Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp18 na. 1 uku. 12-13
  • 3 Inasaidia Kuvumilia Matatizo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 3 Inasaidia Kuvumilia Matatizo
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2018
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • UGONJWA WENYE KUKAWIA
  • HUZUNI
  • Kusali Kunaweza Kukuletea Faida Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Sala— Inaweza Kukuletea Faida Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2018
wp18 na. 1 uku. 12-13

3 Inasaidia Kuvumilia Matatizo

Kuko matatizo yenye kwa sasa hatuwezi kuepuka wala kumaliza. Kwa mufano, ikiwa mutu mwenye ulipenda amekufa ao ikiwa uko na ugonjwa wenye kukawia, pengine jambo lenye unaweza tu kufanya ni kutafuta namna ya kuvumilia maumivu yako. Je, Biblia inaweza kusaidia katika hali hizo ngumu?

UGONJWA WENYE KUKAWIA

Rose anasema hivi: “Niko na ugonjwa wa chembe za uriti wenye unaniletea maumivu makali na yenye kuendelea. Afya yangu imekuwa ya mubaya sana.” Jambo lenye lilimuhangaisha zaidi ni kwamba wakati fulani alishindwa kukaza akili yake juu ya funzo lake la Biblia na juu ya mambo ya kiroho. Lakini alipata musaada katika maneno ya Yesu yenye kuwa katika Mathayo 19:26: “Kwa Mungu mambo yote yanawezekana.” Rose alielewa kuwa kuko njia mbalimbali zenye zinaweza kusaidia mutu kujifunza. Kwa sababu ya maumivu yake, wakati fulani ilikuwa nguvu sana kwake kusoma. Kwa hiyo, alianza kufuata usomaji wa kusikiliza tu wa Biblia na wa vichapo vyenye kutegemea Biblia.a Anasema hivi: “Bila kufanya hivyo, sijue namna gani ningeweza kufanya urafiki wangu pamoja na Yehova uendelee kuwa muzuri.”

Wakati Rose anahuzunika kwa sababu anashindwa kufanya jambo fulani lenye angeweza kufanya zamani, anapata kitulizo katika maneno yenye kuwa katika 2 Wakorintho 8:12: ‘Ikiwa utayari upo kwanza, unakubalika zaidi kulingana na kile ambacho mutu iko nacho, si kulingana na kile ambacho mutu hana.’ Maneno hayo yanamukumbusha Rose kuwa Mungu anapendezwa na mambo yenye anafanya, kwa sababu anafanya mambo yote kulingana na uwezo wake.

HUZUNI

Delphine, mwenye tulizungumuzia mwanzoni, anakumbuka hivi: “Kisha mutoto wangu mwanamuke wa miaka 18 kufa, nilikuwa na huzuni kubwa sana hivi kwamba sikukuwa ninaamini kama ninaweza kuendelea kuishi. Hakuna kile chenye kingeweza kunituliza.” Lakini, alipata kitulizo kikubwa katika maneno ya Zaburi 94:19. Katika andiko hilo, mwandikaji mumoja wa zaburi aliambia Mungu hivi: ‘Fikira zangu zinazofazaisha zilipokuwa nyingi ndani yangu, faraja zako mwenyewe zilianza kuikumbatia nafsi yangu.’ Delphine anasema, “Nilisali kwa Yehova ili anisaidie kupata mambo ya kufanya yenye yangenisaidia kutuliza maumivu yangu.”

Alianza kufanya kazi ya kujitolea. Mwishowe, akaanza kujilinganisha na crayon yenye mutoto anachoraka nayo, yenye inaendelea kutumiwa ili kuchora hata kama ni yenye kuvunjika. Vilevile, hata kama alijisikia kuwa mwenye kuvunjika, alielewa kwamba alikuwa angali na uwezo wa kusaidia wengine. Anakumbuka hivi: “Kwa kushtukia, nilitambua kuwa wakati nilitumia kanuni za Biblia na mawazo ya Maandiko ili kutuliza watu wenye nilikuwa ninajifunza nao Biblia, hiyo ilikuwa njia yenye Yehova alikuwa anatumia ili kunituliza na kunitia nguvu.” Alifanya liste ya watu mbalimbali wenye kuzungumuziwa katika Biblia wenye walipatwa na huzuni nyingi. Alitambua kuwa, “Wote walikuwa watu wenye walikuwa wanasali kwa ukawaida.” Alijifunza pia kuwa mutu “hawezi kupata nguvu za kuvumilia ikiwa hasomake Biblia.”

Kujifunza Biblia kumefundisha Delphine jambo lingine: kukaza akili juu ya mambo ya wakati wenye kuja, hapana juu ya mambo yenye yamekwisha kupita. Tumaini lenye kuzungumuziwa katika Matendo 24:15 linamutuliza: “Kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia.” Namna gani anaonyesha kuwa iko hakika kwamba Yehova atamufufua mutoto wake? Tuache Delphine mwenyewe atoe jibu. Anasema hivi: “Ninamuona mutoto wangu mwanamuke wakati wenye kuja. Yehova amekwisha kupanga ‘siku’ nitamuona tena mutoto wangu. Ninajiona kabisa mimi pamoja naye katika bustani yetu kama vile tu nilimuona na kumupenda siku yenye alizaliwa.”

a Habari nyingi kama hizo za kusikiliza tu zinapatikana kwenye site ya Internete jw.org.

Biblia inaweza kukusaidia kupata kitulizo hata wakati wa magumu mengi

NAMNA GANI MUNGU ANAWEZA KUTUSAIDIA?

Jibu la Biblia liko wazi. Biblia inasema hivi: ‘Yehova yuko karibu na wote wanaomuitia, wote wanaomuitia yeye katika ukweli. Atawatimizia wale wanaomuogopa tamaa yao, naye atasikia kilio chao cha kuomba musaada, naye atawaokoa.’ (Zaburi 145:18, 19) Je, jambo hilo halitutie moyo? Lakini, namna gani, Mungu anajibu sala za watu wenye wanatafuta kwa moyo wote muongozo wake?

KWA KUTUPATIA NGUVU:

Mara nyingi, matatizo yanaweza kutuvunja moyo na kutuchokesha; kimwili, kiakili, na kiroho. (Methali 24:10) Lakini, Yehova ‘anamupa nguvu mutu aliyechoka; naye anazijaza nguvu kamili kwa mutu asiye na nguvu.’ (Isaya 40:29) Mutume Paulo, mwenye alivumilia majaribu makali, anasema hivi: “Kwa mambo yote nina nguvu kupitia yeye anayenipa nguvu.” (Wafilipi 4:13) Paulo alitiwa nguvu na roho takatifu ya Mungu. Wewe pia unaweza kumuomba Mungu akupatie roho takatifu.​—Luka 11:13.

KWA KUTUPATIA HEKIMA:

Utafanya nini ikiwa uko na lazima ya musaada ili kuelewa na kutumikisha mashauri ya Biblia? Mwanafunzi Yakobo aliandika hivi: ‘Ikiwa yeyote kati yenu anakosa hekima, na aendelee kumuomba Mungu, kwa maana yeye anawapa wote kwa ukarimu na bila kushutumu; naye atapewa hiyo.’ (Yakobo 1:5) Unaweza kutenda kulingana na sala zako kwa kusoma Biblia na kutumikisha mafundisho ya Biblia. (Yakobo 1:23-25) Wakati unafanya hivyo, utajionea mwenyewe kwamba mashauri yake ni yenye hekima sana.

KWA KUTUPATIA AMANI:

Hata wakati unapambana na mahangaiko makubwa, Yehova anaweza kukusaidia upate kitulizo. Neno lake linasema hivi: ‘Musihangaike juu ya kitu chochote, bali katika kila jambo kwa sala na dua pamoja na kutoa shukrani maombi yenu na yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote itailinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili kwa njia ya Kristo Yesu.’ (Wafilipi 4:6, 7) Sababu gani usimuombe Yehova akupatie amani?

Lakini, utafanya nini ikiwa matatizo yako hayamalizike haraka? Usiseme mara moja kuwa Mungu amekuacha. Hata kama matatizo yako yanakawia, Mungu anaweza kukupatia ujasiri na nguvu ili uweze kuvumilia. (1 Wakorintho 10:13) Pia, Biblia inaahidi kuwa wakati utakuja wenye matatizo yetu yatamalizika milele!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine