Igeni Yehova kwa kutokuwa na upendeleo
1 Yehova hupendezwa na watu. Bila upendeleo, yeye hukubali kila mtu anayefanya mapenzi yake. (Mdo. 10:34, 35) Wakati Yesu alipohubiria watu, yeye pia hakuwa na upendeleo. (Luka 20:21) Tunahitaji kuiga mfano wao, kama alivyofanya Paulo, ambaye aliandika: “Kuna Bwana yuleyule juu ya wote, aliye tajiri kwa wote wale wanaomwita.”—Rom. 10:12.
2 Kutangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu kwa wote tunaokutana nao huleta “sifa kwa Mungu.” Tunapaswa kuendelea kushiriki ujumbe huu mzuri ajabu na watu wote, bila kujali rangi yao ya ngozi, cheo chao katika jamii, elimu, msimamo wa kifedha, au umashuhuri. (Rom. 10:11-13) Hilo linamaanisha kuhubiria wale wote watakaosikiliza—wanaume, wanawake, vijana, na wazee. Tunahitaji kwenda kwenye kila mlango ili kutolea kila msikilizaji nafasi ya kusikia kweli.
3 Pendezweni na kila mtu: Mradi wetu ni kukutana na kila mtu iwezekanavyo. Wakiwa na jambo hilo akilini, wahubiri fulani wamekuwa wenye matokeo katika kutoa ushahidi kwa watu katika ofisi za madaktari, hospitali, nyumba za kutunzia wale walio katika hali dhaifu, ofisi za kusaidia maskini, na mashirika ya kurudishia watu sifa nzuri. Kwa kuongezea, wahubiri wametoa ushahidi kwa watu walio na kazi ya kutayarisha mazishi, wasimamizi na washauri wa shule, na mahakimu. Wakati tunapokaribia maofisa, ni jambo lenye kufaa kuonyesha uthamini kwao kwa utumishi wenye kusaidia wanaotoa katika jamii. Iweni wenye adabu, na mchague makala yenye kutokea pa wakati wenye kufaa ambayo yanazungumzia kipekee aina yao ya kazi na matatizo yanayohusiana na kazi hiyo.
4 Katika kisa kimoja, dada alijitahidi kuzungumza na hakimu mmoja katika ofisi yake. Baada ya mazungumzo yenye shauku, hakimu huyo akasema: “Je! wajua kinipendezacho juu ya Mashahidi wa Yehova? Wana kanuni zenye msingi mzuri ambazo wao hushikilia kabisa.” Ushahidi mzuri ulitolewa kwa mtu huyo mwenye uvutano.
5 Hatuwezi kusoma katika mioyo ya watu. Walakini, kwa kuzungumza na kila mtu tunayekutana naye, tunaonyesha imani yetu katika uwezo wa Mungu wa kuongoza kazi yetu. Kwa kuongezea, hilo linawapa pendeleo la kusikia na kuitikia ujumbe wa tumaini. (1 Tim. 2:3, 4) Acheni tutumie wakati wetu kwa hekima na tujitahidi kuiga Yehova kwa kutokuwa na upendeleo, kwa kufikisha habari njema kwa watu wote iwezekanavyo.—Rom. 2:11; Efe. 5:1, 2.