Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 5/00 uku. 1
  • “Fulizeni kuwa macho”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Fulizeni kuwa macho”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tuendelee Kutambua Uhitaji Wa Kutenda Kwa Haraka
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Tuwasaidie Watu ‘Waamuke Kutoka Katika Usingizi’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Sababu Gani Tunapaswa ‘Kuendelea Kukesha’?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Unapaswa Kufanya Nini ili Uendelee Kutambua Lazima ya Kuhubiri kwa Haraka?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 5/00 uku. 1

“Fulizeni kuwa macho”

1 Baada ya kueleza habari kuhusu matukio ya maana ambayo yangekuwa alama ya siku za mwisho za mfumo huu wa mambo, Yesu alihimiza wanafunzi wake ‘wafulize kuwa macho.’ (Mk. 13:33) Kwa nini Wakristo wanapaswa kufuliza kuwa macho? Kwa kuwa tunaishi wakati wa hatari zaidi katika historia ya kibinadamu. Hatuwezi kuwa wenye kusinzia kiroho bila hasara yoyote. Jambo hilo lingetufanya tukose kuthamini kazi ambayo Yehova ametutolea kufanya katika wakati huu wa mwisho. Hiyo ni kazi gani?

2 Yehova ni mwenye kufanya watu wake watangaze ulimwenguni pote habari njema kuhusu Ufalme wake​—tumaini pekee kwa wanadamu. Kutumika kwetu kwa ukaribu na tengenezo la Yehova hututambulisha kuwa Wakristo wa kweli, wanaoelewa nyakati na uhitaji wa kusaidia wengine wasikie “semi za uhai udumuo milele.” (Yn. 6:​68) Kwa kushiriki kwa bidii katika kazi hiyo ya maana sana, tunatoa uhakikisho wa kuwa macho kiroho.

3 Wenye Kuchochewa Kuhubiri: Tukiwa Mashahidi wa Yehova, tunapaswa kuwa na maoni yenye kufaa kuhusu huduma yetu. Upendo kwa Yehova na kwa jirani hutuchochea kibinafsi kushiriki katika kazi ya kuhubiri. (1 Kor. 9:​16, 17) Kwa kufanya hivyo, tutajiokoa sisi wenyewe na wale wanaotusikiliza pia. (1 Tim. 4:​16) Acheni liwe azimio letu kushiriki kwa ukawaida iwezekanavyo na kwa wakati mrefu kama inavyohitajiwa katika kuhubiri kuhusu serikali bora zaidi ambayo wanadamu watapata kuwa nayo​—Ufalme wa Mungu!

4 Uharaka wa huduma yetu unakaziwa juu yetu na jambo la maana​—mwanzo wa dhiki kubwa utatokea huku tukiwa bado wenye kujitoa katika kazi hii. Kutojua kwetu siku na saa kunaomba tufulize kulinda na kuwa tayari wakati wote, tukitegemea Yehova kwa njia ya sala. (Efe. 6:​18) Ukubwa wa kazi ya kuhubiri unaendelea kuongezeka. Lakini siku moja karibuni, kazi kubwa zaidi ya kutoa ushahidi katika historia ya kibinadamu itafikia mwisho wake.

5 Fuateni kwa uaminifu amri ya Yesu ya ‘kufuliza kuwa macho.’ Hilo ni jambo la maana zaidi sasa kuliko wakati mwingine wowote. Acheni tuitikie tukiwa wenye kuelewa hali ya uharaka. Leo na kila siku, acheni tubaki wenye kiasi kiroho, walio macho, na wenye kutenda katika utumishi wa Yehova. Ndiyo, acheni ‘tukae macho na kutunza hisi zetu.’​​—1 Thes. 5:6.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine