Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/99 uku. 7
  • Je! wewe unapanga kuhama?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je! wewe unapanga kuhama?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna ya Kuzoea Kutaniko ya Mupya
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Namna Gani Unaweza Kuzoea Kutaniko Lako la Mupya?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2017
  • Uko wa Maana Sana mu Kutaniko la Yehova!
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Namna Kutaniko Inapangwa
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 10/99 uku. 7

Je! wewe unapanga kuhama?

Wakati jibu kwa ulizo hilo ni ndiyo, kuna mambo mengi ambayo wewe na wengine mnahitaji kuchukua hatua ya kufanya. Kwa kufuata hatua za msingi zinazoonyeshwa hapa chini, utajulikana haraka zaidi katika kutaniko lako jipya.

(1) Ukikwisha tu kujua mahali unapohamia, mwandishi wa sasa wa kutaniko lako anaweza kupata anwani ya Jumba la Ufalme la kutaniko lako jipya. Unapofika mahali hapo, tafuta mara moja jumba na upate uhakikisho kuhusu saa za mikutano. Ikiwa makutaniko mengi yanatumia Jumba la Ufalme, omba wazee wakujulishe ni katika eneo la kutaniko gani ambamo wewe unaishi. Usikawie kuhudhuria mikutano na kujuana na wazee wa mahali.

(2) Mwandishi wa kutaniko lako la sasa na yule wa kutaniko lako jipya watashirikiana katika kuhamisha kadi za maandishi ya mhubiri kwa ajili yako na kwa ajili ya familia yako. Barua ya kutambulisha itatumwa pia kwa wazee wa kutaniko lako jipya. (Ona barua ya Juni 1, 1999 kwa mabaraza yote ya wazee, na Majibu ya Maulizo Yenu katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai 1991.) Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko ya huko ingepaswa kujulisha kiongozi wa funzo la kitabu kuhusu kufika kwako ili akutane nawe na kukusaidia upate sehemu yako mpya ya funzo la kitabu.—Rom. 15:7.

(3) Wahubiri wote katika kutaniko lako jipya wanalo daraka lenye kufurahisha la kutimiza—lile la kujuana nawe ili kukufanya ujisikie mwenye kukaribishwa. (Linganisha 3 Yohana 8.) Bila shaka, hilo linamaanisha kwamba unapaswa kuwa kwenye mikutano ili kufurahia badilishano lenye kutia moyo na lenye kujenga pamoja na akina ndugu na dada.

(4) Wewe haungepaswa kungoja hadi kazi yote inayohusika katika kuhama imalizike ili kushiriki katika huduma ya shambani pamoja na kutaniko lako jipya. Kadiri unavyotia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza, mambo mengine yatashughulikiwa, na utajisikia mwenye kutulia katika mazingira yako mapya. (Mt. 6:33) Wakati utakapokaa katika nyumba yako mpya, yaelekea utataka kualika wengine katika kutaniko wakutembelee na kujuana nawe vizuri zaidi.—Rom. 12:13b.

Kuhama ni mradi mkubwa. Hata hivyo, wakati kila mmoja anayehusika anafanya lile linaloombwa, hakutakuwa kushuka kiroho. Wote wataguswa moyo ifaavyo na udugu wetu wa Kikristo wenye upendo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine