Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/06 uku. 8
  • Vijana Wanaoangaza Kama Mianga

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vijana Wanaoangaza Kama Mianga
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Tung’ae Tukiwa Wamulikaji’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • “Acheni nuru yenu ing’ae”
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Tutoe Ushahidi Kupitia Mwenendo Mzuri
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • ‘Muache Nuru Yenu Iangaze’ ili Kumutukuza Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2006
km 1/06 uku. 8

Vijana Wanaoangaza Kama Mianga

1 Yesu aliwaambia wafuasi wake: “Ninyi ndio nuru ya ulimwengu.” (Mt. 5:14, 16) Wangepaswa kuonekana wazi, kama jiji lililowekwa juu ya mlima linaloangazwa na nuru ya jua. Leo, vijana wengi Wakristo ni “wenye kuangaza kama mianga katika ulimwengu” kupitia mwenendo wao mzuri na bidii yao ya kutoa ushahidi.—Flp. 2:15; Mal. 3:18.

2 Kwenye Shule: Unawezaje kutoa ushahidi kwenye shule? Wakati wanapojifunza somo kuhusu dawa za kulevya, mageuzi, maangamizi makubwa ya wanazi, na kadhalika, vijana fulani wametumia nafasi hiyo ili kutoa ushahidi. Dada mmoja aliyeombwa kuandika maelezo kuhusu ugaidi (terrorisme) alitumia nafasi hiyo ili kutoa ushahidi kuhusu Ufalme wa Mungu kuwa tumaini hakika kwa ajili ya wanadamu. Mwalimu alivutiwa na namna alivyoandika mawazo vizuri, na hilo likafungua njia ya kutoa ushahidi zaidi.

3 Njia nyingine ya kuangaza kama mwanga ni kupitia mwenendo wako, mvalio wako na mapambo yako yenye kiasi. (1 Kor. 4:9; 1 Tim. 2:9) Wanafunzi na walimu wanapoona kwamba mwenendo wako ni tofauti, wengine wanaweza kuvutiwa kwenye ukweli, hilo likiwa matokeo ya mwenendo wako bora na kukutolea hivyo nafasi ya kueleza kweli za Biblia. (1 Pet. 2:12; 3:1, 2) Huenda isiwe rahisi kudumisha mwenendo unaoonyesha kwamba unamwogopa Mungu, lakini Yehova atakubariki sana. (1 Pet. 3:16, 17; 4:14) Ili kuchochea wengine wapendezwe na habari njema, unaweza kusoma vichapo vya Biblia mnamo vipindi vya mapumziko au kuviweka mahali ambapo wengine wanaweza kuviona.

4 Ukiacha nuru yako iangaze kwenye shule, hilo litaimarisha imani yako na kukusaidia kujenga sifa nzuri itakayokufanya ujisikie vizuri katika kumtumikia Yehova. (Yer. 9:24) Jambo hilo litakuwa pia ulinzi kwako. Dada mmoja alisema, “Faida moja ya kuzungumza kuhusu imani yangu ni kwamba wanafunzi wenzangu hawajaribu kunishawishi kufanya mambo yanayopingana na Biblia.”

5 Kupanua Utumishi: Njia nyingine ambayo katika hiyo vijana wengi wanaangaza kama mianga ni kwa kupanua huduma yao. Baada ya kumaliza masomo ya juu, ndugu mmoja alihama ili kutumikia mahali palipokuwa na uhitaji mkubwa wa wahubiri wa Ufalme. Alikuwa katika kutaniko ndogo lililokuwa na mzee mmoja tu. Aliandikia rafiki yake mmoja: “Ninafurahia kabisa maisha huku.” Aliongeza: “Utumishi unaburudisha sana! Sisi huzungumza kwa dakika 20 hivi na wenye nyumba kwani wao hutaka kusikia ujumbe wetu. Laiti vijana wote wangefanya jambo hilo na kupata uradhi. Hakuna jambo bora kuliko kumtumikia Yehova kwa nafsi yote.”

6 Tunajivunia sana ninyi vijana wenye kuangaza kama mianga katika ulimwengu! (1 The. 2:20) Mnapomtumikia Yehova kwa moyo wenu wote, kwa nafsi yenu yote, kwa akili yenu yote na kwa nguvu zenu zote, mtavuna “mara mia sasa katika kipindi hiki cha wakati . . . na katika mfumo wa mambo unaokuja uzima wa milele.”—Marko 10:29, 30; 12:30.

[Maulizo ya Funzo]

1. Biblia inaonyeshaje kwamba Wakristo wangepaswa kuonekana wazi, na maneno haya yanawahusuje vijana Wakristo leo?

2. Ni njia fulani gani unazoweza kutumia ili kutoa ushahidi kwa walimu na wanashule wenzako?

3. Unawezaje kuacha nuru yako iangaze shuleni kupitia nwenendo wako?

4. Ni faida fulani gani zinazotokana na kutoa ushahidi kwenye shule?

5. (a) Vijana wengine wanapanuaje huduma yao? (b) Miradi yako ya kiroho ni gani?

6. Ni jambo gani linalokufanya ujisikie vizuri kuhusu vijana katika kutaniko lenu?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine