Nyakati Zinabadilika
1 Biblia inatuambia kwamba “mandhari [tamasha] ya ulimwengu huu inabadilika.” (1 Kor. 7:31, NW) Ni kweli kama nini leo! Iwe tu muda wa maisha yetu, tumeona mabadiliko kamili katika namna ya kufikiri na katika mwenendo wa watu wa tabaka zote za kijamii. Ikiwa tunataka kwamba ujumbe wa Ufalme uwaguse, tunapaswa kuutoa tukijua pia kwamba nyakati zinabadilika. Tunataka kupeleka habari njema kwa jinsi kupendezwa kwa watu kuamshwe na kwamba moyo wao uguswe.
2 Kumepita hivi miaka fulani, kazi ya ushuhuda ilikuwa tofauti katika nchi nyingi, kwani watu walio wengi walikuwa na maisha tulivu na walikuwa wakijisikia katika usalama. Dini ilikuwa inachukua nafasi ya kwanza katika maisha yao; Biblia ilikuwa yenye kuthaminiwa sana. Mara nyingi, ilituomba kuzungumzia maulizo kuhusu mafundisho katika mahubiri. Leo, maisha ya watu ni wenye msukosuko. Dini inasemwa vibaya. Ni watu wachache walio na imani katika Biblia, na nadharia (mafundisho) ya mageuzi imeharibu imani ya wengi katika Mungu.
3 Mwangalizi mmoja wa mzunguko alisema: “Leo, watu wana mahangaiko mengi na matatizo hivi kwamba, inaonekana, inatupasa kuwafundisha kuongoza maisha yao.” Wasiwasi kubwa ya watu kikawaida inahusu wao wenyewe, familia zao na mahangaiko yao. Inahusu vitu ambavyo wanazungumzia zaidi wanapokuwa pamoja. Tunapaswa kuyafikiria katika kazi yetu ya ushuhuda.
4 Ufalme wa Mungu ni Tumaini Hakika la Pekee kwa Wakati Ujao: Watu walio wengi hawana tumaini katika serikali za kibinadamu. Wanafikiri kwamba hawana tazamio lolote la kuona ulimwengu bora maishani mwao. Dini isiyo ya kweli haikufikia kuwatolea sababu yoyote ya kutumaini. Ni kwa sababu hiyo kile ambacho wanadamu wanahitaji, ni kusikia habari njema ya Ufalme wa Mungu. Tuvutie uangalifu juu ya Ufalme huo na tuonyeshe kwamba utaleta suluhisho kwa matatizo yote ya wanadamu.
5 Biblia ni Chanzo Pekee cha Mashauri Yenye Kutumainika: Leo, raia wanadanganywa na viongozi wanaotegemea hekima ya kibinadamu na falsafa za ulimwengu. Watu wanaweza hivyo kuhakikisha kwamba “kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu.” (Yer. 10:23) Jambo bora ambalo wanaweza kujifunza, ni kwamba wanapaswa ‘kuweka tumaini lao katika Yehova kwa moyo wao wote na kutotegemea akili yao.’ (Mit. 3:5) Nyakati zinabadilika, lakini si Biblia. Kwa hiyo, tunapaswa sikuzote kutanguliza Neno la Mungu katika huduma yetu na kufundisha wengine kukubali thamani ya uongozi wa kimungu ambao linatoa. (2 Tim. 3:16, 17) Kwa hiyo, tunapaswa kuonyesha umuhimu wa Biblia kwa watu kwa kuitaja katika utoaji wetu habari, kwa kuitumia ili kujibu kwa maulizo yao na kwa kukazia ulazima wa kujifunza na kutumikisha hekima inayotenda kazi iliyomo.
6 Ijapokuwa nyakati zinabadilika leo, miradi yetu katika huduma inabaki ileile. Imetupasa kuhubiri habari njema ya Ufalme, kutia nguvu tumaini letu katika Neno la Mungu na kusaidia wengine kuelewa ulazima wa kujifunza Biblia pamoja nasi. Yale tunayosema yanapaswa kuambatana na mahitaji ya sasa ya wale ambao tunatolea ushuhuda. Katika njia hiyo, itawezekana kwetu kuwa wenye kushiriki habari njema pamoja na wengine, na hivyo kupata watu wengi iwezekanavyo.—1 Kor. 9:19, 23.