Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/99 uku. 1
  • “Dhihirisheni Subira”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Dhihirisheni Subira”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Katika Kazi Yetu ya Kuhubiri—Tunapaswa Kuonyesha Uvumilivu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Muendelee Kuwa na Uvumilivu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Uvumilivu wa Yehova na Yesu Unatufundisha Nini?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Uvumilivu​—Onyesha Sifa Hii na Uko na Tumaini
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 1/99 uku. 1

“Dhihirisheni Subira”

1 Kadiri tunavyoona mwisho wa mfumo wa mambo mkongwe (uliozeeka sana) wa Shetani ukikaribia zaidi na zaidi, ni jambo la lazima ‘tudhihirishe subira’ huku tukingoja siku ya Yehova ya wokovu. Zaidi sana wakati huu wa karibu na mwisho, jeshi baya la adui lina nia thabiti ya kugeuza uangalifu wetu kutoka lile swali kubwa la enzi kuu ya Yehova na linatujaribu ili likengeushe fikira zetu zielekee mapendezi mengi ya binafsi. Katika njia hiyo, Shetani angetudanganya tuache au tulegeze kazi ya kuhubiri Ufalme. (Yak. 5:​7, 8; Mt. 24:13, 14) Ni katika njia gani tunaweza kuonyesha subira kama hiyo yenye kuhitajiwa?

2 Kwa Kuwa Wenye Kujidhibiti [W 1forbear vi 2]: Tunapokutana na ubaridi au upinzani katika huduma yetu, kujidhibiti kutatusaidia tudumu katika kuhubiri. Hatutaogopeshwa kwa vyepesi au kuumizwa ikiwa watu tunaokutana nao ni wenye hamaki (hasira ya ghafla) na wasio na fadhili. (1 Pet. 2:​23) Nguvu hiyo ya ndani inaweza kutuzuia kusema vibaya juu ya watu katika eneo letu ambao wanaonyesha ubaridi au chuki kali kuelekea kazi yetu, tukijua kwamba maneno kama hayo yanaweza kutuvunja moyo sisi na wale wanaotumika nasi katika huduma.

3 Kwa Ujitahidi Wenye Subira: Inaweza kuomba tuwe na subira wakati hatuwezi kumkuta tena nyumbani mtu anayependezwa tuliyezungumza naye katika utumishi wa shambani. Vivyo hivyo ikiwa wale tunaojifunza nao hawafanyi maendeleo haraka wala kuchukua msimamo kwa ajili ya kweli. Hata hivyo, ujitahidi wenye subira huthawabishwa mara nyingi kwa matokeo mazuri. (Gal. 6:9) Dada mmoja alifanya ziara nyingi za kurudia nyumbani kwa mwanamke kijana kabla ya funzo la Biblia kuanzishwa kwelikweli. Wakati wa ziara tano za kwanza, mwanamke huyo alikuwa na shughuli nyinginezo. Kwenye jaribio la sita, dada huyo aliloweshwa na mvua ya radi, na kisha hakumkuta mtu nyumbani. Hata hivyo, akiwa mwenye nia thabiti ya kumtolea mwanamke huyo nafasi nyingine, dada alimtembelea tena na akamkuta akiwa tayari kujifunza. Baada ya hapo, mwanafunzi huyo alifanya maendeleo thabiti na katika wakati mfupi akayaweka maisha yake wakfu kwa Yehova.[1]

4 Tunajua kwamba siku ya Yehova haitachelewa. Hivyo, tunangoja atimize mambo, tukijua kwamba subira ya Mungu itazaa matunda mazuri. (Hab. 2:3; 2 Pet. 3:​9-​15) Tunapaswa kudhihirisha subira kama anavyofanya Yehova na tusiache huduma yetu. Kwa imani na subira, mtazamie Yehova akuthawabishe kwa kazi yako ngumu.​—Ebr. 6:​10-​12.

[DO NOT SET] References

1. w72 11/15 701-2.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine