Mambo ya Muzuri na ya Mubaya: Uamuzi Wenye Unapaswa Kukamata
Kanuni zenye tunachagula mu maisha njo zitaonyesha kama tutakuwa na furaha ao hapana. Yehova anajua vile. Na njo maana anapenda tuishi kulingana na kanuni zake.
Yehova anapenda tukuwe na amani na furaha mu maisha.
“Mimi, Yehova, niko Mungu wako, mwenye anakufundisha ili ujipatie faida, mwenye anakuongoza katika njia yenye unapaswa kutembea ndani yake. Kama tu ungesikiliza amri zangu! Basi amani yako ingekuwa kama vile muto na haki yako kama mawimbi ya bahari.”—Isaya 48:17, 18.
Juu ni Muumbaji wetu, Mungu anajua namna ya muzuri zaidi ya siye wanadamu kuishi. Wakati tunafuata mambo yenye Mungu anatuambia, hatutahangaika kama ile itatuletea matokeo ya muzuri ao hapana. Tutakuwa tu tunakamata maamuzi ya muzuri, yenye itatuletea amani na furaha.
Yehova hatuombe tufanye mambo yenye inapita uwezo wetu.
“Amri hii yenye ninakuamuru leo haiko nguvu sana kwako, wala haiko kwenye hauwezi kufika.”—Kumbukumbu la Torati 30:11.
Kuishi kulingana na kanuni za Mungu inaweza kuomba tubadilishe namna yetu ya kuwaza na ya kutenda. Lakini, Yehova hatuombe kufanya mambo yenye inapita uwezo wetu. Kusema kweli, juu ni Muumbaji wetu, anajua mambo yenye tuko na uwezo wa kufanya. Na wakati tunafikia kumujua Yehova, tutavumbula kama “amri zake haziko muzigo muzito.”—1 Yohana 5:3.
Yehova anasema kama atasaidia wale wenye wanachagula kufuata kanuni zake.
“Mimi, Yehova Mungu wako, ninashika mukono wako wa kuume, ni mimi mwenye kukuambia, ‘Usiogope. Nitakusaidia.’”—Isaya 41:13.
Inawezekana tuishi namna Yehova anapenda juu atatusaidia. Anaweza kutusaidia kupitia Neno yake Biblia, yenye inatutia moyo na kutupatia tumaini.
Mamilioni ya watu mu dunia yote wamefikia kuona kama kuishi kulingana na kanuni za Biblia kumefanya maisha yao ikuwe muzuri zaidi. Hauone kama inaweza kuwa muzuri ujifunze mambo mingi zaidi juu ya mashauri yenye Biblia inatupatia? Juu ya kufanya vile, unaweza kuanzia kujifunza broshua Furahia Maisha Milele! yenye inategemea Biblia na yenye inapatikana ku jw.org bila kulipa. Ndani muko hizi somo:
Unawaza Biblia Inaweza Kukusaidia?
Biblia Inatupatia Tumaini
Unaweza Kuamini Mambo Yenye Biblia Inasema?
Wakati uko najifunza Neno ya Mungu Biblia, utaona kama haiko kitabu yenye ilishapitwa na wakati, lakini ni kitabu yenye ‘inategemeka sikuzote, sasa na milele.’ (Zaburi 111:8) Kuishi kulingana na kanuni za Biblia njo njia ya muzuri zaidi ya maisha. Lakini, Mungu hatulazimishe kufanya vile. (Kumbukumbu la Torati 30:19, 20; Yoshua 24:15) Ni uamuzi wenye kila mutu anapaswa kukamata.