Kujifunza Unabii wa Danieli
1 Kuanzia juma la Aprili 17, tutajifunza kitabu Sikiliza Unabii wa Danieli! katika Funzo la Kitabu la Kutaniko. Wengi wamekwisha kusoma kitabu hicho chenye kuvutia sana, lakini sasa tuna nafasi ya kufurahia faida zinazotokana na kujifunza habari hiyo katika kikundi. Wahubiri wote, wale wenye kupendezwa, na watoto wote wanaalikwa, ndiyo, wanatiwa moyo, kuwako kila juma kwa ajili ya funzo hilo kamili la kitabu cha Biblia cha Danieli.—Kum. 31:12, 13.
2 Programu ya funzo na maagizo: Programu kamili ya funzo la kitabu Unabii wa Danieli inatolewa katika toleo hili la Huduma Yetu ya Ufalme. Hakikisha kwamba unaweka kopi ya programu hiyo katika kitabu chako cha funzo. Programu hiyo inaonyesha sura na mafungu kutoka katika kitabu hicho, na pia maandiko kutoka Danieli, vitakavyozungumziwa katika funzo la kila juma. Vielezi-chini vinaeleza jinsi na wakati wa kujifunza habari fulani katika kitabu hicho. Mwishoni mwa funzo la kila juma, kiongozi anatiwa moyo kukagua pamoja na kikundi maandiko fulani kutoka Danieli, maandiko yenye kuorodheshwa kwenye programu ya juma hilo. Kadiri wakati unavyoruhusu, maandiko hayo yanaweza kusomwa au kuelezwa. Maandiko fulani yataendelea kutoka juma moja hadi juma lingine kwa sababu ya kuchunguzwa kwenye kuendelea kwa matumizi yake.
3 Jitayarishe kwa ajili ya funzo kamili: Jitihada imefanywa ili kuwezesha kuwe wakati wa kutosha kila juma kwa ajili ya funzo lisilo la haraka-haraka la habari iliyotolewa kuwa mgawo. Masomo manne ni mafupi. Kwa sababu hiyo, mwishoni mwa funzo la juma la Juni 5, kiongozi anaweza kutia ndani kujikumbusha Danieli 2:1-40. Mnamo juma la Juni 26, yeye anaweza kurudilia Danieli 3:1-30. Juma la Septemba 4 linapaswa kutia ndani mazungumzo kamili juu ya picha na maandiko kwenye ukurasa 139. Ramani kwenye kurasa 188 na 189 inapaswa kuzungumziwa kwenye funzo la juma la Oktoba 2.
4 Jitayarishe vizuri kwa ajili ya funzo kila juma, na ufurahie kushiriki katika hilo. Thamini pendeleo lako la kushirikiana na tengenezo la Yehova linaloonekana na kufaidika na ufahamu wenye kina na uelewevu unaotolewa na watiwa mafuta wake waaminifu. (Dan. 12:3, 4) Kwa upole, tia wengine moyo wahudhurie funzo la kitabu kikawaida. Acheni sisi sote tusikilize neno la Mungu la kiunabii kadiri linavyofunuliwa katika kitabu cha Danieli chenye kuogopesha.—Ebr. 10:23-25; 2 Pet. 1:19.