Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp19 na. 2 uku. 6-7
  • Wakati Mutu Mwenye Unapenda Anakufa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wakati Mutu Mwenye Unapenda Anakufa
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAMBO YENYE INAWEZA KUKUSAIDIA UVUMILIE
  • Namna ya Kupiganisha Huzuni Yako
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • ‘Mulie Pamoja na Watu Wanaolia’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Mambo Yenye Unapaswa Kutazamia
    Amuka!—2018
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
wp19 na. 2 uku. 6-7
Bibi na bwana wenye wamefiwa wako pembeni ya bahari wanakamatana mikono na wanaangalia mbele yao

Wakati Mutu Mwenye Unapenda Anakufa

“Wakati ndugu yangu mukubwa alikufa kwa kushtukia, niliishiwa. Miezi mingi kisha, ningemukumbuka kwa kushtukia na kusikia maumivu. Ilikuwa kama vile nilikuwa ninachomwa kisu ndani yangu. Wakati fulani, nilikasirika pia. Juu ya nini ndugu yangu alikufa? Na nilijisikia kuwa mwenye kosa kwa sababu sikupitisha wakati mingi pamoja naye.”​—Vanessa, katika Australia.

IKIWA ulifiwa na mupendwa wako, pengine wewe pia ulipata hisia mingi mbalimbali, kama vile huzuni, kujisikia kuwa peke yako, na kuishiwa. Pengine pia ulikasirika, ulijilaumu, na uliogopa. Pengine hata ulijiuliza ikiwa maisha ingali na maana.

Ukuwe hakika kama huzuni haiko alama ya uzaifu. Ile inaonyesha kama ulihangaikia sana mupendwa wako. Lakini, inawezekana kupata kiasi fulani cha kitulizo kutokana na huzuni yako yenye kuumiza?

MAMBO YENYE INAWEZA KUKUSAIDIA UVUMILIE

Hata kama inaweza kuonekana kama maumivu yako haitaishaka, unaweza kupata kitulizo ikiwa unatumikisha mapendekezo yenye kufuata:

USIJIZUIE KUONYESHA HUZUNI

Watu wote hawaonyeshe huzuni kwa njia ileile na hawafanye muda uleule. Lakini, kulia kunaweza kufanya maumivu yako ipunguke. Vanessa, mwenye tulitaja mwanzoni, anasema hivi: “Ningelia tu; nilikuwa na lazima ya kutuliza maumivu.” Sofía, mwenye dada yake alikufa kwa kushtukia, anasema hivi: “Kufikiria mambo yenye ilitokea kunaumiza sana, ni kama vile kufungua na kusafisha kidonda chenye kuoza. Haiko mwepesi kuvumilia maumivu, lakini ile inasaidia kidonda kipone.”

ELEZEA WENGINE MAWAZO YAKO NA NAMNA UNAJISIKIA

Wakati fulani unaweza kupenda kuwa peke yako, na ile inaeleweka. Lakini, kuvumilia maumivu peke yako ni kama vile kujaribu kubeba peke yako kitu chenye kuwa kilo sana. Jared, mwenye kuwa na miaka 17, mwenye alifiwa na baba yake, anakumbuka hivi: “Nilielezea wengine namna nilijisikia. Siko hakika kama niliongea mambo yenye kueleweka, lakini ninafurahi kuwa niliweza kuelezea wengine namna nilijisikia.” Janice, mwenye tulitaja katika habari ya kwanza, anaonyesha faida ingine: “Kuzungumuza na wengine kulinituliza kwa njia kubwa. Nilijisikia kuwa walinielewa, na sikujisikia kuwa peke yangu.”

KUBALI MUSAADA

Munganga mumoja anasema hivi: “Wakati watu wenye wamefiwa wanaruhusu marafiki na watu wa familia wawasaidie muda mufupi kisha kufiwa na mupendwa wao, mara mingi inakuwa mwepesi kuvumilia na kupata ushindi juu ya huzuni yao.” Uruhusu marafiki wako wajue mambo yenye wanaweza kufanya ili kukusaidia; bila shaka wanapenda kukusaidia, lakini pengine hawajue namna ya kufanya vile.​—Mezali 17:17.

UMUKARIBIE MUNGU ZAIDI

Tina anasema hivi: “Wakati bwana yangu alikufa kwa kushtukia na ugonjwa wa kansere, singeweza tena kumuambia namna nilijisikia, kwa hiyo, ningemuambia Mungu kila kitu! Nilianza kumuomba kila siku anisaidie niweze kuvumilia. Mungu alinisaidia katika njia mingi sana.” Tarsha, mwenye alikuwa na miaka 22 wakati mama yake alikufa, anasema hivi: “Kusoma Biblia kila siku kulinipatia kitulizo. Kulifanya nikuwe na jambo fulani la kufikiria lenye kutia moyo.”

UWAZIE WAKATI WENYE MUPENDWA WAKO ATAFUFULIWA

Tina anaongeza hivi: “Mwanzoni, tumaini la ufufuo halikunituliza juu nilikuwa na lazima ya bwana yangu​—na watoto wangu walikuwa na lazima ya baba yao​—ileile wakati. Lakini, sasa, kisha miaka 4, ninashikamana na tumaini hilo. Ile inanisaidia kuvumilia. Ninawazia wakati wenye nitamuona tena, na ile inaniletea amani na furaha kubwa!”

Pengine hautajisikia muzuri palepale. Lakini hali ya Vanessa inaweza kututia moyo. Anasema hivi: “Unaweza kuwaza kuwa mambo haitakuwa muzuri, lakini hatua kwa hatua utajisikia muzuri.”

Ukumbuke, hata kama utaendelea kukosa mupendwa wako, maisha itakuwa ingali tu na maana. Kupitia musaada wa Mungu wenye upendo, unaweza kuendelea kuwa na marafiki wazuri na maisha yenye kusudi. Na hivi karibuni Mungu atafufua wafu. Anapenda uweze tena kumukumbatia mupendwa wako. Ile wakati maumivu yenye kuwa ndani ya moyo wako itapona milele!

Maandiko ya Biblia Yenye Inaweza Kusaidia

Mungu anaona huzuni na machozi yako.

Muandikaji mumoja wa Biblia alisema hivi: “Kusanya machozi yangu katika chupa yako ya ngozi. Je, hayaandikwe katika kitabu chako?”​—Zaburi 56:8.

Unaweza kumufungulia Mungu moyo wako.

“Mbele [ya Mungu] ninamwanga mahangaiko yangu . . . ninakuita unisaidie, Ee Yehova.”a​—Zaburi 142:2, 5.

Unaweza kuwa na tumaini.

“Kutakuwa ufufuo.”​—Matendo 24:15.

Mungu anaahidi kama atafufua watu wengi sana wenye wamekufa, na iko na tamaa sana ya kufanya vile.b​—Yobu 14:14, 15.

a Yehova ni jina la Mungu kama vile inaonyeshwa katika Biblia.

b Ili kupata habari zaidi kuhusu ufufuo, ona somo ya 30 ya kitabu Furahia Maisha Milele! chenye kuchapishwa na Mashahidi wa Yehova na unaweza kukichukua bila kulipa ku www.jw.org.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine