Je, Unatumia Kitabu Kutoa Sababu?
1. Ni njia gani ambayo mtume Paulo na Yesu walitumia ili kufundisha wengine?
1 Mtume Paulo alijikaza ‘kujadiliana na watu kwa kutumia Maandiko.’ (Mdo. 17:2, 3; 18:19) Kwa kufanya hivyo, alimwiga Yesu, ambaye mara nyingi alitaja Maandiko na kutumia mifano ili kusaidia wasikilizaji wake waelewe mapenzi ya Mungu. (Mt. 12:1-12) Kitabu Kutoa Sababu kimetayarishwa ili kutusaidia kufanya vivyohivyo.
2. Namna gani unaweza kutumia kitabu Kutoa Sababu ili kutayarisha maneno ya utangulizi yenye matokeo mazuri?
2 Namna ya Kutayarisha Maneno ya Utangulizi Yenye Matokeo Mazuri: Kwenye ukurasa wa 9-15 wa kitabu Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko kuna maneno ya utangulizi yenye kuchochea mutu apendezwe. Kujifunza na kutumia maneno mbalimbali ya utangulizi, zaidi sana ikiwa eneo linahubiriwa kwa ukawaida, kutakusaidia kutumia ufundi mbalimbali katika kazi ya kuhubiri, kuwa mwenye kujiambatanisha na hali na kuwa na uwezo wa kuanzisha mazungumzo. Unaweza kusoma maneno ya utangulizi moja kwa moja katika kitabu unapohubiri kwa kutumia telefone ao unapozungumza na mutu kwenye telefone ya mlangoni katika majengo yenye ulinzi mkali.
3. Ni mapendekezo gani yanayopatikana kwenye ukurasa wa 16-24 wa kitabu Kutoa Sababu ambayo yatakusaidia katika kazi ya kuhubiri?
3 Namna ya Kushinda Vizuia-Mazungumzo: Unaweza kufikiria mbele ya wakati vizuia-mazungumzo vinavyoweza kutokea katika eneo na kuchukua dakika chache mbele ya kwenda kwenye mahubiri ili kuchunguza ukurasa wa 16-21 wa kitabu hicho kusudi upate mapendekezo kuhusu jinsi ya kujibu. Je, wasikilizaji fulani wanaweza kuwa Wabudha, Wahindu, Wayahudi ao Waislamu? Ikiwa ndivyo, habari iliyo kwenye ukurasa wa 21-24 inaweza kusaidia.
4. Namna gani tunaweza kutumia kitabu Kutoa Sababu ikiwa mutu anatokeza ulizo ao habari inayoleta ubishi?
4 Namna ya Kujibu Maulizo: Kitabu Kutoa Sababu kinaweza pia kutusaidia ikiwa mutu anauliza ulizo ao kutokeza habari inayoleta ubishi. Unaweza tu kumwambia mutu kwamba ungependa kumwonyesha jambo fulani lenye kupendeza kuhusiana na habari hiyo na kamata kitabu chako Kutoa Sababu. Kwa kuwa habari zinaonyeshwa kufuatana na herufi za alfabeti, fungua kwenye ukurasa ulio na kichwa kikuu ambacho unafikiri kina habari unayotafuta. Kisha, tupia jicho kwenye maulizo yenye kuandikwa kwa herufi nzito. Ikiwa hauone kwa haraka habari unayotafuta, fungua fahirisi iliyo kwenye kurasa za mwisho. Unapopata tu habari yenye kufaa, uisome moja kwa moja katika kitabu. Ikiwa munazungumzia andiko fulani, unaweza kupata habari unayotafuta kwenye ukurasa wa 445 chini ya kichwa “Maandiko Ambayo Mara Nyingi Hutumiwa Kimakosa.”
5. Kitabu Kutoa Sababu kinaweza kutumiwa kwa namna gani zingine zenye kufaidi?
5 Namna Zingine za Kutumia Kitabu Hicho: Watu fulani wanachunga kitabu Kutoa Sababu mahali pao pa kazi ao kwenye masomo ili kiwasaidie kujibu maulizo kama vile, ‘Kwa nini hamuazimishe sikukuu?’ Vijana wamepata habari zenye kusaidia chini ya vichwa “Uumbaji” na “Mageuzi” ili kutayarisha kazi zao za masomo (devoirs). Ikiwa unaenda kumtembelea mutu fulani aliye mgonjwa ao ambaye amefiwa na mpendwa wake, habari iliyo chini ya kichwa “Kitia-Moyo” inaweza kukusaidia umufariji kupitia Maandiko. Pia, kitabu Kutoa Sababu kina habari zenye kusaidia kwa ajili ya wale wanaotayarisha hotuba na wale wanaoongoza mikutano ya utumishi wa shambani.
6. Kusudi letu ni nini tunapohubiri?
6 Tunapohubiri, kusudi letu si kutafuta ushindi katika kubishana na watu; wala si kupasha tu watu habari. Tunataka kufikiri na watu kwa ufundi kupitia Maandiko. Tunapotumia vizuri kitabu Kutoa Sababu, tunaonyesha kwamba tunafikiria kwa uangalifu namna yetu ya kufundisha.—1 Tim. 4:16.