Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp19 na. 2 uku. 8-9
  • Wakati Bibi ao Bwana Anakosa Uaminifu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wakati Bibi ao Bwana Anakosa Uaminifu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • MAANDIKO YA BIBLIA YENYE INAWEZA KUSAIDIA
  • Kupata Kitulizo Wakati wa Magumu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Biblia Inabadili Maisha
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • 3 Inasaidia Kuvumilia Matatizo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2018
  • Mahangaiko Juu ya Familia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
wp19 na. 2 uku. 8-9
Mwanamuke mumoja iko anasali

Wakati Bibi ao Bwana Anakosa Uaminifu

“Nilitaka kufa wakati bwana yangu alisema kama ananiacha ili kutafuta mwanamuke mwenye ni kijana zaidi. Ilikuwa kama vile nilitendewa bila haki, zaidi sana wakati nilikumbuka mambo yote yenye nilifanya kwa ajili yake.”​—Maria, katika Espagne.

“Wakati bibi yangu aliniacha kwa kushtukia, ilikuwa kama vile sehemu fulani ya mwili wangu iliacha kutumika. Ndoto, matumaini, na mipango yetu viliharibika. Kuko siku zenye niliwaza kama jambo hilo halinisumbue, lakini kisha wakati fulani, nilijisikia tena mwenye kuvunjika moyo sana.”​—Bill, katika Espagne.

KUKOSA uaminifu katika ndoa kunaumiza sana. Ni kweli kwamba, watu fulani wenye wameoa ao kuolewa wameona kuwa wanaweza kusamehe bibi ao bwana yao mwenye ameomba musamaha na hivyo kutengeneza tena uhusiano wenye umeharibika.a Lakini, hata kama ndoa hiyo inaweza kuendelea ao hapana, kwa kawaida wale wenye wanavumbua kama bibi ao bwana yao amekosa uaminifu, wanaumia sana. Namna gani watu hao wanaweza kupambana na maumivu yenye wanapata?

MAANDIKO YA BIBLIA YENYE INAWEZA KUSAIDIA

Hata kama wanaweza kuwa na maumivu ya moyoni, bibi na bwana wengi wenye hawana kosa wamepata kitulizo katika Maandiko. Wamejifunza kuwa Mungu anaona machozi yao na kuwa anaumia pamoja nao.​—Malaki 2:13-16.

“Wakati mahangaiko yalinilemea, ulinifariji na kunituliza.”​—Zaburi 94:19.

Bill anakumbuka hivi: “Wakati nilisoma andiko hilo, nilimuwazia Yehova akituliza maumivu yangu kwa upole, kama vile baba mwenye huruma anaweza kufanya.”

“Kwa mutu mushikamanifu unatenda kwa ushikamanifu.”​—Zaburi 18:25.

Carmen mwenye bwana yake alikosa kuwa muaminifu kwake kwa miezi mingi, anasema hivi: “Bwana yangu hakuwa muaminifu. Lakini ningetumainia kuwa Yehova angekuwa muaminifu kwangu. Hangenivunja moyo hata kidogo.”

“Musihangaike juu ya jambo lolote, lakini katika kila jambo kwa sala na sala ya kumulilia Mungu . . . maombi yenu yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote italinda mioyo yenu.”​—Wafilipi 4:6, 7.

Sasha anasema hivi: “Nilisoma ile andiko tena na tena. Kadiri niliendelea kusali, Mungu alinipatia amani katika maisha yangu.”

Wale wote wenye wamezungumuziwa hapo juu, wakati fulani walijisikia kuwa hawataweza kuvumilia. Lakini walimutumainia Yehova Mungu na wakati walisoma Neno lake, walipata nguvu. Bill yeye, anasema hivi: “Imani yangu ilifanya maisha yangu ikuwe na maana wakati ilionekana kuwa kila kitu kimeharibika. Hata kama kwa muda fulani nilitembea ‘katika bonde lenye kivuli kizito,’ Mungu alikuwa pamoja na mimi.”​—Zaburi 23:4.

a Ili kupata habari yenye kuzungumuzia ikiwa unaweza kusamehe ao hapana, ona habari zenye kupatikana katika Amuka! ya tarehe 22, Mwezi wa 4, 1999 chini ya kichwa “Mwenzi Anapokosa Uaminifu.”

Mambo Yenye Inaweza Kukusaidia Uvumilie

Ufikiri sana kuhusu maandiko yenye inaweza kukupatia kitulizo.

Bill anafasiria hivi: “Nilisoma kitabu cha Yobu na kisha cha Zaburi, na nilitia alama kila andiko lenye niliona kuwa lilizungumuzia hali yangu. Nilitambua kama waandikaji hao wa Biblia walipatwa na aina ya maumivu na mahangaiko yenye nilikuwa ninapata.”

Pata kitulizo kupitia muziki.

Carmen anakumbuka hivi: “Wakati sikuweza kulala usiku, nilisikiliza muziki. Ile ilifanya nitulie kabisa.” Daniel anasema hivi: “Nilijifunza kupiga gitari na niliona kuwa muziki ulinisaidia kupata amani ya moyoni.”

Zungumuza na wengine kuhusu namna unajisikia.

Daniel anasema hivi: “Sikuzoea kuambia wengine namna nilijisikia. Lakini, nilikuwa na marafiki fulani wazuri na niliongea nao kila siku. Nilifanya wajue namna nilijisikia kwa kuwaandikia na kwa kuzungumuza nao. Kufanya vile kulinisaidia sana.” Sasha anasema hivi: “Musaada wa watu wa familia yangu ulikuwa wa lazima sana. Sikuzote mama yangu alikuwa pale kwa ajili yangu. Ikiwa nilipenda kuongea, alikamata wakati wa kunisikiliza. Baba yangu pia alifanya nijisikie salama, na alinisaidia nipone polepole kulingana na hali yangu.”

Endelea kusali.

Carmen anasema hivi: “Nilisali kila wakati. Nilijisikia kuwa Mungu alikuwa karibu yangu, akinisikiliza, na kunisaidia. Wakati wote huo wa magumu nilimukaribia Mungu zaidi.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine