Tutoe Ushahidi Kupitia Mwenendo Mzuri
1 Katika ulimwengu wa sasa wenye kuachilia mambo, vijana wengi wasio waangalifu huharibu maisha yao kwa dawa za kulevya, ukosefu wa adili, uasi na jeuri. Hata hivyo, mwenendo wa kuigwa wa vijana wenye kujaa nguvu katika kutaniko la Kikristo unafurahisha kuona na bila shaka huo ni urembo machoni pa Yehova. Unatoa ushahidi wenye nguvu unaoweza kuvuta watu fulani kuelekea kweli.—1 Pet. 2:12.
2 Mambo mengi yaliyoonwa yanaonyesha kwamba mwenendo bora wa vijana Wakristo ulikuwa na uvutano mzuri juu ya watazamaji. Akisimulia juu ya mmoja wa wanafunzi wake aliyekuwa Shahidi wa Yehova, mwalimu mmoja wa kike alisema mbele ya somo lake lote kwamba Yehova, Mungu wa msichana huyo kijana, ndiye Mungu wa kweli. Na hilo kwa sababu msichana kijana huyo alikuwa sikuzote na mwenendo wenye adabu. Mwalimu mwingine aliandikia Sosaiti maneno yafuatayo: repris de w87-SW 1/1 p.5 par. 4.“Mimi ningependa kuwasifu ninyi kwa sababu ya vijana wazuri sana mlio nao katika dini yenu. . . . Vijana wenu ni mfano kweli kweli. Wao wanaheshimu wazee wao, ni waungwana na wanavaa kwa kiasi. Nao wanazijua Biblia zao wee! Hiyo ni dini kweli kweli!”
3 Mwalimu mmoja wa shule ya msingi aliguswa moyoni na mwenendo mzuri wa mwanafunzi mmoja wa somo lake, mwana wa Mashahidi mwenye umri wa miaka saba. Alivutwa na utu mpole na wenye kupendeza wa mtoto, uliokuwa tofauti sana na ule wa wavulana wengine. Alishangazwa na jambo la kwamba alichukua kwa uzito itikadi zake za kidini, akitambua kwamba kijana huyo hakuona haya ya kuwa tofauti kwa sababu ya imani zake. Alipata kuona kwamba alikuwa na dhamiri iliyozoezwa na kwamba alikuwa na uwezo wa “kutofautisha lililo sahihi na lililo kosa pia.” (Ebr. 5:14) Hatimaye, mama ya mvulana huyo alimtembelea mwalimu huyo, na funzo la Biblia likaanzishwa. Baadaye, mwalimu huyo alibatizwa na akawa mwishowe painia wa kawaida!
4 Mwanamume kijana mmoja alivutwa na mwenendo mzuri wa dada Mkristo Shahidi wa Yehova wa shule yake. Alikuwa tofauti sana: mwenye adabu, mwenye bidii ya kujifunza, na aliyevaa kwa adabu sikuzote; zaidi ya hayo, tofauti na binti wengine, hakuchezacheza kamwe na wavulana. Kijana mwanamume huyo aliona kwamba dada alifuata kanuni za kibiblia katika maisha yake. Akamuuliza maswali juu ya imani zake, na yale aliyosikia yalimgusa moyo. Akaanza kujifunza, hakukawia kubatizwa, na baadaye akawa painia, kisha mwanamemba wa Betheli.
5 Ikiwa wewe ni Mkristo kijana unayetaka kutoa ushahidi mzuri kwa wengine, uwe mwangalifu kwa mwenendo wako katika kila njia. Usijitie kamwe katika hali ya kupatwa na madhara kwa kuwa na msimamo mzuri kuelekea uachiliaji-mambo wa ulimwengu, iwe katika mielekeo yake, maoni yake au namna zake za kuishi. Uwe kielelezo cha hali ya juu katika maneno yako, mavazi yako, kujipamba kwako, si wakati unaposhiriki kwenye mahubiri na kuhudhuria mikutano tu, bali pia wakati unapoenda shuleni au wakati wa tafrija. (1 Tim. 4:12) Ni furaha kwako kama nini wakati mtu fulani anapopendezwa na kweli kwa sababu umeacha ‘nuru yako ing’ae’ kupitia mwenendo wako mzuri!—Mt. 5:16.