Mambo ya Kutosahau kwa Ajili ya Ukumbusho
Mwaka huu, mwadhimisho wa Ukumbusho utafanyika Siku ya Nne, Aprili 1. Wazee wangepaswa kutoa uangalifu kwa mambo yafuatayo:
◼ Katika kupanga wakati kwa ajili ya mkutano huo, hakikisheni kwamba mifano haitapitishwa kabla ya jua kutua.
◼ Kila mmoja, kutia ndani msemaji, angepasa kujulishwa wakati kamili na mahali pa mwadhimisho huo.
◼ Aina yenye kufaa ya mkate na divai lazima vipatikane na kufanywa viwe tayari.—Ona Mnara wa Mlinzi wa Machi 1, 1985, ukurasa 17. Ref: well verified
◼ Sahani, bilauri, na meza yenye kufaa na nguo ya mezani lazima viletwe kwenye jumba na kupangwa mbele ya wakati.
◼ Jumba la Ufalme au mahali pengine pa mkusanyiko huo lazima pasafishwe kikamili kabla ya wakati.
◼ Wakaribishaji na wahudumu wangepasa kuchaguliwa na kupewa maagizo mbele ya wakati kuhusu kazi yao na utaratibu wenye kufaa.
◼ Mipango lazima ifanywe ili kuhudumia mpakwa-mafuta yeyote asiyejiweza au asiyeweza kuwako.
◼ Ikiwa makutaniko mengi yamepanga kutumia Jumba la Ufalme lilelile, lazima kuwe upatanisho mwema kati ya makutaniko ili kuepuka songamano lisilohitajika katika sebule au mwingilio, kwenye njia za waenda kwa mguu, na mahali pa kuegeshea magari.