Mafunzo Ya Biblia Zaidi Yanatakwa
1 Yehova Mungu ni mwenye kubariki tengenezo lake la kidunia kwa ukuzi wenye kuendelea. Mwaka wa utumishi uliopita, watu 375 923 walibatizwa kuzunguka ulimwengu wote—wastani wa zaidi ya wanafunzi wapya 1 000 kila siku, au karibu 43 kila saa! Katika sehemu mbalimbali za dunia, kazi ya Ufalme ni yenye kusitawi na maongezeko yenye kutokeza ni yenye kupatikana, ingawa makumi ya miaka ya magumu ambayo ndugu zetu wanaweza kuwa wamepata. Ni jambo lenye kufurahisha kusoma juu ya maendeleo yanayofanywa katika kueneza habari njema!
2 Mwaka wa utumishi uliopita, tulipata pia ongezeko katika hesabu ya wastani wa mapainia wasaidizi, vitabu, broshua, na magazeti yaliyoangushwa Burundi, Congo-Brazzaville na Congo-Kinshasa. Hudhurio kwenye Ukumbusho lilifikia hesabu kubwa mpya. Namna gani kuhusu mafunzo ya Biblia? Hesabu ya jumla ya mafunzo ya Biblia ilipunguka kwa asilimia 4 Burundi na kwa asilimia 10 Congo-Brazzaville, lakini iliongezeka kwa asilimia 14 Congo-Kinshasa. Mafunzo ya Biblia ndilo jambo la maana katika kazi ya kufanya wanafunzi. Kila mmoja wetu anaweza kufanya nini ili kupindua mwelekeo huo wenye kushuka katika mafunzo ya Biblia?
3 Tutie Nguvu Tamaa ya Kuongoza Funzo: Sisi wenyewe tunahitaji kutia mkazo juu ya kuwa nguvu kiroho na wenye kutenda. Wafuasi wa kweli wa Kristo ni “wenye bidii kwa kazi zilizo bora.” (Tit. 2:14) Wakati tunapochunguza upya huduma yetu, je! tunaweza kusema kwamba sisi ni wenye bidii kufuatilia uangushaji wote wa vichapo uliofanywa katika shamba? Je! sisi ni wenye furaha kuhusu kutolea funzo la Biblia la nyumbani kwa wote wanaoonyesha kupendezwa? (Rom. 12:11) Au je! tunahitaji kukomaza tamaa kubwa zaidi ya kufanya ziara za kurudia na kuanzisha mafunzo ya Biblia ya nyumbani?
4 Usomaji wa Biblia wa kibinafsi, kuhudhuria kikawaida mikutano, na funzo la vichapo vitatulinda tukiwa wenye afya kiroho na wenye kutiwa nguvu na roho ya Mungu. (Efe. 3:16-19) Hilo litatia nguvu imani yetu na tumaini letu katika Yehova na upendo wetu kwa mwanadamu mwenzetu. Tutasukumwa kufundisha ukweli kwa mtu mwingine, na kwa njia hiyo huduma yetu itakuwa yenye kupendeza, yenye mafanikio na yenye kuvutia. Ndiyo, tungetaka mafunzo zaidi ya Biblia!
5 Tujifunze Na Familia Yetu Kwanza: Wazazi Wakristo walio na watoto wanaoishi nyumbani wangepaswa kufikiria programu yao ya funzo la Biblia la familia la kawaida. (Kum. 31:12; Zab. 148:12, 13; Mez. 22:6) Lingekuwa jambo lenye faida sana kwa wazazi kujifunza broshua Anataka na baadaye kitabu Ujuzi pamoja na watoto wao ili kuwatayarisha wajifanye wenye kufaa kuwa wahubiri wasiobatizwa na kwa ajili ya wakfu na ubatizo. Bila shaka habari za ziada zinaweza kuchunguzwa, ikitegemea juu ya uhitaji na umri wa mtoto. Mzazi anayejifunza na mtoto asiyebatizwa anaweza kuhesabu funzo, wakati na ziara za kurudia, kama inavyoonyeshwa katika “Majibu kwa Maulizo Yenu” ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Oktoba 1987.
