Sisi Tunafundishwa na Yehova
1 Programu ya ulimwenguni pote ya elimu ni yenye kufanya kazi katika mabara 233 chini ya uongozi wa Kimungu. Hakuna kitu kinachoweza kulingana na hiyo, ambacho ulimwengu huu waweza kutoa. Mfunzi wetu Mtukufu, Yehova, ni mwenye kutufundisha jinsi ya kujipatia faida sasa kadiri anavyotuelimisha pia kwa ajili ya uhai udumuo milele.—Isa. 30:20; 48:17.
2 Shule za Elimu ya Kimungu: Fikiria shule zinazoendelea sasa kwa faida ya watu wa Yehova. Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, inayoongozwa kila juma katika makutaniko 87,000 hivi, inazoeza mamilioni ya wahubiri wa Ufalme ili wawe wahudumu wa habari njema wenye matokeo. Je! wewe umejiandikisha kwenye shule hiyo? Je! wewe ni mmoja wa yale maelfu yaliyohudhuria Shule kwa Ajili ya Utumishi wa Painia? Labda kiwango cha saa kilichopunguzwa kitawezesha watu wengi zaidi kuwa mapainia na kujifanya wawe wenye kustahili ili kuhudhuria shule hiyo. Ile Shule ya Mazoezi ya Kihuduma ya miezi miwili, ambayo sasa huongozwa katika lugha kubwa kuzunguka ulimwengu, ni yenye kuwapa vifaa wazee na watumishi wa huduma waseja ili wachukue madaraka makubwa zaidi ya kitheokrasi. Mara kwa mara, wazee na watumishi wa huduma hupata maagizo ya pekee katika Shule ya Huduma ya Ufalme.
3 Majengo ya Kitovu cha Elimu cha Watchtower katika Patterson, New York, ni yenye kutumiwa ili kupokea shule tatu za pekee, zinazoandaa mazoezi ya kitheokrasi yenye kuendelea. Yale masomo ya miezi mitano ya Shule ya Biblia ya Gileadi ya Watchtower inatayarisha wahudumu kwa ajili ya kazi ya kimishonari katika mashamba ya nchi za kigeni. Washiriki wa Halmashauri ya Tawi kutoka ulimwenguni pote wanahudhuria masomo ya miezi miwili kuhusu namna ya kuendesha kazi katika matawi. Mnamo Mei 1999, masomo mapya ya miezi miwili kwa ajili ya waangalizi wasafiri yalianza na darasa la wanafunzi 48 kutoka Shirikisho la Amerika na Canada. Mwishowe, watumishi wa Yehova wote hupata faida bora kutokana na mazoezi anayoyaandaa Yehova kupitia shule hizo mbalimbali.
4 Tunafundishwa kwa Kusudi Gani? Mshiriki mmoja wa Baraza Linaloongoza alisema: “Programu yetu ya kielimu ya wakati huu imekusudiwa kuleta watu wote wa Yehova kila mahali kwenye ile hali bora ya ukomavu inayofafanuliwa kwenye Mithali 1:1-4.” Yehova na aendelee kumpa kila mmoja “ulimi wa wale wanaofundishwa.”—Isa. 50:4.