Tuwe Na Mradi Wakati Wa Ziara Zetu Za Kurudia
1 Tunapomrudilia mtu mara ya pili, tujikaze kutumia andiko moja litakalotajirisha maarifa ambayo mtu anayo juu ya habari ya kibiblia ambayo tulizunguzia.
2 Mojawapo ya miradi ya ziara za kurudia wakati tulipoacha magazeti ni kuanzisha njia ya ugawaji. Utoaji mwepesi kama huu ungeweza kuwa wenye matokeo:
◼ “Ninatumaini kwamba ulipenda usomaji wa makala inayofasiria kwa nini tunapaswa kumwogopa Mungu, katika Mnara wa Mlinzi ambao niliacha. Leo ninakuletea makala inayofaa ya Amkeni! inatokeza ulizo hili: ‘Kwa Nini Maisha Ni Mafupi Mno?’ Ni ulizo nzuri, sivyo?” Tuendelee kwa kusema kwa mfano: “Yohana 3:16 linaripoti maneno yenye kujulikana sana ya Yesu kuhusu ahadi ya kuishi milele. Ikiwa unakubali gazeti hili, utatiwa moyo na tumaini imara ambalo Neno la Mungu linatoa.” Tuseme baadaye kwamba tutarudi tena kumletea namba nyingine zinazofuata na kwamba tutazungumza mara nyingine tena yale Mungu ameahidi kwa wanadamu watiifu. Tukumbuke kwamba kila mara tunapomletea mtu magazeti, tunaweza kuhesabu ziara ya kurudia.
3 Ikiwa tuliacha gazeti lenye kichwa cha habari “Ulimwengu Usio na Vita—Lini?” tungeweza kusema:
◼ “Maisha yangefananaje ikiwa hakungekuwa tena vita? [Tuache mtu ajibu.] Angalia yale Mungu anakusudia kufanya.” Tusome Zaburi 37:10, 11, na tueleze hali zitakazokuwa duniani wakati mapenzi ya Mungu yatakapofanyika juu yake. Tumkumbushe msikilizaji mambo kwa ajili yayo Yesu alifundisha wanafunzi wake kusali, kulingana na Mathayo 6:9, 10. Tumfanye afikiri juu ya maana ya maneno ya Yesu. Ikiwa mtu anaonyesha kweli kupendezwa, tunaweza kumtolea uandikisho kwenye Mnara wa Mlinzi au kwenye Amkeni! na kuchukua mipango ili kurudi tena kuzungumza naye.
4 Ikiwa tunarudi tena kuzungumza juu ya makala “Kwa Nini Maisha ni Mafupi Mno?” tunaweza kuanzisha mazungumzo kama ifuatavyo:
◼ “Wakati uliopita, tulizungumza juu ya muda wa maisha ya mwanadamu. Kama ulivyoona bila shaka katika makala ya Amkeni! wanasayansi wana tumaini ndogo sana la kutusaidia kuishi zaidi ya miaka 70 au 80. Lakini unafikiri nini juu ya yale Biblia inaahidi? [Tuache mtu ajibu.] Biblia inaonyesha kwamba Mungu anakusudia kufanya jambo fulani bora kwa ajili wa mwanadamu.” Tusome Yohana 17:3, na tuseme kwamba maarifa yanaweza kuongoza kwenye uhai wa milele. Kufikia hapo, tutolee funzo la Biblia au tusikilizane juu ya siku nyingine ili kuwa na mazungumzo mengine ya Biblia wakati ujao.
5 Kuanzisha funzo la Biblia ni mradi wa lazima wa huduma yetu. Labda tumemtembelea mara nyingi mtu fulani anayekubali magazeti. Kwa nini tusianzishe mazungumzo kama ifuatavyo wakati ujao tutakapokutana na mtu huyo:
◼ “Watu wana kila aina ya mawazo kuhusu dini na manufaa yake katika maisha ya kisasa. Imani mbalimbali kuhusu sababu kwa nini Mungu ameruhusu uovu au sababu ya kuzeeka na kifo yanatofautiana. Wengine wangependa pia kujua yale wanapaswa kufanya ili kwamba Mungu asikilize sala zao.” Tufungue mojawapo ya vichapo vilivyotengenezwa kwa ajili ya funzo la Biblia katika sehemu inayofasiria habari ambayo, kwa maoni yetu, itampendeza mtu, na tuonyeshe kwa ufupi jinsi tunavyoongoza funzo.
6 Yehova anajiwekea miradi. Na tumwige mnamo mwezi wa Oktoba kwa kuwa na mradi wakati wa ziara zetu za kurudia.