Tuige Imani Yao
1 Mtume Paulo alionyesha kwamba imani ni “taraja lililohakikishwa la mambo yatumainiwayo, ule wonyesho dhahiri wa mambo halisi ingawa hayatazamwi.” ‘Bila imani haiwezekani kumpendeza Mungu’, aliongeza. (Ebr. 11:1, 6, NW) Paulo anatuhimiza kufurika kwa imani, kwa kujizoeza yenyewe na kuifuatia.—2 Kor. 4:13; Kol. 2:7; 2 Tim. 2:22.
2 Biblia inajaa na vielelezo vyenye kustahajabisha vya imani. Katika Waebrania sura 11, Paulo anapanga orodha ndefu ya mashahidi ambao walionyesha imani kwa kila jaribu. Mnapatikana Abeli, mfia-imani wa kwanza. Noa anatajwa, kwani, kwa imani yake, alionyesha hofu ya Mungu ya muhimu iliyookoa nyumba yake. Abrahamu anasifiwa kwa imani yake na kwa utiifu wake. Musa pia, kwani kwa imani yake alibaki imara kama mtu aliyekuwa akimwona Yule asiyeonekana. Vielelezo hivyo vilikuwa vingi hivi kwamba, anasema Paulo, wakati ungemkosa ikiwa angeendelea kueleza yote yanayowahusu. Sisi ni wenye shukrani kama nini kuweza kutia nguvu imani yetu kwa kufikiria hayo ‘matendo ya mwenendo mtakatifu’ na ‘matendo [hayo] yanayoonyeshwa na ushikamanifu kwa Mungu!’—2 Pt. 3:11.
3 Kwenye karne ya kwanza, Yesu aliuliza ulizo lifuatalo: “Mwana wa watu anapokuja ataona imani katika dunia?” (Lk. 18:8, ZSB) Kwa hiyo, je! kuna kati yetu, leo, vielelezo hai vya imani? Je! tunawaona wanaume na wanawake, vijana na watu wazee-wazee, wakionyesha imani isiyoyumba-yumba katika Yehova, kama ilivyokuwa kwa watumishi wa Mungu wa nyakati za kibiblia?
4 Vielelezo vya Kisasa vya Imani: Vielelezo vyenye kustaajabisha vya imani havikosekani kando-kando yetu! Imani ya waangalizi wanaotuongoza inastahili kuigwa. (Ebr. 13:7) Lakini si peke yao wanaoonyesha imani yenye kielelezo. Kila kutaniko lina washiriki waaminifu wanaodumu katika utumishi wao kwa Yehova tangu siku nyingi, mara nyingi wakiwa wenye kupambana na matatizo ya kila aina.
5 Dada zetu waaminifu ambao, tangu miaka mingi, wanavumilia upinzani wa mume mkali wanastahili kusifiwa. Baba na mama waliweza kushindana peke yao na mwito wa malezi ya watoto. Kati yetu kuna wanawake wajane wazee-wazee wanaoshiriki kwa namna ileile utendaji kadha wote wa kutanilo, na ingawa wengine hawana familia yoyote ili kuwasaidia. (Ona Lk. 2:37.) Imani ya wale wanaovumilia magumu ya afya yanayoendelea inatushangaza bila kukoma. Walio wengi wanaendelea kutumikia kiaminifu ingawa vizuizi vinavyowazuia kupokea mapendeleo ya kitheokrasi ya ziada. Vijana wengine Mashahidi walijizoeza kwa uhodari imani ingawa upinzani shuleni. Ushikamanifu wetu kwa Mungu unaimarika kwa kadiri tunavyowaona mapainia waaminifu wanaodumu mwaka baada ya mwaka, wakishindana na magumu makali. Kama Paulo, wakati ungetukosa ikiwa tungeweza kueleza yale yote ndugu na dada hao waliweza kupatwa nayo katika utumishi wa Ufalme, matendo yote ya imani waliyotimiza!
6 Vielelezo hivyo vya imani vinatuletea faraja na kitia-moyo. (1 Thes. 3:7, 8) Tunayo sababu ya kuiga imani yao, kwa kuwa “wenye kutenda kwa haki ndio furaha ya [Yehova].”—Mez. 12:11.