Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 5/99 uku. 8
  • Njia za Kupanua Huduma Yako

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Njia za Kupanua Huduma Yako
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna ya Kupanua Utumishi Wako
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Je, Unataka Kufanya Mengi Zaidi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Wahubiri wa Ufalme Wanapewa Mazoezi
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Unatimiza kwa Ukamili Utumishi Wako?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 5/99 uku. 8

Njia za Kupanua Huduma Yako

1 Zaidi ya miaka 40 iliyopita, makala yenye kichwa “Je! Wewe Wafanya Yote Uwezayo?” ilitokea katika Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 1955. Ilionyesha kwa upendo jinsi inavyowezekana kwa watu wa Yehova kufanya jitihada ya kila mmoja katika huduma iwe bora ili wazidishe utendaji wa Ufalme. Shauri hilo zuri latumika leo pia, kadiri tunavyoendelea kufanya zaidi na zaidi yote tuwezayo [Meaning: to make improvement].

2 Utumishi wetu wote ungepaswa kuchochewa na ile amri kubwa kuliko zote: “Lazima umpende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote na kwa nguvu zako zote.” (Mk. 12:30) Tunaonyesha upendo wetu kamili kwa Yehova kwa kutumia kikamili nafasi zinazopatikana kwetu ili kuendeleza kazi yake ya Ufalme. Fikiria njia zifuatazo ambazo kwa hizo unaweza kupanua huduma yako.

3 Chukua Dadaraka Lako: Akina ndugu walio wakfu waweza kujitahidi kujifanya wawe wenye kustahili kuwa watumishi wa huduma na baadaye kuendelea ili kutumikia wakiwa wazee. Makala “Je! Wewe Wajitahidi Kufikia?” na “Je! Wewe Wastahili Kutumikia?,” katika toleo la Mnara wa Mlinzi wa Septemba 1, 1990, yalichochea akina ndugu wengi wajifanye kuwa tayari kwa ajili ya madaraka katika kutaniko. Uliza wazee wa kwenu madokezo ya pekee kuhusu jinsi unavyoweza kufikia na kujifanya kuwa mwenye kustahili.

4 Wazee na watumishi wa huduma walio waseja waalikwa wafikirie kwa makini kujaza ombi kwa ajili ya Shule ya Mazoezi ya Kihuduma. Unaweza kupata habari kuhusu shule hiyo kwa kusoma mitajo chini ya “École de formation ministérielle” katika Index des publications de la Société Watchtower 1986-​1995, 1996, na 1997. Je! wewe waona huo ‘mlango mkubwa uongozao kwenye utendaji’ ukijifungua mbele yako? (1 Kor. 16:9a) Ndugu wengi waliopita kwenye mlango huo hawakufikiria kamwe mapendeleo yote ya utumishi yaliyowezekana baada ya kumaliza shule hiyo, lakini sasa wao ni wenye kushughulikia mgawo wao wakiwa mapainia mahali ambapo uhitaji ni mwingi au wakiwa mapainia wa pekee, au wakitumika kwenye Betheli, au wakiwa waangalizi wasafiri​—katika nchi hii au kwingineko.

5 Fikia Utumishi wa Wakati Wote: Vijana wanaopata diploma, wake wa nyumbani, na mtu mwingine yeyote aliyefikia umri wa kustaafu (kuacha) kazi ya kimwili wangeweza kufikiria kwa makini kupainia. Rudilia nyongeza katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Agosti 1998, kisha uzungumze na mapainia ambao hali zao zilifanana na zile za maisha yako mwenyewe. Yaweza kuwa kwamba utachochewa kupanua huduma yako kwa kupania, kama wanavyofanya. (1 Kor. 11:1) Je! ingewezekana kupanua utendaji wako hadi saa 70 kwa mwezi na hivyo kutumika ukiwa painia wa kawaida?

6 Zaidi ya ndugu na dada 17,000 sasa ni wenye kutumikia katika ofisi za tawi na makao ya Betheli kuzunguka ulimwengu. Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 1995 yazungumzia matakwa ili kujaza ombi kwa ajili ya utumishi kama huo. Kwa nini usisome nyongeza hiyo na kuona ikiwa wewe ni mmoja unayeweza kuwa mwenye kustahili kwa ajili ya pendeleo hilo la pekee la utumishi wa Betheli?

7 Tumikia Mahali Ambapo Uhitaji Ni Mkubwa Zaidi: Je! unaishi mahali ambapo eneo latembelewa kwa ukawaida au ambapo kuna ndugu wengi kwa ajili ya kuchangia mzigo? Je! umefikiria kupanua huduma yako kwa kuhamia mahali ambapo uhitaji ni mwingi zaidi? Labda kuhama huko kwaweza kuwa kwenda katika eneo la mashambani la karibu ambapo wafanyakazi zaidi wahitajiwa. (Mt. 9:​37, 38) Hili halipaswi kufanywa bila kufikiriwa kimbele. Jambo hilo lastahili kufikiriwa kwa njia ya sala. (Lk. 14:28-​30) Zungumzia hali yako pamoja na wazee na mwangalizi wa mzunguko. Watafikiri nawe waone ikiwa ni jambo la hekima kufanya uhamaji huo sasa au kujitayarisha kwa ajili ya kufanya hivyo wakati ujao. Ikiwa wataka kuandikia Sosaiti kusudi upate dokezo kuhusu mahali ambapo ungeenda, barua yenye kutiwa sahihi na Halmashauri ya Utumishi wa Kutaniko lako yapaswa kusindikiza barua yako.

8 Fanya Utumishi Wako Uwe Bora: Huenda sote twaweza kushiriki kikamili zaidi katika huduma kwa kufanya utumishi wetu wa shambani uwe bora. Je! wewe washiriki katika pande zote za kazi, kutia ndani ushahidi wa kutoka nyumba hadi nyumba na wa vivi hivi, na kazi ya kufanya ziara za kurudia na kuongoza mafunzo ya Biblia? Ikiwa wewe waongoza funzo, je! waweza kufanya ustadi wako wa kufundisha uwe bora? Ingekuwa vizuri kurudilia nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1996 kwa ajili ya madokezo unayoweza kutumia ili kuchochea wanafunzi wajitoe wakfu na kubatizwa.

9 Njia za kupanua na kufanya huduma yetu iwe bora zazungumziwa kwa kirefu zaidi katika sura 9 ya kitabu Tumefanywa Tengenezo Tutimize Huduma Yetu. Kwa kweli, sisi sote tungepaswa kutaka kufanya mengi zaidi iwezekanavyo katika utumishi wa Mungu. Kwa nini usifikirie kwa makini miradi yako ya kiroho? Fanya kama 1 Timotheo 4:15 linavyopendekeza: “Fikiri kwa uzito juu ya mambo haya; vama katika hayo, ili kusonga mbele kwako kupate kuwa dhahiri kwa watu wote.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine