Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/00 uku. 8
  • Jinsi ya kusitawisha uwezo wa kufikiri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Jinsi ya kusitawisha uwezo wa kufikiri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Je, Unatumia Kitabu Kutoa Sababu?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 2/00 uku. 8

Jinsi ya kusitawisha uwezo wa kufikiri

1 Maana moja ya neno “kufikiri” ni “kusema na mtu mwingine kiasi cha kwamba unakuwa na uvutano juu ya matendo na maoni yake.” Ili kufanya matokeo yako katika huduma yawe bora, unahitaji kusitawisha uwezo wa kufikiri na watu unaokutana nao. (Mdo. 17:2-4) Lakini unawezaje kusitawisha ufundi huo?

2 Huo huanza na kutafakari: Wakati unapojifunza kweli za Biblia, utaona kuwa jambo lenye kusaidia kufikiri juu ya kweli hizo. Ikiwa sehemu fulani zinaonekana kuwa ngumu kidogo, chukua wakati wa kufanya utafiti na kutafakari majibu. Tafuta kuelewa waziwazi mafasirio yanayotolewa, na pia sababu za Kimaandiko za mafasirio hayo.

3 Kujitayarisha kwa ajili ya huduma kunahusika: Fikiri juu ya jinsi ungeweza kufasiri kweli kwa aina mbalimbali za watu. Tunga ulizo lenye kuchochea kufikiri ili kuamsha kupendezwa. Amua jinsi ya kuliunganisha na wazo la Kimaandiko na ufikiri juu ya hilo. Fikiria kimbele vipingamizi vinavyoweza kutokezwa, na ufikiri kuhusu jinsi ya kuvizungumzia. Katika kichapo kinachopendekezwa, chagua wazo kuu linaloweza kutumika vizuri zaidi.

4 Fuata kielelezo cha Yesu: Yesu alitoa kielelezo kizuri zaidi cha kufikiri kwa matokeo kwa kutumia Maandiko. Ili kuchanganua jinsi alivyofundisha, fikiria simulizi linalopatikana kwenye Luka 10:25-37. Ona hatua zifuatazo: (1) Ongoza uangalifu kwenye Maandiko wakati wa kujibu maulizo ya watu. (2) Waalike watoe maoni yao, na uwapongeze wakati wanapotoa maelezo yenye akili. (3) Hakikisha kwamba uhusiano kati ya ulizo na Maandiko unaendelea kukaziwa. (4) Tumia mfano wenye kuvutia moyo ili kuwa hakika kwamba maana ya kweli ya jibu yanaeleweka.—Ona Mnara wa Mlinzi wa Kifaransa wa Machi 1, 1986, kurasa 27-8, mafungu 8-10.

5 Tumia kifaa tulichotolewa: Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko kilitangazwa kikiwa kitabu cha mkononi kwa ajili ya huduma ya shambani. Utangulizi wake mbalimbali, majibu kwa vizuia-mazungumzo vinavyoweza kutokea, nukta kwa ajili ya kutoa sababu vinatusaidia kusitawisha uwezo wa kufikiri. Kitabu Kutoa Sababu ni kifaa chenye thamani ambacho tungepaswa kuchukua sikuzote katika utumishi, na hatungepaswa kamwe kusita kukitumia wakati tunaposhiriki mazungumzo ya Biblia. Rudilia kurasa 7-8 za kitabu hicho ili kuona jinsi ya kukitumia kwa faida kubwa zaidi.

6 Kusitawisha uwezo wako wa kufikiri kutaongeza ufundi wako katika kazi ya kuhubiri na kufundisha. Hilo litatokeza baraka tele kwako na kwa wale unaokutana nao katika huduma.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine