Wapi njo Tunaweza Kupata Muongozo Wenye Kutumainika Leo?
Mu hii dunia yenye mambo iko nabadilika-badilika, nini itakusaidia ukuwe hakika kama maamuzi yenye unakamata itakuletea furaha? Nini njo itakusaidia ukuwe hakika kama mambo yenye inaonekana muzuri leo haitaonekana mubaya kesho?
Biblia itakusaidia ukamate maamuzi yenye hautahuzunikia kisha. Ile inawezekana namna gani? Biblia ni kitabu ya Muumbaji wetu, na anajua mambo yenye inaweza kutuletea kabisa furaha ya kweli na usalama wa kweli.
“Amekuambia mambo mema.”—Mika 6:8.
Tunaweza kutumainia mashauri ya hekima yenye kuwa mu Biblia. Inakuwaka tu yenye ‘kutegemeka sikuzote, sasa na milele.’—Zaburi 111:8.
Unawaza namna gani kama weye peke unachunguza ili kuona namna Biblia inaweza kukusaidia mu hii dunia mwenye mambo iko nabadilika-badilika?