6 Tufanye Mipango Yetu ya Kibinafsi Iwe Bora: Kwa kuchunguza hesabu ya magazeti, broshua, na vitabu vilivyoangushwa, hakuna shaka kwamba kiasi kikubwa cha mbegu ni chenye kutawanywa. Mbegu hizo za ukweli ambazo zimepandwa zina uwezekano mkubwa wa kutokeza wanafunzi wapya. Lakini je! mlimaji au mpanda-bustani anaweza kwa kweli kutosheka ikiwa ameendelea kupanda, na baada ya jitihada zake zote, hakuchukua kamwe wakati wa kuvuna? Bila shaka hapana. Vivyo hivyo, huduma yenye kufuatiliwa ni ya lazima.
7 Je! unapanga kikawaida wakati wa kufanya ziara za kurudia? Rudilia bila kukawia kupendezwa kote kulikopatikana. Fanya ziara za kurudia ukiwa na kusudi la kuanzisha funzo la Biblia. Je! unafanya maandishi yenye kuwa wazi, ya kisasa, na yenye kupangwa vizuri ya ziara zako za kurudia? Pamoja na jina na anwani ya msikilizaji, uwe hakika kwamba umeandika tarehe ya ziara ya kwanza, maangusho yoyote, maelezo mafupi juu ya yale yaliyozungumziwa, na jambo linaloweza kuzungumziwa wakati wa ziara ifuatayo. Acha nafasi juu ya maandishi yako kwa ajili ya habari za ziada zitakazoongezwa baada ya kila ziara ya kurudia.
8 Tufikirie Namna ya Kufanya Ziara ya Kurudia: Ni nini mambo fulani ya kulinda akilini wakati tunapofanya ziara ya kurudia kwa mtu aliyependezwa? (1) Tuwe wenye shauku, wenye urafiki, wachangamfu, na wa vivi hivi. (2) Tuzungumzie habari au maswali yanayompendeza. (3) Tufanye mazungumzo yawe rahisi, yenye kupendeza, na ya kimaandiko. (4) Wakati wa kila ziara, tujitahidi kufundisha msikilizaji wetu jambo fulani atakalolitambua kuwa la thamani kwake kibinafsi. (5) Tujenge uthamini wa mapema kwa ajili ya habari itakayozungumziwa wakati wa ziara ijayo. (6) Tusikae kwa muda mrefu. (7) Tusiulize maswali yenye kutatiza msikilizaji wetu au kumweka katika hali yenye kujaribu. (8) Tutumie ufahamu ili kwamba tusihukumu maoni mabaya au tabia mbaya za msikilizaji wetu kabla ya kusitawisha uthamini wa kiroho.—Kwa ajili ya msaada wa ziada juu ya namna ya kuwa wenye matokeo katika kufanya ziara za kurudia na kuanzisha mafunzo ya Biblia, ona nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Aprili 1997.
9 Tujaribu Kila Uwezekano: Katika kutaniko moja, lilikuwa jambo lenye kuwezekana kupata majina na namba ya nyumba za wakaaji wote katika jengo lenye kulindwa sana. Barua iliandikwa kwa kila mkaaji kibinafsi, na trakti mbili zilitiwa ndani ya bahasha. Mwishoni mwa barua, funzo la Biblia la nyumbani lilitolewa na namba ya simu ya mahali ilitiwa ndani hivi kwamba mpokeaji angeweza kujibu. Katika siku chache, mwanamume kijana aliita akiomba funzo. Ziara ya kurudia ilifanywa siku iliyofuata, na funzo likaanzishwa katika kitabu Ujuzi. Usiku uleule alihudhuria kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko, na akaendelea kuhudhuria mikutano yote. Karibu wakati uohuo, akaanza usomaji wa kikawaida wa kila siku wa Biblia. Alifanya maendeleo thabiti kuelekea ubatizo.
10 Wahubiri katika gari moja la kikundi walipanga kufanya pamoja ziara fulani za kurudia. Wakati dada mmoja alipofanya moja ya ziara zake, mtu aliyekuwa akimtafuta hakuwako nyumbani, lakini mwanamke mwingine kijana alijibu kwenye mlango, akisema: “Nimekuwa nikiwangoja.” Mwenye nyumba alikuwa amepokea mapema kitabu Ujuzi kutoka kwa mtu aliyejuana naye. Wakati dada walipogonga kwenye mlango wake, mwanamke huyo alikuwa amesoma kitabu chote mara mbili na alikuwa ameguswa na habari iliyokuwa ndani. Alisema kwamba hakushangaa kuona Mashahidi wakimtembelea siku hiyo kwa kuwa alikuwa amekuwa akisali ili kwamba waje na kujifunza Biblia pamoja naye. Funzo lilianzishwa, akaanza kuhudhuria mikutano ya kutaniko, na akafanya maendeleo ya haraka.
11 Dada mmoja ambaye ni mwenye kubatizwa kwa karibu miaka 25 alimtolea mama yake kitabu Ujuzi siku chache zilizopita. Mama yake, ambaye ni mshiriki wa kanisa, alianza kukisoma kitabu hicho. Baada ya kumaliza sura mbili, akaita binti yake, na kwa mshangao wa binti yake, akasema: “Ninataka kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova.” Mama huyo akaanza kujifunza na sasa ni mwenye kubatizwa.
12 Jaribu Madokezo Yafuatayo: Je! umekwisha kutumia utoaji wa moja kwa moja kwa kuanzisha mafunzo? Unaweza tu kusema: “Ikiwa ungetaka kuwa na funzo la Biblia la nyumabani bila malipo, ninaweza kukuonyesha kwa dakika chache tu namna linavyofanywa. Ikiwa unalifurahia, unaweza kuendelea.” Wanapotiwa katika hali hiyo, watu wengi hawasiti kukubali toleo na kuangalia namna funzo la Biblia linavyoendeshwa.
13 Mwanzoni mwa funzo, onyesha mwanafunzi namna ya kujitayarisha mapema kwa kusoma maandiko yaliyotajwa na kutia kistari kwenye maneno makuu katika kujibu kwa maulizo yaliyochapwa. Tia mkazo tu kwa mambo makuu. Ingawa tunaweza kuhitaji kutokuwa washupavu katika vipindi vichache vya kwanza, ni jambo la lazima kwamba funzo la Biblia lifanywe kwa msingi wa kikawaida. Weka katika akili namna utakavyofanya utangulizi wa sala kuwa sehemu ya maana ya funzo na namna utakavyotayarisha mwanafunzi kimaandiko kwa ajili ya upinzani. Kwa vyovyote, fanya funzo lipendeze.
14 Kwa kweli, si wanafunzi wote wa Biblia wanaofanya maendeleo kwa mwendo uleule. Wamoja hawapendezwi kiroho kama vile wengine wala kuwa haraka kuelewa mambo wanayofunzwa. Wengine wanaishi maisha yenye shughuli sana na hawawezi kutoa wakati unaohitajika ili kumaliza sura moja kila juma. Hivyo, katika hali fulani linaweza kuwa jambo la lazima kuchukua zaidi ya kipindi kimoja cha funzo ili kumaliza sura fulani fulani na miezi ya ziada ili kumaliza kitabu. Katika hali fulani tunaweza kujifunza broshua Anataka kwanza na kisha kuendelea na kitabu Ujuzi; katika zingine, baada ya kumaliza kitabu Ujuzi, tunaweza kuona kuwa jambo lifaalo kujifunza broshua Anataka. Hilo, likiongezewa kuhudhuria kwao kwenye mikutano ya kutaniko, litasaidia kila mwanafunzi kupata msingi thabiti katika ukweli.
15 Zaidi ya yote, sali kwa ajili ya funzo la Biblia! (1 Yn. 3:22) Moja ya mambo yaliyoonwa yenye kuthawabisha kwa Mkristo ni kutumiwa na Yehova ili kusaidia mtu fulani kuwa mwanafunzi wa Yesu Kristo. (Mdo. 20:35; 1 Kor. 3:6-9; 1 Thes. 2:8) Huu ndiyo wakati wa kuonyesha bidii kubwa katika kazi ya mafunzo ya Biblia, tukitumainia kikamili baraka nyingi za Yehova juu ya jitihada zetu za kuanza mafunzo zaidi!
[Caption on page 5]
Je! wewe unasali ili uanzishe funzo jipya la Biblia?