Omba msaada
1 Maneno yenye kupuliziwa “ngumu kushughulika nazo” yanatoa maelezo ifaavyo kuhusu nyakati zetu za hatari. (2 Tim. 3:1) Kwa sababu hiyo, unaweza kufanya nini wakati unapokutana na matatizo makali ya kiroho ambayo unaweza kujisikia kuwa mwenye kukosa vifaa ili kukabiliana nayo?
2 Je, wewe ni tayari kuzungumza na mshiriki wa kutaniko mwenye kukomaa kiroho? Mtu fulani anaweza kusita kwa sababu ya kutojua la kufanya, akiwa asiyetaka kulazimisha, au akishakia ikiwa kuna yeyote anayeweza kusaidia kwelikweli. Bila shaka, tunapaswa kujitahidi kushughulikia madaraka yetu ya kibinafsi vizuri zaidi iwezekanavyo, lakini tungepaswa kujisikia huru sikuzote kutafuta msaada katika mambo yanayohusisha hali yetu ya kiroho.—Gal. 6:2, 5.
3 Mahali pa kuanzia: Unaweza kutaka kumkaribia kiongozi wako wa funzo la kitabu na kuuliza ikiwa unaweza kutumika naye katika utumishi wa shambani. Hilo litakutolea nafasi ya kumjulisha tamaa yako ya kukua kiroho. Ikiwa yeye ni mtumishi wa huduma, mjulishe kwamba unahitaji msaada wa kiroho, naye ataomba wazee wakusaidie. Au unaweza kumkaribia yeyote kati ya wazee ili kuzungumzia mambo yenye kukuhangaisha.
4 Ni msaada wa aina gani unaohitaji? Je, jambo fulani limepunguza bidii yako? Je, wewe ni mzazi mwenye kulea watoto peke yako huku ukijaribu kuwalinda wakiwa karibu na kutaniko? Je, wewe ni mtu mzee-mzee anayehitaji msaada? Au je, kuna tatizo fulani linalokuvunja moyo? Kushughulika na nyakati zetu za hatari kunaweza kuwa jambo gumu—lakini si jambo lisilowezekana. Msaada unapatikana.
5 Jinsi wanaume wazee wanavyosaidia: Wazee hujali kwelikweli. Watasikiliza mahangaiko yako. Ikiwa wahubiri wengine wanapambana na vizuizi vilevile, wazee watafikiria hilo kadiri wanavyochunga na kufundisha kutaniko. Wakiwa “mifano ya kuiga kwa kundi,” wao hubaki tayari kutumika pamoja nanyi kwa furaha. (1 Pet. 5:3, ZSB) Kusikiliza akina ndugu hao wenye ujuzi wakati wanapofikiri juu ya kanuni za Biblia kunaweza kufanya huduma yako iwe bora na kukusaidia katika maisha yako binafsi.—2 Tim. 3:16, 17.
6 Yesu ametutolea kwa wingi “zawadi [zikiwa] wanaume.” (Efe. 4:8) Hilo lamaanisha kwamba wazee wako hapo ili kukusaidia. Wako tayari kukusaidia. Kwa kweli, wao ‘ni vitu vyako.’ (1 Kor. 3:21-23) Kwa hiyo, badala ya kurudi nyuma, uwe huru kutoa maoni yako. Omba msaada unaouhitaji.