; 1 Yohana 4:8) Zaidi ya ile, juu ni Muumbaji wetu, iko na hekima na ujuzi mingi ili kutupatia mashauri ya muzuri zaidi. (Zaburi 100:3; 104:24) Lakini, Mungu halazimishake watu waishi kulingana na kanuni zake.

Yehova alipatia mwanaume na mwanamuke wa kwanza Adamu na Eva kila kitu yenye walikuwa nayo lazima juu wakuwe na maisha yenye furaha. (Mwanzo 1:28, 29; 2:8, 15) Na aliwapatia maagizo ya mwepesi yenye alitazamia kama wangetii. Lakini, aliwapatia pia uhuru wa kuchagula kama watatii ile maagizo ao hapana. (Mwanzo 2:9, 16, 17) Jambo ya kuhuzunisha ni kama, Adamu na Eva walichagula kuishi kulingana na kanuni zao wenyewe kuliko kuishi kulingana na kanuni za Mungu. (Mwanzo 3:6) Ile ilileta matokeo gani? Wanadamu wanaweza kweli kujiamulia mambo ya muzuri na ya mubaya? Hapana. Kwa miaka mingi inaonekana kama kuacha kufuata kanuni za Yehova hailetake amani na furaha ya milele.—Muhubiri 8:9.

Biblia inatupatia muongozo wenye tuko nao lazima ili tukamate maamuzi ya hekima juu ya mwenendo hata kama tunaishi wapi, ao hata kama familia yetu ni ya namna gani. (2 Timoteo 3:16, 17; ona kisanduku “Kitabu ya Watu Wote.”) Ona namna Biblia inafanyaka vile.

Ona juu ya nini inafaa kabisa kuita Biblia “neno la Mungu.”—1 Watesalonike 2:13. Angalia video Ni Nani Aliandikisha Biblia? ku jw.org.

KITABU YA WATU WOTE

Tunaweza kutazamia kama Muumbaji mwenye upendo na mwenye hekima anapaswa kufanya muongozo wake ukuwe mwepesi kupatikana kwa watu wote. Fikiria hii mambo kuhusu Biblia:

Watu wa mu inchi mbalimbali wako nasoma Biblia. Biblia za papier na za kielektroniki ziko mbele yao.
  • Zaidi ya 3500 Ile ni hesabu ya luga zenye Biblia imetafsiriwa yote ao kwa sehemu; hakuna kitabu ingine yenye imetafsiriwa mu luga za mingi sawa ile.

  • Zaidi ya 5000000000 Ile ni hesabu ya kopi za Biblia zenye zimechapishwa; hakuna kitabu ingine yenye iko sawa ile.

Biblia haionyeshe kama rangi fulani ya ngozi, taifa fulani, kabila ao desturi fulani ni ya muzuri zaidi kuliko ingine. Kusema kweli ni kitabu ya watu wote.

Soma Biblia ku Enternete ku jw.org (inapatikana mu luga zaidi ya 250)

Mwanaume moya iko nasoma Biblia na iko nashota kidole kwenye iko nasoma.

JUU YA NINI WATU FULANI HAWAONAKE BIBLIA KUWA YA MAANA?

Watu fulani wanawazaka kama Biblia haiwezi kabisa kuwaongoza muzuri. Wanaweza kusema hivi:

Mawazo ya watu: “Biblia inajipingaka.”

Kweli njo hii: Inaweza kuonekana sawa vile sehemu fulani za Biblia zinapingana na zingine, lakini kama unatafuta kujua namna na wakati wenye ile Maandiko iliandikwa utaona kama haipingane hata kidogo.

Juu ya kuona mifano fulani, soma habari “Je, Biblia Inajipinga Yenyewe?” ku jw.org.

Mawazo ya watu: “Watu wenye wanasemaka kama wanafuataka Biblia, wanafanyaka mambo ya mubaya. Sasa, Biblia inaweza kutuongoza namna gani?”

Kweli njo hii: Kama watu wako na tabia ya mubaya juu hawatumikishe mafundisho ya Biblia, ile haiko kosa ya Biblia. Ayo peke ilisemaka hata mbele ya wakati kama watu wengi, kutia ndani viongozi wa dini wenye kusema kama wanatii mambo yenye Biblia inasema, wangejiendesha mu njia yenye kuwa tofauti kabisa na mambo yenye kuwa ndani. Ilisemaka pia kama mafundisho ya Biblia ‘ingetukanwa.’—2 Petro 2:1, 2.

