Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/99 uku. 4
  • Watumishi wa Huduma Hutoa Utumishi Wenye Thamani

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Watumishi wa Huduma Hutoa Utumishi Wenye Thamani
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Watumishi wa Huduma Wanafanya Kazi ya Maana
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Watumishi wa Huduma Wanafanyaka Kazi Gani?
    Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Onyesha Shukrani Juu ya “Zawadi Katika Wanadamu”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Ndugu​—⁠Muko Najikaza juu Mufikie Kuwa Watumishi wa Huduma?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 3/99 uku. 4

Watumishi wa Huduma Hutoa Utumishi Wenye Thamani

1 “Wamejionyesha kuwa wanaume walio wakf kweli kweli ambao imani yao imeonyeshwa kwa utumishi wenye bidii wa Ufalme na katika kusaidia wengine wawe imara katika imani.” Hivyo ndivyo kinavyosema kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu, kwenye ukurasa 57, kuhusu watumishi wa huduma. Ndiyo, kielelezo cha kiroho ambacho watumishi wa huduma wetu hutoa chastahili kuigwa. Kufanya kazi pamoja nao na pamoja na wazee “hutokeza ukuzi wa mwili ili kujijenga huo wenyewe katika upendo.”​—Efe. 4:​16.

2 Watumishi wa huduma hutimiza kazi ya maana sana katika kutaniko. Fikiria utumishi wao bora wote: kushughulika na akaunti, vichapo, magazeti, maandikisho na maeneo; kutumika kama wakaribishaji; kushughulika na vikuza-sauti; na kutunza Jumba la Ufalme. Wao hushiriki Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi. Baadhi yao waweza hata kutoa hotuba za watu wote na kuongoza baadhi ya mikutano ya kutaniko. Kama viungo vya mwili, watumishi wa huduma hutimiza utumishi mbalimbali tunaouhitaji.​—1 Kor. 12:12-​26.

3 Kuona watumishi wa huduma wakishirikiana na wazee kwa umoja kama sehemu ya baraza moja la wahudumu, kwa heshima na uelewano, hutia moyo wengine wafanye viyvo hivyo. (Efe. 4:​16) Kwa kutimiza madaraka yao kwa uaminifu kila juma [Meaning: regularly]na kwa kuonyesha kupendezwa binafsi na wengine, wao huchangia katika kufanya kutaniko lenye maendeleo kiroho.

4 Tunaweza kufanya nini ili kuonyesha uthamini wetu kuelekea watumishi wa huduma wanaofanya kazi ngumu? Tunahitaji kujua kazi walizogawiwa na kuonyesha utayari wa kushirikiana nao wakati msaada wetu unapohitajiwa. Kwa neno na kwa tendo, tunaweza kuwajulisha kwamba kazi yao ni yenye kuthaminiwa. (Mez. 15:23) Wale wanaofanya kazi ngumu kwa ajili yetu wastahili shukrani yenye kutoka moyoni.​—1 Thess. 5:​12, 13.

5 Neno la Mungu laonyesha daraka na sifa zenye kustahilisha za watumishi wa huduma. (1 Tim. 3:​8-​10, 12, 13) Utumishi wao mtakatifu wenye thamani ni wa lazima katika utendaji wa kutaniko. Wanaume kama hao wastahili kitia-moyo chetu chenye kuendelea, kadiri wote walivyo na “mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.”​—1 Kor. 15:58.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine