Je, Unataka Kufanya Mengi Zaidi?
1 Yesu alilinganisha Ufalme na hazina zenye thamani. (Mt. 13:44-46) Ile kazi ya kueneza habari ya Ufalme pia ni hazina yenye thamani. Huduma hiyo inastahili nafasi ya kwanza maishani mwetu, ingawa kushiriki kikamili katika kazi hiyo kunahusisha kiasi fulani cha kujinyima. (Mt. 6:19-21) Je, unataka kufanya mengi zaidi katika utumishi wa Ufalme?
2 Fikiria Mambo Haya ya Lazima: Mambo mengi yanahitajiwa ili kupanua ushiriki wetu binafsi katika huduma: (1) kuazimia kutia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza maishani (Mt. 6:33); (2) kutumikisha imani na kutegemea Yehova (2 Kor. 4:1, 7); (3) kutafuta msaada wa Mungu kupitia sala yenye unyofu na ya kuendelea (Luka 11:8-10); (4) kufuatia mambo na kutenda kulingana na sala zetu.—Yak. 2:14, 17.
3 Njia za Kupanua Huduma Yetu: Sisi sote tunaweza kujiwekea mradi wa kimsingi wa kupitisha kwa ukawaida wakati fulani katika huduma kila mwezi. Lakini je, umekwisha kufikiria pia kutumia kila nafasi inayojitokeza ili kutoa ushahidi wa vivi hivi, kujitahidi kufanya utoaji wako mbalimbali uwe wenye maana zaidi, kuongeza matokeo ya ziara zako za kurudia, na kujitahidi kuongoza mafunzo ya Biblia ya nyumbani yenye kuendelea? Je, unaweza kuwa painia msaidizi au wa kawaida au kutumikia mahali ambapo uhitaji ni mkubwa zaidi? Ikiwa wewe ni ndugu aliyebatizwa, je, unaweza kujitahidi kutimiza sifa ili kuwa mtumishi wa huduma au mzee? (1 Tim. 3:1, 10) Je, unaweza kupanua huduma yako kwa kujaza ombi kwa ajili ya utumishi wa Betheli, Shule ya Mazoezi ya Kihuduma, au mazoezi ya kimishonari kwenye Shule ya Gileadi?—Luka 10:2.
4 Ndugu mmoja aliyekuwa na kazi ya wakati wote na aliyepitisha wakati mwingi katika utendaji mbalimbali wa michezo alitiwa moyo awe painia wa kawaida. Akaanza utumishi wa painia msaidizi na kisha akarekebisha hali zake ili kuanza huduma ya wakati wote. Baadaye akahudhuria Shule ya Mazoezi ya Kihuduma, ambayo ilisaidia kumtayarisha kwa ajili ya mgawo wake wa sasa akiwa mwangalizi msafiri. Yeye ni mwenye furaha sana kuona aliitikia kitia-moyo alichopewa, naye ana uhakika kwamba yeye ni mwenye furaha zaidi kutokana na uamuzi wake wa kufanya mengi zaidi katika utumishi wa Ufalme.
5 Yehova hubariki wale wanaojitoa. (Isa. 6:8) Usiache kitu chochote kikuzuie usipanue huduma yako na kupata kutosheka kwingi hata zaidi na burudisho kutokana na jambo hilo.