Jinsi Washiriki wa Familia Wanavyofanya Kazi Pamoja ili Kushiriki Kikamili—Katika Mikutano ya Kutaniko
1 Familia za Kikristo zapaswa kutii amri ya kukusanyika pamoja kwenye mikutano ya kutaniko. (Ebr. 10:24, 25) Kwa kushirikiana vizuri, wote wanaweza kufanikiwa katika kutayarisha, kuhudhuria na kushiriki mikutano. Hali za familia hutofautiana, lakini kuna mambo ambayo mume Mkristo, mke mwenye kuamini au mzazi anayelea watoto pekee yake waweza kufanya ili kuendeleza umoja wa familia katika mambo ya kiroho, bila kujali hesabu na umri wa watoto walio katika nyumba.—Mez. 1:8.
2 Chukueni Wakati wa Kutayarisha: Washiriki wa familia hufanya kazi pamoja ili kuona ikiwa kila mmoja ametayarishwa ifaavyo kwa ajili ya mikutano ya kutaniko. Wengi huchunguza pamoja makala ya Funzo la Mnara wa Mlinzi la kila juma. Wengine hujitayarisha kwa ajili ya Funzo la Kitabu au husoma pamoja usomaji wa Biblia wa juma. Mradi ni kuwa na mawazo makuu akilini kabla ya kuhudhuria mikutano. Katika njia hiyo, wote watafaidika zaidi kutokana na yale yanayosikiwa na watakuwa wenye kuandaliwa vifaa ili kushiriki wakati nafasi itakapopatikana.—1 Tim. 4:15.
3 Azimieni Kushiriki: Kila mmoja katika familia angepaswa kuwa na mradi wa kutangaza tumaini lake mbele ya wengine kwa kutoa maelezo kwenye mikutano. (Ebr. 10:23) Je! mshiriki mmoja wa familia anahitaji msaada au kitia-moyo ili afanye hivyo? Ni msaada gani ambao kila mmoja anahitaji katika kutayarisha vipindi vya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi? Wake hufurahi wakati waume wao hufanya hatua ya kwanza na kuwapa labda wazo kuhusu mfano wenye kupatana na habari au kikao chenye kufaa. Wazazi hawapaswi kuwaza kwamba wanapaswa kutayarisha vipindi kwa ajili ya watoto wao wadogo. Kufanya hivyo kungeweza kusonga uwezo wa mtoto wa kuanzisha mambo. Lakini wazazi wanaweza kusaidia watoto wao na kuwasikiliza wanapojizoeza kwa sauti kubwa.—Efe. 6:4.
4 Tengenezeni Mambo ili Mhudhurie: Tangu umri mdogo, watoto wanaweza kufundishwa kuvaa na kuwa tayari kwenda kwenye mikutano pa wakati uliochaguliwa. Washiriki wa familia wangepaswa kushirikiana katika kufanya kazi za nyumbani ili ukawio usiwepo.—Ona madokezo katika vitabu Furaha ya Familia, ukurasa 112, na Vijana Huuliza, kurasa 316-17.
5 Wazazi na watoto wanaweza kufikiri kwa makini juu ya maneno ya Yoshua wa kale, aliyesema: “Mimi na nyumba yangu, tutatumikia BWANA.” Kwa hiyo, azimieni kufanya kazi pamoja ili kushiriki kikamili katika mikutano ya kutaniko.—Yos. 24:15.