Juu ya kuona mufano moya wenye unaonyesha namna viongozi wa dini wamefanya mambo yenye inapingana kabisa na mafundisho ya Biblia, soma habari “Je, Dini Ni Biashara?” ku jw.org.

Mawazo ya watu: “Watu wenye wanafanyaka mambo yenye Biblia inafundisha hawaheshimiake wengine wenye kuwa tofauti nao.”

Kweli njo hii: Biblia inatia watu moyo waheshimie wengine. Haiunge mukono. . .

  • kujiona kuwa wa maana zaidi kupita wengine.—Wafilipi 2:3.

  • kutoheshimia watu wenye kuwa tofauti na siye ao wenye wako na imani tofauti na yetu.—1 Petro 2:17.

  • kukaza wengine wakubali mawazo yetu.—Matayo 10:14.

Biblia inaonyesha kama Mungu anatendeaka tu watu muzuri na anapenda na siye tufanye vile.—Waroma 9:14.

Juu ya kujua mambo mingi zaidi, usome habari “Kuvumilia Wengine—Biblia Inaweza Kukusaidia” ku jw.org.

NAMNA BIBLIA INAONYESHA MUONGOZO WA MUNGU

Biblia inatuambia juu ya uhusiano wenye Mungu alikuwa nao pamoya na wanadamu tangu mwanzo. Mambo yenye kuwa mu Biblia inatusaidia kujua mawazo ya Mungu juu ya mambo ya muzuri na ya mubaya, mambo yenye kutuletea faida na hatari. (Zaburi 19:7, 11) Mambo yenye tunajifunzaka mu Biblia inakuwaka tu ya kweli, na itatusaidia tukamate maamuzi ya hekima juu ya mwenendo mu maisha yetu ya kila siku.

Kwa mufano, tufikirie shauri yenye kupatikana mu Mezali 13:20: “Mwenye anatembea na wenye hekima atakuwa na hekima, lakini mwenye kufanya urafiki na wajinga ataumia.” Hii kanuni inaendelea kutusaidia leo, sawa tu vile ilikuwa nawasaidia watu zamani. Mu Biblia muko kanuni mingi sana zenye zinaweza kutusaidia na zenye ni za maana.—Ona kisanduku “Mashauri ya Biblia Inakuwaka tu na Faida.”

Lakini, pengine unaweza kujiuliza hivi: ‘Namna gani naweza kuwa hakika kama mashauri ya Biblia inaweza kunisaidia leo?’ Mu habari yenye kufuata tutazungumuzia mifano fulani ya mu wakati wetu.

a Yehova njo jina ya pekee ya Mungu.—Zaburi 83:18.

MASHAURI YA BIBLIA INAKUWAKA TU NA FAIDA

Hata kama Biblia iliandikwa kumepita karibu miaka 2000, inaendelea tu kuwa na faida leo. Watu wako na lazima ya mambo ileile sawa zamani, ni kusema, wangali tu na lazima ya kuwa na maisha ya muzuri na yenye furaha. (Muhubiri 1:9) Mashauri yenye kuwa mu Biblia ingali inaweza kutusaidia kufikia ile maisha.

Kuwa Munyoofu

  • “Tunataka kujiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.”—Waebrania 13:18.

  • “Ule mwenye kuiba asiibe tena; lakini afanye kazi kwa bidii.”—Waefeso 4:28.

Kuishi Muzuri na Wengine

  • “Kila mumoja aendelee kutafuta, hapana faida yake mwenyewe, lakini faida ya ule mutu mwingine.”—1 Wakorinto 10:24.

  • “Muendelee kuvumiliana na kusameheana kwa kupenda.”—Wakolosai 3:13.

Kukamata Maamuzi

  • “Mujinga anaamini kila neno, lakini mwerevu anafikiria sana kila hatua.”—Mezali 14:15.

  • “Mutu mwerevu anaona hatari na kujificha, lakini wenye hawana uzoefu wanaendelea mbele na kupata matokeo ya mubaya.”—Mezali 22:3.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine