Katika Kazi Yetu ya Kuhubiri—Tunapaswa Kuonyesha Uvumilivu
1. Namna gani Yehova ameonyesha uvumilivu kuelekea wanadamu?
1 Mungu ni mvumilivu sana kuelekea wanadamu. (Kut. 34:6; Zab. 106:41-45; 2 Pet. 3:9) Kazi ya kuhubiri Ufalme ulimwenguni pote ni mfano mmoja mzuri sana unaoonyesha jinsi Mungu anavyowavumilia wanadamu kwa upendo. Yehova amejikaza sana kuwasaidia wanadamu kwa miaka karibu 2,000, na bado anaendelea kuwavuta kwake watu wenye mioyo ya haki wanaotaka kufanya urafiki pamoja naye. (Yoh. 6:44) Namna gani tunaweza kuiga uvumilivu wa Yehova katika kazi yetu ya kuhubiri?
2. Namna gani tunaweza kuonyesha uvumilivu tunapohubiri katika eneo letu?
2 Tunapohubiri Nyumba kwa Nyumba: Tunaiga uvumilivu wa Yehova kwa kuhubiri “bila kuacha” katika eneo ambalo watu hawaonyeshi kupendezwa na ujumbe wetu. (Mdo. 5:42) Tunaonyesha uvumilivu tunapokutana na watu wanaokataa ujumbe wetu, wanaotucheka, ao kutupinga. (Marko 13:12, 13) Pia, tunaonyesha uvumilivu tunapoendelea kujikaza kumwangia mbegu za ukweli maji hata wakati ambapo ni vigumu kupata watu wenye kupendezwa na ujumbe wetu nyumbani.
3. Kwa nini uvumilivu unahitajiwa tunaporudilia watu na tunapoongoza mafunzo ya Biblia?
3 Tunapoongoza Mafunzo ya Biblia: Ili kukomalisha mumea, inaomba uvumilivu. Tunaweza kuutunza mumea, lakini hatuwezi kuufanya ukomae haraka. (Yak. 5:7) Vivyo hivyo, ukuzi ao ukomavu wa kiroho unafanyika polepole na hatua kwa hatua. (Marko 4:28) Watu tunaojifunza nao wanaweza kuona kwamba ni vigumu kuachana na mafundisho ya uongo ya dini zao ao desturi zisizopatana na maandiko. Hatupaswi kuwakaza wafanye mabadiliko kwa sababu tu tunapenda wakomae kiroho. Tunapswa kuwa na uvumilivu ili kuachia roho ya Mungu wakati wa kutosha ili ifanye kazi ndani ya moyo wa mwanafunzi.—1 Kor. 3:6, 7.
4. Namna gani kuonyesha uvumilivu kunaweza kutusaidia kupata matokeo mazuri tunapowahubiria watu wa jamaa wasio Mashahidi?
4 Tunaposaidia Watu wa Jamaa Wasio Mashahidi: Ijapokuwa tunatamani sana kuona watu wa jamaa yetu wasio Mashahidi wajifunze kweli, tunapaswa pia kuonyesha uvumilivu; tutangojea wakati unaofaa ili kuzungumza nao kuhusu mambo tunayoamini, tunapaswa kuwa waangalifu ili tusiwavuruge na mambo mengi kwa wakati mmoja. (Mhu. 3:1, 7) Wakati huo wa kubaki kimya, tutawafundisha kupitia mwenendo wetu mzuri, na nafasi ikijitokeza tutakuwa tayari kuzungumza nao kuhusu mambo tunayoamini kwa tabia-pole na heshima kubwa. (1 Pet. 3:1, 15) Kwa kweli, tukionyesha uvumilivu katika kazi yetu ya kuhubiri, tutapata matokeo mazuri zaidi na tutampendeza Baba yetu wa mbinguni.