Kisanduku Cha Maulizo
◼ Je, kutaniko liwe na ramani (carte) kamili ya eneo layo iliyowekwa mahali palipo wazi katika Jumba la Ufalme?
Ndiyo, ramani kamili ya eneo inapaswa kuwekwa katika fremu (cadre) na iwekwe wazi kwenye ukuta katika Jumba la Ufalme. Ramani hiyo isiwekwe kwenye ubao wa matangazo. Inapaswa kuonyesha mipaka yote ya eneo la kutaniko na mipaka ya kila eneo mojamoja likiwa na namba yake. Mipaka ya maeneo ya makutaniko yote yanayotumia Jumba la Ufalme lilelile inapaswa kuonyeshwa. Hiyo itasaidia wahubiri na wale wanaopendezwa vilevile wajue wanaishi katika eneo la kutaniko gani. Kuonyesha sehemu za Funzo la Kitabu la Kutaniko kwenye ramani pia kutasaidia wote wajue mahali funzo la kitabu walilogawiwa linapopatikana. Ramani hiyo inapaswa kuonyesha mambo yote (kama vile majina au mipaka) kulingana na jinsi yalivyo kwa sasa.
Kuonyesha ramani hiyo ni kikumbusha kwa wahubiri wote kwamba, ikiwezekana, ingekuwa vizuri kuwa na mgawo wako wa eneo la kibinafsi. Ramani inasaidia wale wanaotaka kuchagua eneo lililo karibu na nyumbani kwao. Huenda ikasaidia kuokoa wakati wa mikutano ya utumishi, ikimwezesha kiongozi aelekeze bila kukawia kila kikundi cha wahubiri kwenye eneo ambalo wamegawiwa kuhubiri.
Pia ramani hiyo inatoa uthibitisho kwamba kutaniko lina mpango wa kuhubiri ujumbe wa Ufalme kikamili katika eneo lake.—Luka 9:6.